Thursday, February 19, 2026
TANZANIA NA MSUMBIJI KUIMARISHA USHIRIKIANO KATIKA SEKTA YA AFYA
![]() |
| Waziri
wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mahmoud Thabit
Kombo (Kulia) akiwa na Balozi wa Msumbiji nchini Tanzania Mhe. Ricardo Mtumbuida (Kushoto). |
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Msumbiji
zimeeleza dhamira ya kuimarisha zaidi ushirikiano wa pande mbili katika maeneo
ya kimkakati, ikiwemo Sekta ya Afya ili kuleta maendeleo ya wananchi wake.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano
wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo na Balozi wa Msumbiji
nchini Mhe. Ricardo Mtumbuida, wameeleza dhamira hiyo walipokutana na kufanya
mazungumzo tarehe 18 Februari, 2026 katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es
Salaam.
Mazungumzo hayo yalilenga kubainisha
maeneo ya ushirikiano zaidi kati ya nchi hizo mbili kwa lengo la kuongeza
ushirikiano katika Sekta ya afya, kukuza uchumi, na kujadili maandalizi ya
Mkutano wa Tume ya Kudumu ya Pamoja unaotarajiwa kufanyika nchini mwaka huu.
Kwa upande wake Mhe. Balozi Kombo pia
amewakaribisha wananchi wa Msumbiji kunufaika na huduma za Afya za kibingwa na
kibobezi zinazopatikana nchini ikiwa ni sehemu ya kuendeleza mshikamano na
ushirikiano wa kihistoria kati ya Tanzania na Msumbiji.
Naye Balozi wa Msumbiji nchini, Mhe.
Ricardo Mtumbuida, ameishukuru Tanzania kwa ushirikiano wa kindugu unaoendelea
kuipatia nchi yake, na kusisitiza azma ya Msumbiji ya kuimarisha uhusiano wa
kidiplomasia na kiuchumi na Tanzania ili kukuza ustawi wa wananchi wa mataifa
yote mawili
![]() |
| Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika
Mashariki Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo |
![]() |
| Balozi wa Msumbiji nchini Mhe. Ricardo Mtumbuida |
|
|









.jpeg)
