Wednesday, September 25, 2013

Tanzania yasaini Itifaki ya Kimataifa ya Kukomesha Biashara Haramu ya Bidhaa za Tumbaku

Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Mhe. Hussein Mwinyi (Mb.)  akiwa katika picha ya pamoja na Naibu Balozi  katika Ubalozi wa Kudumu wa Tanzania, New York, Mhe. Ramadhan Mwinyi, Bi. Tully Mwaipopo, Afisa katika Ubalozi wa Tanzania, New York  na Bw. Santiago Villalpando, Mkuu wa Kitengo cha Mikataba wa Umoja wa Mataifa mara baada ya Mhe. Mwinyi kusaini Itifaki ya Kimataifa ya  Kukomesha Biashara Haramu ya Bidhaa zitokanazo na Tumbaku. Tanzania imekuwa nchi ya 24 duniani kusaini Itifaki hiyo ambapo kukamilika kwake kutatoa fursa kwa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa kudhibiti biashara hiyo ambayo kwa kiasi kikubwa hugharimu na kuathiri afya za watu. (Picha kwa Hisani ya Win Khine wa Umoja wa Mataifa)










Mhe. Membe akutana kwa mazungumzo na Naibu Waziri wa Uingereza

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akisalimiana na Naibu Waziri wa Uingereza anayeshughulikia Mambo ya Nje na Jumuiya ya madola, mhe. Mark Simmonds walipokutana kwa mazungumzo Mjini New York wakati wa Kikao cha 68 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.

Mhe. Membe na Mhe. Simmonds katika picha ya pamoja.
Mhe. Membe akizungumza na Mhe. Simmonds kuhusu masuala ya ushirikiano baina ya nchi hizi mbili.
Ujumbe ulioambatana na Mhe. Simmonds.
Mhe. Simmonds akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo.
Ujumbe wa Tanzania wakati wa mazungumzo. Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Balozi Dora Msechu, akifuatiwa na Bi. Tully Mwaipopo, Bw. Grayson Ishengoma na Bw. Togolani Mavura Maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.   





                            Na Rosemary Malale, New York


TANZANIA YAIPONGEZA UINGEREZA KWA KUANZISHA HUDUMA YA VIZA ZA HARAKA KWA WATANZANIA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) ameishukukuru na kuipongeza Serikali ya Uingereza kwa kuanzisha huduma mpya itakayowawezesha Watanzania kupata viza za kuingia nchini humo kwa haraka.

Huduma hiyo ambayo ilitangazwa na nchi hiyo hivi karibuni kupitia Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Mhe. Diana Melrose ni moja ya mipango ya nchi hiyo ya kuimarisha uhusiano kati ya nchi hizi mbili. Huduma hiyo hukamilika kwa takribani siku tano hadi kupata viza.

Akizungumza hivi karibuni na Naibu Waziri wa Uingereza anayeshughulikia Mambo ya Nje na Jumuiya ya Madola, Mhe. Mark Simmonds Mjini New York, Marekani wakati wa Kikao cha 68 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Mhe. Membe alisema kuwa anaishukuru nchi hiyo kwa kuichagua Tanzania katika mpango huo ikiwa ni mshirika wake muhimu wa maendeleo na kwa kuzingatia kuwa uchumi wa Tanzania unakua kwa haraka katika siku za hivi karibuni hivyo itarahisisha na kuimarisha biashara baina ya nchi hizi mbili.

Aidha, Mhe. Membe aliongeza kuwa Watanzania wengi wamekuwa wakijishighulisha na biashara mbalimbali ndani na nje ya nchi ikiwemo Uingereza hivyo mpango huo wa viza za haraka utawasaidia kuimarisha biashara zao badala ya kukatishwa tamaa na mlolongo mrefu wa kufuatilia viza uliokuwepo hapo awali.
“Tunaishukuru sana Serikali ya Uingereza kwa kuanzisha huduma hiyo ya utoaji viza za haraka, hata hivyo bado tunaiomba ifikirie tena uwezekano wa kurejesha huduma ya utoaji viza Jijini Dar es Salaam badala ya kufuatilia viza hizo Nairobi nchini Kenya”, alisema Waziri Membe.

Aidha, aliomba kiwango cha nyongeza kilichowekwa cha shilingi laki mbili na nusu kwa ajili ya kukamilisha mchakato wa viza hiyo ya haraka kipunguzwe kwani ni kikubwa kwa Watanzania.
Akizungumza kwa upande wake, Mhe. Simmonds alisema kuwa Uingereza itaendelea kuimarisha ushirikiano na Tanzania hususan katika masuala ya biashara na uwekezaji.

Mkutano huo wa Mhe. Waziri Membe na Mhe. Simmonds ulihudhuriwa na Wajumbe wengine akiwemo Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Dora Msechu.

-Mwisho-





Mhe. Rais Kikwete azindua Mpango wa Kuzishirikisha Sekta mbalimbali kupambana na Malaria

 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akitoa hotuba ya kuzindua rasmi Mpango mpya wa Kimataifa utakaohusisha Sekta mbalimbali katika kukabiliana na Ugonjwa wa Malaria duniani. Uzinduzi huo umefanyika katika Ofisi za Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani chini ya uratibu wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) kwa kushirikiana na Taasisi ya Roll Back malaria Partbership.
iongoni mwa wageni waliohudhuria uzinduzi huo akiwemo Waziri wa Afya na Ustawai wa Jamii, Dkt. Hussein Mwinyi (Mb.) (kulia) wakimsikiliza Mhe. Rais Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akihutubia.
Rais wa Msumbiji, Mhe. Armando Guebuza akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mpango wa kuzishirikisha Sekta mbalimbali katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Malaria.                                           


Mhe. Rais Kikwete na Mhe. Rais Guebuza wakiwa na wageni waalikwa wengine.

Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Mhe. Liberata Mulamula akiwa na wageni waalikwa wakati wa uzinduzi wa mpango wa kukabiliana na malaria kwa kuzishirikisha sekta mbalimbali.

Mshauri wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Malengo ya Milenia, Prof. Jeffrey Sachs akizungumza wakati wa uzinduzi wa mpango huo.
Mwakilishi wa Taasisi ya Roll Back Malaria Partnership mjini New York Bw. Herve Verhoosel akimkabidhi Mhe. Rais Kikwete mfano wa kifaa cha kufukuzia mbu  wakati wa uzinduzi wa mpango wa mapambano dhidi ya malaria.

Mhe. Mwinyi akifurahia jambo na Bi. Rebeca Grynspan kutoka UNDP pamoja na Bi. Ellen Maduhu, Afisa kutoka Ubalozi wa Tanzania, New York.

Tuesday, September 24, 2013

ASKARI WA JWTZ ALIYEJERUHIWA CONGO NA KUFARIKI AAGWA LEO LUGALO


Mkuu wa Majeshi, Jenerali Davis Mwamunyange akizungumza

Askari Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) wakiwa wamebeba sanduku lililohifadhi mwili wa Askari mwenzao, Marehemu Private, Hugo Munga alifariki dunia Septemba 18 mwaka huu huko Pretoria Afrika Kusini kufuatia majeraha aliyoyapata akiwa na vikosi vya MONUSCO Congo DRC katika operations ya kuwaondoa waasi wa M23. Mwili wa Munga ulisafirishwa jana kwenda Mkoani Kilimanjaro kwa mazishi. Shughuli hiyo ya kuaga mwili wa marehemu ilifanyika Viwanja vya Jeshi Lugalo, Dar es Salaam.

Wanajeshi wa JWTZ waliokuja kumuaga Mwanajeshi mwenzao Marehemu Jovitha Barnaba Munga.


Mama wa Marehemu, Jovitha Barnaba Munga akisaidiwa kuaga mwili wa mwanae.

Baadhi ya waombolezaji ambao ni Askari wenzake Marehemu pamoja na wana familia wakiwa eneo la tukio.

Wanajeshi wa JWTZ wakipita kutoa heshima zao za mwisho kwa Marehemu.





Picha na maelezo kwa hisani ya Father Kidevu blog