Monday, February 19, 2024

UJUMBE WA NDC WATEMBELEA WIZARA


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba (Mb) amekutana na Ujumbe wa Chuo cha Taifa cha Ulinzi (NDC) jijini Dodoma, Februari 19, 2024.


Ujumbe huo unaongozwa na Mkuu wa Chuo cha NDC, Balozi Meja Jenerali Wilbert A. Ibuge, upo katika ziara ya mafunzo ya kutembelea taasisi mbalimbali kujifunza kuhusu mchango wa taasisi hizo katika maendeleo ya nchi hususan kwenye sekta ya ulinzi. Ujumbe huo wenye jumla ya washiriki 88, unahusisha Wakufunzi 33, na Wanachuo 55 kutoka Tanzania na mataifa ya Afrika ikiwemo Nigeria, Namibia, Misri, Zambia na Zimbabwe.

 

Mej. Gen. Ibuge alieleza kuwa malengo ya chuo hicho ni kuwandaa Maafisa Waandamizi ndani na nje ya nchi kutoka vyombo vya Usalama na Watumishi wa Umma katika nyanja ya Usalama na Stratejia. Wakati wa ziara hiyo, ujumbe huo umeshiriki kwenye mjadala kuhusu Umuhimu wa Kuimarisha usalama wa jamii zinazoishi mipakani kwa ajili ya usalama endelevu wa Taifa (Enhancing Border Community Security for Sustainable National Security).


Ujumbe huo umepokea wasilisho kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, ambapo Balozi Dkt. Shelukindo alielezea majukumu ya Wizara hususan katika kuhamasisha usalama mipakani. Majukumu hayo yanahusisha uratibu wa mikutano ya ujirani mwema na Tume za Kudumu za Pamoja za Ushirikiano (JPCs), Vituo Vya Utoaji Huduma Kwa Pamoja Mipakani (OSBPs), na kuratibu itifaki za kikanda na kimataifa.


Aidha, Wizara na Chuo cha NDC zimeahidi kuendelea kushirikiana katika masuala mbalimbali yakiwemo mafunzo kwa Watumishi na maeneo mengine muhimu kwa maslahi ya pande zite mbili

Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya  na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo akiwa katika mazungumzo na Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Ulinzi, Mej. Gen. Wilbert Ibuge wakati ujumbe wa chuo hicho ulipofanya ziara ya mafunzo Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Bi. Chiku Kiguhe akitoa neno la ukaribisho wakati wa kikao baina ya uongozi wa Wizara na ujumbe kutoka Chuo cha Taifa cha Ulinzi

Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo akitoa neno kuhusu majukumu ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, hususan yanayohusu ulinzi na usalama kwa wanachuo wa Chuo cha Taifa cha Ulinzi.

Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Ulinzi, Mej. Gen. Wilbert Ibuge akitoa maelezo mafupi kuhusu malengo na majukumu ya Chuo cha Taifa cha Ulinzi wakati wa kikao baina ya uongozi wa Wizara na ujumbe wa chuo hicho.
Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo akitoa neno kuhusu majukumu ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, hususan yanayohusu ulinzi na usalama kwa wanachuo wa Chuo cha Taifa cha Ulinzi.
Mkurugenzi wa Sera na Mipango katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Haji Janab akitoa wasilisho kuhusu majukumu ya Wizara wkati wa kikao baina ya uongozi wa Wizara na ujumbe wa chuo cha Taifa cha Ulinzi

Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Ulinzi, Mej. Gen. Wilbert Ibuge akitoa maelezo mafupi kuhusu malengo na majukumu ya Chuo cha Taifa cha Ulinzi wakati wa kikao baina ya uongozi wa Wizara na ujumbe wa chuo hicho.

Mmoja wa wanachuo wa Chuo cha Taifa cha Ulinzi akijitambullisha  wakati ujumbe wa chuo hicho ulipofanya ziara ya mafunzo Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki jijini Dodoma.

Mwanachuo akijitambulisha 

Mwanachuo akijitambulisha 
Mwanachuo akijitambulisha 

Mwanachuo akiuliza swali baada ya kusikiliza wasilisho kuhusu majukumu ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Mwanachuo akiuliza swali baada ya kusikiliza wasilisho kuhusu majukumu ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo akijibu maswali mbalimbali yayoulizwa na wanachuo wa Chuo cha Taifa cha Ulinzi

Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Ulinzi, Mej. Gen. Wilbert Ibuge akitoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali yaliyojitokeza wakati wa kikao baina ya uongozi wa Wizara na ujumbe kutoka Chuo cha Taifa cha Ulinzi

Mwanachuo akiuliza swali baada ya kusikiliza wasilisho kuhusu majukumu ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Kaimu Mkurugenzi wa Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii, Mhandisi Abdillah Mataka akitoa ufafanuzi kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu Vituo vya Pamoja vya Mipakani 

Mwakilishi kutoka Idara ya Siasa, Ulinzi na Usalama, Bw. Amani Mwatonoka akifafanua masuala ya usalama katika mipaka wakati wa kikao baina ya kikao baina ya uongozi wa Wizara na ujumbe wa Chuo cha Taifa cha Ulinzi

Mwanachuo akitoa neno la hukrani baada ya kikao baina ya kikao baina ya uongozi wa Wizara na ujumbe wa Chuo cha Taifa cha Ulinzi

Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo akitoa zawadi kwa Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Ulinzi, Mej. Gen. Wilbert Ibuge baada ya ujumbe wa chuo hicho kufanya ziara ya mafunzo Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki jijini Dodoma.

Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Ulinzi, Mej. Gen. Wilbert Ibuge akitoa zawadi kwa Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo baada ya ujumbe wa chuo hicho kufanya ziara ya mafunzo Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki jijini Dodoma.



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.