Monday, November 3, 2014

Ujumbe wa wanajeshi wamtembelea Balozi wa Tanzania nchini Malawi

Balozi wa Tanzania, nchini Malawi Mhe. Patrick Tsere (watatu  kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na ujumbe wa wanajeshi sita ukiongozwa na Brigedia Jenerali  Ernest Golinoma Mstaafu (wanne kutoka kulia) walipo mtembelea Ofisini kwake wakiwa na Tuzo walizopata baada ya kushiriki mashindano ya mchezo wa gofu yaliyofanyika mwishoni mwa juma, mjini Lilongwe. Ujumbe huo wa wanajeshi kutoka Tanzania ulikuwa umealikwa na Jeshi la Malawi kucheza gofu ikiwa ni maadhimisho ya kuwakumbuka Waafrika walioshiriki Vita vya Pili vya Dunia na kutimiza miaka mia baada ya vita vya kwanza.
 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.