Wednesday, October 30, 2024

MAFANIKIO YA RAIS SAMIA KATIKA SEKTA YA AFYA YALETA HAMASA KWENYE MKUTANO WA MERCK FOUNDATION


Mafanikio ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan katika sekta ya afya yamewavutia wabia wa maendeleo katika sekta hiyo kuwekeza zaidi nchini, ili kuongeza upatikanaji wa huduma bora za afya na kukuza maendeleo ya Taifa. 

Hayo jamejili leo tarehe 29 Oktoba 2024 kwenye Mkutao wa 11 wa Taasisi ya Merck Foundation Africa Asia Luminary unaoendelea katika Hoteli ya Johari Rotana jijini Dar es Salaam ambao umefunguliwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia.

Mkutano huo uliofanyika Tanzania kwa mara ya kwanza umewakutanisha wadau wa Afya, Wenza wa Marais kutoka Mataifa 15 ya Afrika na Asia, Wawakilishi kutoka taasisi za kimataifa, Wanadiplomasia, waandishi wa habari na Wanataaluma mbalimbali kwa lengo la kubadilishana uzoefu, kujadili na kutafuta suluhu dhidi ya changamoto mbalimbali za afya na kijamii zinazokabili bara la Afrika na Asia. 

Wenza hao 15 wa Marais wanatoka; Zanzibar, Burundi, Kenya, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Gabon, Ghana, Liberia, São Tomé and Príncipe, Malawi, Maldives, Zimbabwe, Msumbiji, Cabo Verde na Gambia. 

Akifungua mkutano Rais Samia amesema Serikali imefanya maboresha makubwa katika sekta ya afya ikiwemo uboreshaji wa mifumo ya utoaji wa huduma za afya ikijumuisha ongezeko la vituo vya afya, vifaa tiba na kuimarika kwa huduma bora za afya za mama na mtoto.

“Nikiwa kama Mwanamke na Mama nimefanya kazi kubwa kwa kushirikiana na wadau katika kuboresha mifumo ya matibabu na utoaji wa elimu kwa umma ili kupiga vita ongezeko la magojwa katika jamii ikiwemo magonjwa yasiyo ambukiza” Alisema Mhe. Rais Samia. 

Rais Samia ameeleza kuwa juhudi hizo zilizofanywa na Serikali zimeleta mapinduzi makubwa katika sekta ya afya ikiwemo kupunguza vifo vinavyotokana na uzazi na upatikanaji wa huduma bora za afya katika jamii. 

Aidha Rais Samia ameishukuru Taasisi ya Merck Foundation kwa kufadhili miradi mbalimbali inayochangia kuboresha huduma za afya kwa mwanawake na kutoa mafunzo stahiki kwa watumishi katika sekta ya afya hatua ambayo imewezesha kuimarisha sekta za hiyo kwa nchi za Afrika na Asia. 

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Merck Foundation Dkt. Rasha Kelej amemwelezea Rais Samia kuwa ni Kiongozi mahiri Mwanamke na mwenye ushawishi duniani kutokana juhudi zake za kuibua na kutetea agenda zinazowezesha kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wanawake kitaifa na kimatiafa. 

“Tumefarijika na kuvutiwa na namna Tanzania imepiga hatua kubwa katika kuboresha sekta ya afya, elimu, kuwezesha wanawake kiuchumi na mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia. Hii imetupa hamasa kubwa ya kuendelea kushirikiana na Tanzania kwa kutanua uwigo wa huduma zetu hapa nchini ili kuhakikisha jamii ya Tanzania inapata maendeleo endelevu.” Alisema Dkt. Rash 

Awali Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawanake na Makundi Maalumu Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima ameeleza kuwa Serikali imeweka mazingira mazuri ya kisera na kisheria katika kukuza usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake na wasichana. Amebainisha kuwa mazingira hayo yamechangiwa na Sera ya Taifa ya Jinsia na Maendeleo ya Wanawake ya mwaka 2023, uanzishwaji wa Programu madhubuti za Elimu kwa Wasichana na Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi kupitia mikopo na mafunzo ya ujuzi wa biashara. 

Mkutano huo wa siku mbili wa Merck Foundation ambao unatarajiwa kuhitimishwa kesho tarehe 30 Oktoba 2024 umehudhuriwa na washiriki takriban 6000 kutoka nchi zaidi ya 50 duniani. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akifungua Mkutano wa 11 wa Merck Foundation Africa Asia Luminary katika hoteli ya Johari Rotana Jijini Dar es Salaam tarehe 29 Oktoba, 2024.
Sehemu ya Wenza wa Wakuu wa nchi mbalimbali Barani Afrika wakifuatilia Mkutano wa 11 wa Merck Foundation Africa Asia Luminary uliokuwa ukiendelea katika hoteli ya Johari Rotana Jijini Dar es Salaam tarehe 29 Oktoba 2024.
Mkutano ukiendelea
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Cosato Chumi (Mb.) akisalimiana na wageni mbalimbali kwenye Mkutano wa 11 wa Merck Foundation Africa Asia Luminary uliofanyika katika hoteli ya Johari Rotana Jijini Dar es Salaam
Mwenza wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Mama Mariam Mwinyi akifurahia jambo kwenye Mkutano wa 11 wa Merck Foundation Africa Asia Luminary uliofanyika katika hoteli ya Johari Rotana Jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya Wenza wa Wakuu wa nchi mbalimbali Barani Afrika wakifuatilia Mkutano wa 11 wa Merck Foundation Africa Asia Luminary uliokuwa ukiendelea katika hoteli ya Johari Rotana Jijini Dar es Salaam tarehe 29 Oktoba 2024.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Merck Foundation Dkt. Rasha Kelej akizungumza kwenye hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa 11 wa Merck Foundation Africa Asia Luminary uliofanyika katika hoteli ya Johari Rotana Jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya Mabalozi wa Tanzania wanaoiwakilisha nchi sehemu mbalimbali wakifuatilia Mkutano wa 11 wa Merck Foundation Africa Asia Luminary uliofanyika katika hoteli ya Johari Rotana Jijini Dar es Salaam.



Mwanza wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.  Mama Mbonimpaye Mpango kwenye Mkutano wa Mkutano wa 11 wa Merck Foundation Africa Asia Luminary uliofanyika katika hoteli ya Johari Rotana Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Mawasiliano katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwenye Mkutano wa 11 wa Merck Foundation Africa Asia Luminary uliofanyika katika hoteli ya Johari Rotana Jijini Dar es Salaam.
Mwenza wa Rais wa Jamhuri ya Ghana Mhe. Mama Rebecca Victoria Akufo-Addo akiwasalimia washiriki wa Mkutano wa 11 wa Merck Foundation Africa Asia Luminary uliofanyika katika hoteli ya Johari Rotana Jijini Dar es Salaam.
Mwenza wa Rais wa Jamhuri ya Kenya Mhe. Mama Rachel Ruto akiwasalimia washiriki wa Mkutano wa 11 wa Merck Foundation Africa Asia Luminary uliofanyika katika hoteli ya Johari Rotana Jijini Dar es Salaam.
Mwenza wa Rais wa Jamhuri ya Maldives Mhe. Mama Sajidha Mohamed akiwasalimia washiriki wa Mkutano wa 11 wa Merck Foundation Africa Asia Luminary uliofanyika katika hoteli ya Johari Rotana Jijini Dar es Salaam.
Mkutano ukiendelea

Tuesday, October 29, 2024

RAIS SAMIA WATAKIA HERI WANANCHI WA BOTSWANA KATIKA UCHAGUZI WA TAREHE 30 OKTOBA, 2024

 TAARIFA YA MHESHIMIWA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, NA MWENYEKITI WA ASASI YA SIASA, ULINZI NA USALAMA YA JUMUIYA YA MAENDELEO KUSINI MWA AFRIKA (SADC - ORGAN) KUHUSU UCHAGUZI MKUU WA JAMHURI YA BOTSWANA TAREHE 30 OKTOBA, 2024.

 


 

Monday, October 28, 2024

BALOZI MAHADHI , AIR ASIA WATEMBELEA OFISI ZA TTB



Balozi wa Tanzania Nchini Malaysia Mhe Dkt. Mahadhi Juma Maalim ameongoza ujumbe wa wawekezaji kutoka Shirika la Ndege la Malaysia (AirAsia) kutembelea Ofisi za Bodi ya Utalii Tanzania (TTB ).


Katika Ofisi za TTB wamekutana na kuzungumza na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TTB Balozi Dkt. Ramadhan Dau na kuelezea dhima yao ya kuanzisha safari za ndege za moja kwa moja kutoka Malaysia kuja Tanzania na hivyo kuongeza idadi ya watalii kutoka mataifa mbalimbali duniani kuja Tanzania.


Mhe. Balozi Mahadhi na ugeni wake wako nchini kuangalia jinsi ya kuimarisha ushirikiano katika sekta ya anga kati ya Tanzania na Malaysia.


Shirika la Air Asia lina ndege 250 zinazotua katika viwanja 147 duniani.







Sunday, October 27, 2024

MHE. PINDA , SEOM WAKUTANA NA MACHIFU WA BOTSWANA


Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi ya Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC-SEOM) Mhe. Mizengo Pinda, akisalimiana na Kiongozi wa Machifu wa Botswana Chifu Gaborone wa kabila la Batlokwa walipokutana jijini Gaborone tarehe 27 Oktoba, 2024

 

Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi ya Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC-SEOM) Mhe. Mizengo Pinda, akisalimiana na Kiongozi wa Machifu wa Botswana Chifu Gaborone wa kabila la Batlokwa walipokutana jijini Gaborone tarehe 27 Oktoba, 2024

 

 

 

 

Kiongozi wa Machifu wa Botswana Chifu Gaborone wa kabila la Batlokwa akizungumza na Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi ya Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC-SEOM) Mhe. Mizengo Pinda na ujumbe wake (hawako pichani) walipokutana jijini Gaborone tarehe 27 Oktoba, 2024

 

Kiongozi wa Machifu wa Botswana Chifu Gaborone wa kabila la Batlokwa akizungumza na Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi ya Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC-SEOM) Mhe. Mizengo Pinda na ujumbe wake (hawako pichani) walipokutana jijini Gaborone tarehe 27 Oktoba, 2024

 

 Baadhi ya Machifu wa Botswana wakifuatilia kikao chao na Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi ya Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC-SEOM) Mhe. Mizengo Pinda na ujumbe wake (hawako pichani) walipokutana jijini Gaborone tarehe 27 Oktoba, 2024

 

mmoja wa Machifu wa Botswana akizungumza  kikao cha machifu  na Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi ya Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC-SEOM) Mhe. Mizengo Pinda na ujumbe wake (hawako pichani) walipokutana jijini Gaborone tarehe 27 Oktoba, 2024

 

 Kiongozi wa wa Chama cha Real Alternative Bw.  Gaontebale Mokgosi akizungumza  kikao cha machifu  na Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi ya Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC-SEOM) Mhe. Mizengo Pinda na ujumbe wake (hawako pichani) walipokutana jijini Gaborone tarehe 27 Oktoba, 2024

 Kiongozi wa wa Chama cha Real Alternative Bw.  Gaontebale Mokgosi akizungumza  kikao cha machifu  na Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi ya Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC-SEOM) Mhe. Mizengo Pinda na ujumbe wake (hawako pichani) walipokutana jijini Gaborone tarehe 27 Oktoba, 2024


Baadhi ya Machifu wa Botswana katika picha ya pamoja na Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi ya Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC-SEOM) Mhe. Mizengo Pinda na ujumbe wake (hawako pichani) walipokutana jijini Gaborone tarehe 27 Oktoba, 2024




Kiongozi wa Machifu wa Botswana Chifu Gaborone wa kabila la Batlokwa akizungumza na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Said Shaib Mussa huku Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi ya Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC-SEOM) Mhe. Mizengo Pinda akiwaangalia walipokutana jijini Gaborone tarehe 27 Oktoba, 2024

 

Kiongozi wa wa Chama cha Real Alternative Bw.  Gaontebale Mokgosi (wapili kulia waliokaa) katika picha ya pamoja na Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi ya Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC-SEOM) Mhe. Mizengo Pinda na ujumbe wake (hawako pichani) walipokutana jijini Gaborone tarehe 27 Oktoba, 2024

 

 

Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi ya Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC-SEOM) Mhe. Mizengo Pinda, amekutana na kuzungumza na machifu kutoka koo mbalimbali za nchini Botswana katika kikao kilichofanyika jijini Gaborone tarehe 27 Oktoba 2024 ikiwa ni sehemu ya vikao ambavyo SEOM imekuwa ikifanya na wadau mbalimbali wa uchaguzi nchini humo.

 

Mhe. Pinda ametumia kikao hicho kuwajulisha machifu hao kuhusiana na kazi ya uangalizi wa uchaguzi mkuu wa Botswana kuanzia maandalizi, mwenendo wake na jinsi mambo yalivyo wakati huu wa uchaguzi ikiwa ni kutekeleza jukumu la Uangalizi kwa kuzingatia misingi na miongozo ya uchaguzi wa kidemokrasia iliyowekwa na SADC.

 

Aliwaambia machifu hao kuwa SEOM imekuwa ikikutana na wadau mbalimbali na  kuzungumza nao moja kwa moja na hivyo kupata picha halisi ya jinsi mwenendo na maandalizi ya uchaguzi huo yalivyo na kuongeza kuwa SEOM imepeleka waangalizi wake katika majimbo yote ya uchaguzi ili kuangalia hali inavyokwenda, itakavyokuwa siku ya uchaguzi na baada ya uchaguzi.

 

Akizungumza katika kikao hicho Kiongozi wa Machifu wa Botswana Chief Gaborone toka kabila la Batlokwa alisema wao kama machifu wana jukumu la kuhakikisha koo zao hazigawanyiki licha ya kuwa wananchi wao ni wafuasi wa vyama vya siasa na kwa kufanya hivyo  amani na usalama vitaendelea kuwepo katika maeneo yao.

 

Alisema wao wakiwa viongozi wa kimila na kijadi nchini humo wana wajibu wa kuwahimiza wananchi kushiriki katika michakato ya siasa ili waweze kuchagua viongozi wa kisiasa ambao wataongoza nchi kwa kipindi husika.

 

Amesema wao sio wanasiasa ila wanashirikiana na viongozi serikali kuhakikisha wananchi wanashiriki kikamilifu katika shughuli za siasa kwa kufuata sheria, kanuni, taratibu na miongozo iliyopo akitolea mfano wa Tume Huru ya Uchaguzi ya Botswana ilivyowafuata na kuwajulisha juu ya juu ya kufanyika kwa zoezi la uandikishaji wapiga kura na kuwaomba kuwasaidia kufikisha ujumbe huo wa uandikishaji wapiga kura kwa wananchi kwenye maeneo yao.

 

Naye Chifu Lotlamoreng kutoka kabila la Barolong amesema kama chifu akitaka kujihusisha moja kwa moja na masuala ya siasa ni lazima aondoke katika kazi ya uchifu ili aweze kuwa huru kujihussiha na masuala ya siasa nchini humo.

 

Wamesema machifu hawajazuiwa kugombea nafasi za siasa ila wanatakiwa wajue kuwa ukiamua kugombea na kushiriki kama mgombea unatakiwa kuondoka katika ofisi ya chifu ili kuepuka mgogoro wa maslahi na sheria Sheria ya Machifu ya mwaka 2008 ambayo inawatambua machifu na Ofisi zao nchini Botswana.

 

Ameongeza kuwa katiba ya Botswana pia inatambua Ofisi ya Machifu na inawatambua machifu hao ambo wako zaidi ya 500 wakiwamo machifu wananwake ambao wanakaribia 100.

Katika mkutano mwingine, SEOM ilikutana na Kiongozi wa wa Chama cha Real Alternative Bw.  Gaontebale Mokgosi ambaye alionyesha wasiwasi kuhusu maandalizi ya uchaguzi huo ambayo yamefanywa na Tume Huru ya Uchaguzi (IEC), akitaja kuchelewa kwa uchapishaji wa karatasi za kupigia kura kama mfano wa mandalizi duni ya uchaguzi huo na wanadhani kuwa IEC haiko tayari kuendesha uchaguzi huru na wa na haki.

Chama hicho kilisisitiza umuhimu wa kuongeza utoaji wa elimu ya wapiga kura na kupendekeza kuwa IEC inapaswa kushirikiana kwa karibu na vyama vya siasa nchini Botswana ili kuhamasisha watu wengi zaidi kushiriki zoezi la kuandikisha wapiga kura na kujitokeza kupiga kura. Pia walisisitiza umuhimu wa ofisi ya ushirikiano wa vyama vya kisiasa kutakiwa kufanya kazi zaidi mwaka huu wa uchaguzi kinyume na ilivyokuwa kwakuwa ofisi hiyo ina jukumu muhimu la kuunganisha IEC, vyama vya kisiasa, na raia kwa ujumla.

 


MHE. PINDA AKUTANA NA JUMUIYA YA WANADIPLOMASIA WANAOWAKILISHA NCHI ZAO BOTSWANA


Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC-SEOM) Mhe. Mizengo Pinda, na ujumbe wake katika  kikao na Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao nchini Botswana kilichofanyika jijini Gaborone tarehe 26 Oktoba 2024


Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC-SEOM) Mhe. Mizengo Pinda, na ujumbe wake (kulia) katika  kikao na Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao nchini Botswana kilichofanyika jijini Gaborone tarehe 26 Oktoba 2024


Balozi wa Tanzania nchini Botswana Mhe. James Bwana (Kushoto) akiwa na Mabalozi wenzake wanaoziwakilisha nchi zao nchini Botswana wakifutiliamkutano wao na Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC-SEOM) Mhe. Mizengo Pinda uliofanyika jijini Gaborone tarehe 26 Oktoba 2024


Kiongozi wa Mabalozi na Balozi wa Angola nchini Botswana Mhe. Beatriz Morais (kushoto) akiwa na mabalozi wenzake wanaoziwakilisha nchi zao nchini Botswana wakifutilia mkutano wao na Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC-SEOM) Mhe. Mizengo Pinda uliofanyika jijini Gaborone tarehe 26 Oktoba 2024


Balozi wa Tanzania nchini Botswana Mhe. James Bwana (Kushoto) akiwa na Mabalozi wenzake wanaoziwakilisha nchi zao nchini Botswana wakifutiliamkutano wao na Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC-SEOM) Mhe. Mizengo Pinda uliofanyika jijini Gaborone tarehe 26 Oktoba 2024


Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC-SEOM) Mhe. Mizengo Pinda, katika picha ya Pamoja na Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao nchini Botswana baada ya mkutano kati ya SEOM na Jumuiya ya wanadisplomasia wanaoziwakilisha nchi zao nchini Botswana uliofanyika jijini Gaborone tarehe 26 Oktoba 2024 uliolenga kusikiliza maoni na mtazamo wa Mabalozi kuhusiana na mwenendo wa uchaguzi mkuu wa Botswana unaotarajiwa kufanyika tarehe 30 Oktoba 2024.


Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC-SEOM) Mhe. Mizengo Pinda, akizungumza na Balozi wa Marekani nchini Botswana, Mhe. Howard Van Vranken, baada ya mkutano kati ya SEOM na Jumuiya ya wanadisplomasia wanaoziwakilisha nchi zao nchini Botswana uliofanyika jijini Gaborone tarehe 26 Oktoba 2024 ambao ulilenga kusikiliza maoni na mtazamo wa Mabalozi kuhusiana na mwenendo wa uchaguzi mkuu wa Botswana unaotarajiwa kufanyika tarehe 30 Oktoba 2024.

 

Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi ya Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC-SEOM) Mhe. Mizengo Pinda, amekutana na kuzungumza na Jumuiya ya Wanadiplomasia wanaoziwakilisha nchi zao nchini Botswana katika kikao kilichofanyika jijini Gaborone tarehe 26 Oktoba 2024.

Akizungumza katika kikao hicho Mhe. Pinda amewaarifu wanadiplomasia hao juu ya majukumu ya SEOM  katika kutekeleza jukumu la Uangalizi kama lilivyokasimiwa na SADC na kusisitiza kuwa SEOM inaifanya kazi hiyo kwa kuhakikisha nchi husika inazingatia na kufuata misingi na miongozo ya uchaguzi wa kidemokrasia ya SADC.

Ameeleza kuwa SEOM imekutana na wadau mbalimbali ikiwa ni sehemu ya ratiba za misheni hiyo kusikiliza na kuzungumza moja kwa moja na wadau wa uchaguzi huo kupata picha halisi ya jinsi mwenendo na maandalizi ya uchaguzi huo unavyokwenda.

Amesema SEOM imekuwa ikiangalia jinsi mwenendo, mipango na utaratibu wa uchaguzi huo unavyoendeshwakwa, kuangalia kama elimu kwa wapiga kura imetolewa vya kutosha, kama inaendelea kutolewa kwa wadau wote wa uchaguzi huo na kama kumekuwa na ushirikishwaji kwa wadau wote wa uchaguzi nchini humo na hivyo kuwa na uelewa wa pamoja kuhusiana na uchaguzi mkuu wa Botswana uliopangwa kufanyika tarehe 30 Oktoba,2024.

Amesema SEOM imepeleka waangalizi wake katika majimbo yote ya uchaguzi ili kuangalia hali inavyokwenda , itakavyokuwa siku ya uchaguzi na baada ya uchaguzi na watakuwa na mikutano na watu mbalimbali ikiwa ni sehemu ya kusikiliza na kupata maoni ili kuhakikisha kazi yao ya uangalizi inakwenda vizuri

Akizungumza katika kikao hicho Mkuu wa Mabalozi hao na Balozi wa Jamhuri ya Angola Mheshimiwa Beatriz Morais ameishukuru SEOM kwa kufikiria kukutana na mabalozi kama moja ya wadau wa uchaguzi wa Botswana ili kusikiliza mtazamo wao kuhusiana na mwenendo wa uchaguzi na kuwapongeza wananchi wa Botswana kwa hali ya utulivu waliyonayo na hivyo kuwa na amani na usalama katika maeneo yote.

Naye Balozi wa Ufaransa nchini Botswana amepongeza hali ya amani na utulivu iliyoko nchini Botswana wakati huu wakielekea katika uchaguzi mkuu na kuongeza kuwa ni jambo la msingi na la mfano kwa nchi za Afrika na nyinginezo.

Balozi wa Tanzania nchini Botswana mwenye makazi yake nchini Afrika Kusini Mhe. James Bwana amepongeza Serikali ya Botswana kwa kuruhusu na kuwakaribisha waangalizi wa uchaguzi nchini humo na kuwa tayari kushirikiana nao na kuwapongeza wananchi wa Botswana kwa utulivu waliounesha katika kipindi hiki na kuwatakia kila la heri katika uchaguzi mkuu ujao.

SEOM pia imekutana na viongozi wa vyama vya siasa vya  BPF, BMD na Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika (MISA) Botswana. Vyama vya siasa katika mikutano yao wameelezea kutokuridhishwa kwao na mwenendo wa uchaguzi huo huku wakisema kumekuwa na uhaba wa karatasi za kupigia kura hali ambayo inawatia mashaka juu ya uchaguzi huo kufanyika kwa uhuru na kwa haki na kuongeza kuwa kitendo cha kuchelewa kutangazwa mapema kwa tarehe ya uchaguzi kumevifanya vyama vya upinzani nchini humo kutokuwa na maandalizi mazuri ya uchaguzi huo.

Chama cha BPF kimesema wanaamini kuwa matokeo ya kurudiwa kwa kura za awali zilizohussisha Diaspora, vyombo vya ulinzi na usalama na majimbo matatu zitaongeza matumaini kwa wananchi na hivyo kujitokeza kwa wingi kushiriki uchaguzi huo.

Nayo MISA Botswana amesema taasisi yao imekuwa ikijishughulisha na utoaji wa elimu kwa waandishi wa Habari juu ya kuandaa na kuripoti taarifa za uchaguzi ila wanaelewa kuwa wnachama wao wanakabiliwa na ushindani mkubwa kutoka kwa taarifa zinazotolewa na wananchi kupitia mitandao ya kijamii ambazo hazizingatii misingi na maadili ya uandishi wa habari.

 






Friday, October 25, 2024

MHE. PINDA AKUTANA NA RAIS WA BOTSWANA

Mkuu wa Misheni ya Uangalizi ya Uchaguzi wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC - SEOM) kwenye Uchaguzi Mkuu wa Botswana na Waziri Mkuu wa zamani wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mizengo Pinda akisalimiana na Rais wa Jamhuri ya Botswana Mheshimiwa Mokgweetsi Eric Keabetswe Masisi alipofika Ofisini kwa Mheshimiwa Masisi kujitambaulisha na ujumbe wake tarehe 24 Oktoba, 2024. Mhe. Pinda na ujumbe wake wako nchini Botswana  kuangalia uchaguzi mkuu wa nchi hiyo uliopangwa kufanyika tarehe 30 Oktoba 2024

 
Mkuu wa Misheni ya Uangalizi ya Uchaguzi wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC - SEOM) kwenye Uchaguzi Mkuu wa Botswana na Waziri Mkuu wa zamani wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mizengo Pinda akisaini kitabu cha wageni alipowasili  Ofisini kwa Mheshimiwa Masisi kujitambaulisha na ujumbe wake tarehe 24 Oktoba, 2024.

Rais wa Jamhuri ya Botswana, Mheshimiwa Mokgweetsi Eric Keabetswe Masisi (kushoto) akizungumza na Mkuu wa Misheni ya Uangalizi ya Uchaguzi wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC - SEOM) kwenye Uchaguzi Mkuu wa Botswana na Waziri Mkuu wa zamani wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mizengo Pinda alipokutana na ujumbe wa SEOM katika Ikulu ya Gaborone tarehe 24 Oktoba 2024. Kulia ni Katibu Mtendaji wa SADC, Mheshimiwa Elias Magosi.

Rais wa Jamhuri ya Botswana, Mheshimiwa Mokgweetsi Eric Keabetswe Masisi (kushoto) na Mkuu wa Misheni ya Uangalizi ya Uchaguzi wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC - SEOM) kwenye Uchaguzi Mkuu wa Botswana na Waziri Mkuu wa zamani wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mizengo Pinda walipokutana  Ikulu ya Gaborone tarehe 24 Oktoba 2024.

Kikao kikiendelea

Kikao kikiendelea

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Botswana, Mhe. Dkt. Lemongang Kwape (kulia), na watendaji wake waliposhiriki kikao kati ya Rais wa Jamhuri ya Botswana, Mheshimiwa Mokgweetsi Eric Keabetswe Masisi (kushoto) na Mkuu wa Misheni ya Uangalizi ya Uchaguzi wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC - SEOM) kwenye Uchaguzi Mkuu wa Botswana na Waziri Mkuu wa zamani wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mizengo Pinda alipowatembelea Ikulu jijini Gaborone.

Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC-SEOM), Mheshimiwa Mizengo Pinda, na baadhi ya wajumbe wake walipofika Ofisini kwa kwa Rais wa Jamhuri ya Botswana, Mheshimiwa Mokgweetsi Eric Keabetswe Masisi,  jijini Gaborone.






Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC-SEOM), Mheshimiwa Mizengo Pinda, akiangalia picha za waliowahi kuwa Marais wa Jamhuri ya Botswa alipofika ofisini kwa  Rais wa Jamhuri ya Botswana, Mheshimiwa Mokgweetsi Eric Keabetswe Masisi,  jijini Gaborone.


 

Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC-SEOM), Mheshimiwa Mizengo Pinda, amekutana na Rais wa Jamhuri ya Botswana, Mheshimiwa Mokgweetsi Eric Keabetswe Masisi, katika ofisi yake jijini Gaborone. SEOM ilitumia ziara hiyo kujitambulisha kwa Mhe. Rais Masisi na kubadilishana mawazo kuhusu hali ya kidemokrasia na maendeleo nchini Botswana.

Akizungumza na Mheshimiwa Masisi, Mheshimiwa Pinda alisisitiza wajibu wa SEOM kulingana na Misingi na Mwongozo wa SADC kuhusu Uchaguzi wa Kidemokrasia na kuonesha utayari kwa SEOM kutekeleza jukumu la uangalizi katika uchaguzi mkuu ujao wa Botswana.

Mhe. Pinda alieleza shukrani zake kwa mapokezi mazuri aliyoyapata yeye na timu yake tangu walipowasili Botswana na kumueleza Mhe. Rais Masisi kuwa kabla ya kukutana na yeye, SEOM ilikutana na kuzungumza na wadau mbalimbali, ambao ni pamoja na Tume Huru ya Uchaguzi ya Botswana (IEC), Kamishna wa Polisi wa Botswana, Wizara ya Mambo ya Nje, viongozi wa vyama vya kisiasa, NGO, na Mabalozi wanaowakilisha Botswana na SADC.

Aliongeza kuwa timu hiyo pia ilipitia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii ili kupata ufahamu kuhusu masuala yanayohusiana na uchaguzi mkuu ujao wa nchi hiyo.

Kwa upande wake, Mhe. Rais Masisi aliwakaribisha waangalizi wa SEOM na kuwahakikishia kuwa Batswana iko tayari kwa uchaguzi mkuu utakaofanyika tarehe 30 Oktoba 2024 na kuongeza kuwa Serikali ya Botswana iko tayari kushirikiana na wadau wote, ikiwa ni pamoja na waangalizi na aliwaambia SEOM kuzungumza na yeyote wanayefikiri atawasaidia kutekeleza jukumu lao la uangalizi.

“Serikali iko tayari kufanya kazi na waangalizi; nendeni mkazungumze na yeyote mnayefikiri anaweza kuwasaidia nyinyi na timu yenu kufanya kazi zenu vizuri. Botswana ni nyumbani kwa SADC; nyote mnakaribishwa hapa na fanyeni kazi yenu  kwa uhuru," alisisitiza Mheshimiwa Masisi.

Alisema anaamini kuwa Tume Huru ya Uchaguzi ya Botswana (IEC) imeshirikisha wadau wote wanaohusika na uchaguzi huo mkuu, na kwamba Serikali yake ina imani kuwa kila kitu kitakuwa sawa na uchaguzi utakuwa huru, haki, na wa kuaminika, na kwamba usalama na amani vitakuwepo wakati wa uchaguzi na hata baada ya uchaguzi huo.

Aliwahakikishia wajumbe wa SEOM kuwa Serikali imetumia rasilimali zote zilizopo kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa mafanikio makubwa na alisisitiza kuwa Serikali iko tayari kutoa msaada wowote kwa SEOM pale itakapohitajika.

Septemba 2024, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa Ulinzi na Usalama ya  SADC TROIKA, alimteua Mheshimiwa Pinda kuongoza Misheni ya  Uangalizi wa SADC katika uchaguzi mkuu wa Botswana.

SEOM ilijumuisha maafisa kutoka Sekretarieti ya SADC, wanachama wa Taasisi ya SADC Troika kutoka Jamhuri ya Malawi, Zambia, na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, pamoja na Baraza la Ushauri la Uchaguzi la SADC (SEAC).

 


 

Thursday, October 24, 2024

Waandishi Waendesha Ofisi 16 mafunzoni Mjini Morogoro


Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, imefanikiwa kupeleka waandishi waendesha Ofisi 16 kwenye mafunzo ya matumizi fasaha ya Kiswahili Sanifu, yanayoendeshwa na Baraza la Kiswahili Tanzania (BAKITA). Mafunzo hayo yanayofanyika katika Hoteli ya Morena Mjini Morogoro yalianza tarehe 21 Oktoba 2024 na yatahitimishwa tarehe 26 Oktoba 2024 

Akifungua mafunzo hayo Mratibu wa Mafunzo kutoka BAKITA Bi. Razati Mmary alieleza kuwa mafunzo hayo yanalenga kuwawezesha Waandishi Waendesha Ofisi kuwa na matumizi ya Kiswahili Fasaha na Sanifu katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

 

Aidha, alisisitiza Waandishi waendesha Ofisi wanao wajibu wa kurekebisha makosa yaliyozoeleka katika uandishi wa nyaraka za Serikali.