Wednesday, September 1, 2021

BALOZI SOKOINE AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA CANADA NCHINI


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine, leo terehe 1 Septemba 2021 amekutana na kufanya mazungumzo na Mhe. Pamela O’Donnell Balozi wa Canada nchini Tanzania, yaliyofanyika jijini Dodoma. 

Katika mazungumzo hayo Balozi Sokoine na Balozi Pamela O’Donnell wamejadili masuala mbalimbali muhimu katika kudumisha na kuboresha mahusiano ya kidiplomasia na ushirikiano katika masuala ya uchumi baina ya Tanzania na Canada. Kwa kipindi cha takribani miongo sita mahusiano ya Tanzania na Canada yamejikita katika maeneo mbalimbali ya kiuchumi na kijamii kama vile maendeleo ya viwanda, afya, kuendeleza rasilimali watu, ujenzi wa miundombinu na uboreshaji wa mazingira. 

Tanzania ilianzisha mahusiano ya kidiplomasia na Canada mwaka 1961 mara baada ya uhuru. 
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo na Balozi wa Canada nchini Tanzania Mhe. Pamela O’Donnell yaliyofanyika katika Ofisi ya Wizara jijini Dodoma.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine na Balozi wa Canada nchini Tanzania Mhe. Pamela O’Donnell wakijadili jambo walipokutana kwa mazungumzo jijini Dodoma.
Balozi wa Canada nchini Tanzania Mhe. Pamela O’Donnell akielezea jambo kwenye mazungumzo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine. 

Mazungumzo yakiendelea

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.