Thursday, February 8, 2024

DKT. KIBESSE ATETA NA GAVANA WA KAUNTI YA KISUMU

Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Mhe. Dkt. Bernard Kibesse amefanya ziara katika Kaunti ya Kisumu ambapo pamoja na mambo mengine, amekutana kwa mazungumzo na Gavana wa Kaunti ya Kisumu – Kenya, Mhe. Prof. Peter Nyon’go, tarehe 8 Februari 2024. 

 Balozi Kibese na Gavana Nyong’o wamekubaliana kuandaa mkutano wa ujirani mwema kati ya mikoa ya Tanzania na Kenya inayopakana kwenye eneo la Ziwa Victoria ili kuweka mikakati ya kuimarisha ushirikiano wa kijamii, kibishara na kiusalama katika maeneo hayo ikiwemo mikoa ya Mwanza na Mara kwa upande wa Tanzania na Kisumu na Migori kwa upande wa Kenya

Vilevile wamekubaliana kufuatilia mpango wa kuwa na miundombinu ya barabara inayopita kwenye mwambao wa Ziwa Victoria upande wa Tanzania na Kenya.

Gavana wa Kaunti ya Kisumu – Kenya, Mhe. Prof. Peter Nyon’go akizungumza na  Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Mhe. Dkt. Bernard Kibesse (kushoto) alipomtembelea Ofisini kwake katika Kaunti ya Kisumu




No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.