Tuesday, February 6, 2024

WAZIRI MAKAMBA AKUTANA NA VIONGOZI WA TAASISI YA AMANI YA MARTI AHTISAARI.

 

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba akizungumza na Balozi wa Finland nchini Mhe. Thereza Zitting walipokutana  katika Ofisi Ndogo za Wizara jijini Dar Es Salaam na kuzungumza na wawakilishi wa taasisi ya Amani ya Martti Ahtisaari.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba akizungumza alipokutana na Balozi wa Finland nchini Mhe. Thereza Zitting na wawakilishi wa taasisi ya Amani ya Martti Ahtisaari (hawapo katika picha) walipokutana  katika Ofisi Ndogo za Wizara jijini Dar Es Salaam.


 Balozi wa Finland nchini Mhe. Thereza Zitting akizungumza katika kikao na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba walipokutana  katika Ofisi Ndogo za Wizara jijini Dar Es Salaam na kuzungumza na wawakilishi wa taasisi ya Amani ya Martti Ahtisaari.

Mkuu wa Taasisi ya Marrti Ahtisaari Kanda ya Kusini mwa Jangwa la Sahara Bi. Tiina Kukkamaa-Bah akizungumza katika kilichofanyika katika Ofisi ndogo za wizara jijini Dar es Salaam kati ya taasisi hiyo na Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba akizungumza katika na Balozi wa Finland nchini Mhe. Thereza Zitting  na wawakilishi wa taasisi ya Amani ya Martti Ahtisaari walipokutana  katika Ofisi Ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba akizungumza katika picha ya pamoja na Balozi wa Finland nchini Mhe. Thereza Zitting  na wawakilishi wa taasisi ya Amani ya Martti Ahtisaari walipokutana  katika Ofisi Ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam


 


                
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba amekutana na kuzungumza na viongozi wa taasisi ya Amani ya Martti Ahtisaari katika Ofisi Ndogo za Wizara jijini Dar Es Salaam.

Katika mazungumzo hayo viongozi hao wamekubaliana kuendelea kushirikiana na kufanya kazi pamoja ili kumuenzi na kuendeleza falsafa ya Mwanzilishi wa Taasisi hiyo na  Rais wa zamani wa Finland Haya Martti Ahtisaari katika kutafuta amani na kutatua migogoro duniani.

Akizungumza katika kikao hicho Mhe. Waziri Makamba amesema Tanzania iko tayari kushirikiana na taasisi hiyo ili kuendelea kuenzi azma ya hayati Martti Ahtasaari ya kutafuta amani na kutatua migogoro duniani.

“Tupo tayari kufanya kazi na taasisi yenu, tuko tayari kuandaa makubaliano rasmi kupitia Kituo cha Uhusiano cha Kimataifa. Pia, tuko tayari kuendelea kuwa marafiki wakubwa na kushiriki katika mashauriano kuhusu jinsi taasisi yenu itakavyoona inafaa, tunaweza kufuatilia jitihada za kutafuta amani katika eneo la ukanda wetu,” alisema Mhe. Waziri Makamba.

Balozi wa Finland nchini Mhe. Theresa Zitting  alisema Finland iko tayari kushirikiana na kufanya kazi na Tanzania kwa kuwa wanaona kuna nafasi Tanzania inaweza kushiriki katika kutafuta amani na usalama.

Naye Mkuu wa Taasisi ya Marrti Ahtisaari Kanda ya Kusini mwa Jangwa la Sahara Bi. Tiina Kukkamaa-Bah amesema Tanzania na viongozi wake walikuwa marafiki wazuri wa muasisi wa taasisi yao na kwa hali hiyo ndio maana wanapanga kushirikiana na Tanzania ili kuunga mkono jitihada za muanzilishi wao kutafuta amani na usalama katika eneo  la Kusini mwa jangwa la Sahara kupitia Ukanda wa Maziwa Makuu, SADC, Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Taasisi ya Martti Ahtisaari ni shirika lisilo la kiserikali la nchini Finland linalofanya kazi ya kuzuia na kutatua migogoro kupitia mazungumzo  na upatanishi, ilianzishwa mwaka 2000 na Rais wa zamani wa Finland na mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel Hayati Martti Ahtisaari.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.