Wednesday, February 14, 2024

ASKOFU DKT. MALASUSA AONGOZA IBADA YA KUMUAGA LOWASSA

 

Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheli Tanzania (KKKT), Dkt. Alex Malasusa ameongoza ibada ya kumuaga Waziri Mkuu Mstaafu Hayati Edward Lowassa katika Kanisa la Azania Front jijini Dar es Salaam tarehe 14 Februari, 2024.

Akihubiri katika ibada hiyo iliyohudhuriwa na mamia ya wananchi Dkt. Malasusa ameeleza kuwa Hayati Lowassa pamoja na familia yake walipenda sana ibada katika maisha yao ya kila siku.

"Kuleta mwili wa mtu asiyependa ibada Kanisani ni kuutesa mwili wa mhusika na hivyo Hayati Lowassa amestahili kuletwa hapa kwakuwa ni sehemu aliyokuwa ameipenda kuja" alisema Dkt. Malasusa

Pia ameeleza ni muhimu kwa viongozi wenye wafuasi nyuma yao kuwa na utaratibu wa kusikiliza neno la Mungu kwa ajili ya kuendelea kuongoza watu wao vizuri na kuleta tija katika yale waliyopewa nafasi ya kuyasimamia.

Ibada hiyo pia ilihudhuriwa na Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Jaji Sinde Warioba, Waziri Ofisi ya Rais- Kazi Maalum, Mhe. George Mkuchika, Waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene,  Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu, Dkt. Jim Yonaz, Kaimu Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mhe. Edward Mpogolo, Mke wa Rais Mstaafu wa Serikali ya Awamu Tatu, Mama Anna Mkapa, Mke wa Waziri Mkuu Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Tatu, Mama Esther Sumaye, Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya na Viongozi wengine Waandamizi wa Serikali na  Kanisa.







 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.