Thursday, February 28, 2019

Prof. Kabudi akutana na viongozi mbalimbali wakati wa kikao cha 40 cha Baraza la Haki za Binadamu la UN

Waziri wa Katiba na Sheria ambaye pia ni Kiongozi wa Ujumbe wa Tanzania katika Kikao cha 40 cha Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi (wa tatu kushoto) akizungumza na Kamishna wa Haki za Biandamu, Bi. Michelle Bachelet (mwenye miwani kulia) kuhusu masuala ya haki za binadamu. Wakati wa mazungumzo yao, Bi. Bachelet aliipongeza Serikali ya Awamu ya Tano kwa kupambana na rushwa, kupigia hatua za maendeleo ya kiuchumi, kuendelea kuwahifadhii wakimbizi na ushiriki katika ulinzi wa amani barani Afrika. Kwa upande wake, Prof. Kabudi alisema Tanzania itaendeea kulinda Haki za Binadamu kwa wananchi wote na kuahidi kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na Ofisi ya Kamishna huyo.
Mhe. Prof. Kabudi na ujumbe wake wakiwa katika picha ya pamoja na Bi. Michelet.
Mhe. Prof. Kabudi akiwa katika picha ya pamoja na Bw. Hassan Shire, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi isiyo ya kiserikali ya Defenddeffenders mara baada ya mazungumzo kati yao. Pamoja na mambo mengine mazungumzo yao yalijikita kwenye masuala yanayohusu haki za binadamu ambapo, Mhe. Prof. Kabudi aliishauri taasisi hiyo ambayo inajishughulisha na masuala ya haki za binadamu  kujikita katika kufanya tafiti ili kuandaa taarifa za uhakika kuhusu nchi za Afrika ikiwemo Tanzania zinavyotekeleza haki za binadamu. 
Mhe. Prof. Kabudi ( wa tatu kushoto) na ujumbe wake wakiwa katika picha ya pamoja na Bw. Shire (wa nne kulia) na mjumbe aliyeongozana naye Bw. Nicolas Agostini (wa pili kulia) 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.