Tuesday, December 5, 2017

Waziri Mahiga amuaga balozi wa U.A.E aliyemaliza muda wake wa uwakilishi nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiongea na Balozi wa Umoja wa Falme za Kiarabu nchini (U.A.E), Mhe Abdulla Ibrahim Alsuwaidi alipomtembelea katika ofisi za Wizara Jijini Dar es Salaam tarehe 05 Disemba 2017.

Mhe. Abdulla Ibrahim Alsuwaidi amemaliza muda wake wa uwakilishi hapa nchini ambapo pamoja na mambo mengine Waziri Mahiga amemshukuru kwa ushirikiano mzuri aliouonyesha alipokuwa nchini. Pia amemtakia safari njema na utekelezaji mwema wa majukumu mapya atakayopangiwa.

Mhe. Abdulla Ibrahimu Alsuwaidi akitoa neno la shukrani kwa Mhe. Waziri Mahiga ambapo alitumia fursa hiyo kutoa shukrani kwa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Serikali ya Jamhuri ya Muungano kwa ujumla kwa kumwezesha kutekeleza vema majukumu yake katika muda wake wote wa uwakilishi hapa nchini. Pia akaahidi U.A.E itaendeleza kudumisha ushirikiano wa kidiplomasia pamoja na ushirikiano katika sekta za miradi ya maendeleo.

Mazungumzo yakiendelea.

Waziri Mahiga akimuga Balozi wa U.A.E aliyemaliza muda wake wa Uwakilishi nchini.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.