Wednesday, September 15, 2021

UFARANSA KIUANZISHA SAFARI YA NDEGE KUJA ZANZIBAR

Na Mwandishi Wetu, Dar

Serikali ya Ufaransa kupitia Shirika lake la ndege ‘Fance Airline’ inategemea kuanzisha safari mpya ya ndege kutoka Ufaransa moja kwa moja hadi Zanzibar kuanzia 19 Oktoba 2021.

Hayo yamebainishwa na Balozi Mteule wa Ufaransa hapa nchini Mhe. Nabil Hajlaouvi wakati alipokuwa anawasilisha nakala ya Hati za utambulisho kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Balozi Nabil amemhakikishia Mhe. Waziri Mulamula kuwa Airfance inaanzisha safari ya ndege ya moja kwa moja kutoka Ufaransa kuja Zanzibar –Tanzania ambapo katika uzinduzi wa safari hiyo utaongozwa na Waziri wa mambo ya Nje uwa Ufaransa tarehe 19 Oktoba 2021.

Pia Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amepokea nakala ya Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi mteule wa Somalia hapa nchini mhe. Zahra Ali Hassan ambapo pamoja na mambo mengine, Balozi Zahra amemhakikishia Waziri Mulamula kuwa Somalia itaendelea kuhakikisha kuwa mahusiano yake na Tanzania yanazidi kuimarika.

Katika tukio jingine, Balozi Mulamula amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Umaja wa Ulaya hapa nchini mhe. Manfredo Fanti wamejadiliana masuala mbalimbali ya ushirikiano katika sekta mbalimbali ikiwemo miundombinu pamoja ufadhili wa miradi mbalimbali ya maendeleo hapa nchini.

Balozi Mulamula pia amekutana na kufanya mazungumzo baadhi ya Mabalozi wa nchi za Nordic hapa nchini ambao ni Balozi wa Denmark, hapa nchini Mhe. Mette Norgaard Dissing-Spandet, Balozi wa Norway hapa nchini, Mhe. Elisabeth Jacobsen, Balozi wa Sweden hapa nchini Mhe. Anders Sjoberg

Kwa upande wake Balozi wa Denmark, hapa nchini Mhe. Mette Norgaard Dissing-Spandet amemhakikishia Waziri Mulamula kuwa pamoja na kuwa Denmark imesema kuwa itafunga ubalozi wake hapa nchini ifikapo 2024, bado nchi hiyo itaendelea kushirikiana kwa karibu na Tanzania na katika kukuza miradi mbalimbali ya maendeleo iliyopo baina ya mataifa hayo kwa maslahi mapana ya pande zote mbili.

Aidha, Waziri Mulamula amekutana kwa mazungumzo na Balozi wa Norway hapa nchini, Mhe. Elisabeth Jacobsen, Balozi wa Sweden hapa nchini Mhe. Anders Sjoberg ambapo viongozi hao wamejadiliana masuala mbalimbali ya kukuza na kuendeleza uhusiano wa kidiplomasia uliopo baina ya Tanzania na mataifa yao.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula akimsikiliza Balozi Mteule wa Ufaransa hapa nchini Mhe. Nabil Hajlaouvi mara baada ya kuwasilisha nakala ya Hati za utambulisho katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam



 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.