Wednesday, September 1, 2021




Umoja wa Mataifa umetangaza nafasi ya kazi ya Katibu Mkuu Msaidizi atakayeshughulikia masuala ya Amani (Assistant Secretary General for Peacebuilding Support). Fursa hii iko wazi kwa nchi wanachama wote wa Umoja wa Mataifa. 


Maelezo zaidi ya nafasi hiyo na jinsi ya kuwasilisha maombi yanapatikana kupitia  ukurasa wa Tovuti ya Umoja wa Mataifa wa https://www.un.org/peacebuilding/supportoffice.
 
Mwisho wa kupokea maombi hayo ni tarehe 20 Septemba 2021.

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki inawahimiza Watanzania wenye sifa kuomba nafasi hiyo.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.