Saturday, February 24, 2024

INDIA YATANGAZA NEEMA KWA ZAO LA MBAAZI NCHINI


 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba akifurahia jambo na Waziri wa Biashara na Viwanda wa India Mhe. Piyush Goyal walipokutana kwa mazungumzo jijini New Delhi. 

India imeridhia Tanzania kuuza kiasi cha mbaazi inachoweza nchini humo kuanzia sasa hadi Machi 2025.

Makubaliano hayo yamefikiwa leo tarehe 24 Februari 2024 wakati wa mazungumzo baina ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba(Mb.) na Mwenyeji wake Waziri wa Biashara na Viwanda wa nchini humo Mhe. Piyush Goyal yaliyofanyika jijini New Delhi. 

Kadhalika, katika mazungumzo hayo viongozi hao wamekubaliana kufanyika kwa Mkutano wa Tume ya Pamoja ya Biashara mwezi Aprili 2024 ili kuweka mikakati ya pamoja ya kukuza biashara baina ya Tanzania na India. 

Awali kabla ya kufikiwa kwa makubaliano haya India iliridhia Tanzania kuuza kiasi cha tani laki mbili pekee za mbaazi kwa mwaka.

Waziri Makamba alikuwa nchini India kushiriki Mkutano wa Raisina 2024 sambamba na kufuatilia utekelezaji wa makubaliano yaliyofikiwa wakati wa ziara ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliyoifanya nchini humo mwezi Oktoba 2023.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba akisalimiana na Waziri wa Biashara na Viwanda wa India Mhe. Piyush Goyal walipokutana kwa mazungumzo ofisini kwake jijini New Delhi. 
Mazungumzo yakiendelea
 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba akiwa na Waziri wa Biashara na Viwanda wa India Mhe. Piyush Goyal baada ya mazungumzo yaliyofanyika Ofisini kwake jijini New Delhi. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba akiwa katika Wizara ya Viwanda na Biashara, India. Wakwanza kulia ni Balozi wa Tanzania nchini humo Mhe. Anisa Mbega.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.