Friday, February 9, 2024

RAIS WA POLAND ATEMBELEA HOSPITALI YA AGHAKHAN

 

Rais wa Jamhuri ya Poland Mheshimiwa Andrzej Duda akizungumza bada ya kutembelea mradi wa matibabu ya dharura unaoendeshwa katika hospitali ya Aghakhan jijini Dar es Salaam ili kujionea utekelezaji wa mradi huo.

Rais wa Jamhuri ya Poland Mheshimiwa Andrzej Duda (mwenye tai nyekundu) na Mke wake Bibi Agata Kornhouser-Duda (kushoto) walipotembelea mradi wa matibabu ya dharura unaoendeshwa katika hospitali ya Aghakhan jijini Dar es Salaam ili kujionea utekelezaji wa mradi huo.


Mke wa Rais wa Poland  Bibi Agata Kornhouser-Duda akizungumza kitu walipotembelea mradi wa matibabu ya dharura unaoendeshwa katika hospitali ya Aghakhan jijini Dar es Salaam ili kujionea utekelezaji wa mradi huo




 

 

Rais wa Jamhuri ya Poland Mheshimiwa Andrzej Duda na Mke wake Agata Kornhouser-Duda wametembelea mradi wa matibabu ya dharura unaoendeshwa katika hospitali ya Aghakhan jijini Dar es Salaam ili kujionea utekelezaji wa mradi huo.

Kupitia Mradi huo Serikali ya Poland imetoa msaada wa Dola za Marekani 1,136,703 kwa ajili ya kusaidia utekelezaji wa mradi huo unaolenga kutoa msaada kwa sekta ya matibabu na kusaidia elimu ya wahudumu wa afya katika mkoa wa Dar es Salaam.

Poland pia inafadhili miradi kama hiyo katika Hospitali za Temeke, Mwananyamala, kituo cha Afya Chamazi na Hospitali ya Wilaya ya Nyamagana ya mkoani Mwanza.

 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.