Thursday, September 25, 2014

Minister Membe at the Thirteenth Commonwealth Foreign Affairs Ministers Meeting

Hon. Bernard Membe, Tanzania's Minister for Foreign Affairs and also CMAG Chair, register his contribution at the Commonwealth Foreign Affairs Ministers Meeting on Thursday September 25, 2014. Also with him at the Meeting is Tanzania's High Commissioner to the United Kingdom, Amb. Peter  Kallaghe.





Wednesday, September 24, 2014

Hon. Bernard Membe in bilateral talks at the margins of the 69th Session of the United Nations General Assembly

Hon. Bernard Membe in bilateral talks with his New Zealand counter part Hon. Murray McCully, Minister for Foreign Affairs and Trade. Hon. McCully is also the deputy chair of Commonwealth Ministerial Action Group (CMAG) while Minister Membe is the current chair of CMAG. 



Hon. Bernard Membe shaking hands with his Norwegian counterpart Hon. Borge Brende, Minister for Foreign Affairs, before holding bilateral talks along the margins of the 69th Session of the United Nations in New York. 



Hon. Bernard Membe and Tanzania delegation in brief discussion with Commonwealth Secretary General H.E. Kamalesh Sharma during the 69th Session of the United Nations General Assembly in New York. Also present in the picture (bellow) is Amb. Peter Kallaghe, Tanzania High Commissioner to the United Kingdom.



Hon. Bernard Membe in bilateral discussions with H.E. Mr. Pham Binh Minh, Vietnamese Deputy Prime Minister and Minister for Foreign Affairs.  The two leaders discussed briefly on areas of cooperation between Vietnam and Tanzania. 



Hon. Bernard Membe and his Kenyan counterpart Amb. Amina Mohamed, Minister for Foreign Affairs and International Trade. The two met briefly during the 69th Session of the United Nations General Assembly in New York, USA. 



Hon. Bernard Membe and United Kingdom's Minister for Africa Hon. James Philip Duddridge shaking hands after they held brief talks regarding bilateral relations between UK and Tanzania. 






Monday, September 22, 2014

Makamu wa Rais akutana na Balozi wa Norway nchini nawa Tanzania Rwanda

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Balozi wa Norway nchini Tanzania, Hanne Marie Kaarstad, wakatialipofika ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Septemba 22, 2014 kwa mazungumzo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohamed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Norway nchini Tanzania, Hanne Marie Kaarstad, (wa pili kulia) na ujumbe wake baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohamed Gharib Bilal, akimkaribisha Balozi wa Tanzania Rwanda, Mhe.Ali Said Siwa, wakati alipofika ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohamed Gharib Bilal, akizungumza na Balozi wa Tanzania, nchini Rwanda, Mhe.Ali Said Siwa.

---------------------------------------------------------------------------------------------------
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal leo amekutana na mabalozi wa Norway na Balozi mteule wa Tanzania nchini Rwanda na kufanya nao mazungumzo ofisini kwake ikulu jijini Dar es salaam.

Balozi wa Norway nchini Tanzania mheshimiwa Hanne Marie Kaarstad ndiye aliyekuwa wakwanza kufanya mazungumzo na mheshimiwa Makamu wa Rais ambapo licha ya kufika kujitambulisha alimueleza mheshimiwa Makamu wa Rais kuwa atajitahidi kuimarisha uhusiano baina ya nchi hizi mbili katika kipindi chake kama Balozi na kwamba Tanzania ni nchi rafiki kwa Norway na akasisitiza kuzidi kuimarisha uhusiano hasa katika masuala ya utunzaji wa mazingira.

Kwa upande wake mheshimiwa Makamu wa Rais alimueleza Balozi Hanne kuwa, Tanzania inajivunia uhusiano wake na Norway na kwamba uhusiano huo kwa sasa unazidi kuimarika na tena Tanzania inategemea kujifunza mengi toka Norway kutokana na nchi hiyo kuwa miongoni mwa nchi zenye technolojia ya juu katika masuala ya gesi na mafuta.

Balozi Hanne ambaye aliwahi kufanya kazi nchini Tanzania pia alionesha kufurahishwa kwake na maendeleo ambayo Tanzania inapiga na kufafanua kuwa mji wa Dar es Salaam ni kiashiria kimojawapo kinachoonesha wazi kuwa Tanzania inakuwa kwa kasi.

Pia, Mheshimiwa Makamu wa Rais alimpokea Balozi Ali Said Siwa aliyepangiwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Rwanda nakumtaka Balozi huyo kuhakikisha anasaidia mahusiano baina ya nchi zetu kuzidi kuimarika huku akimsisitiza kuhusu uhusiano wetu kama majirani na pia wananchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. 

Balozi Siwa alitumia nafasi hiyo kumshukuru Mheshimiwa Makamu wa Rais kwa uteuzi wake na akaahidi kuiwakilisha vema Tanzania nchini Rwanda.

Sunday, September 21, 2014

Waziri Membe aungana na Wana-Diaspora Marekani Kumuenzi Rais Kikwete kwenye "Usiku wa Jakaya"

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete kwenye meza kuu mara baada ya kuwasili kwenye "Usiku wa Jakaya" ambapo Watanzania waishio nchini Marekani - Diaspora walimpongeza kwa uongozi wake nchini Tanzania. Wengine kwenye meza kuu ni Mhe. Bernard Membe, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Liberata Mulamula Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Mhe. Amina Salum Ali, Balozi wa Umoja wa Afrika nchini Marekani na Bw. George Sebo, Mwenyekiti wa CCM Tawi la DMV, Marekani. 


Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye picha ya pamoja na baadhi ya waandaaji wa "Usiku wa Jakaya" sherehe za kumpongeza Rais Kikwte kwa uongozi bora nchini Tanzania. Sherehe hizo zilifanyika kwenye Hoteli ya JW Marriott jijini Washington DC na kuhudhuriwa na vikundi mbalimbali vya Watanzania wanaoishi nchini Marekani.  
Mhe. Bernard Membe, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Mhe. Liberata Mulamula, Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico wakifurahia jambo wakati wa sherehe za kumpongeza Rais Kikwete zilizofanyika tarehe 19 Septemba 2014, Washington DC nchini Marekani. 

Rais Jakaya Kikwete akipokea tuzo (ya kikombe) kutoka kwa Watanzania waishio Jimboni California wakiongozwa na Balozi wa Heshima Mhe. Ahmed Issa wakati wa kutoa zawadi. Mhe. Rais alipewa zawadi mbalimbali na vikundi vilivyowakilisha Watanzania kutoka Majimbo ya Minnesota, Illinois, California, North Carolina n.k.

Balozi Juma Maharage, Mkuu wa Idara ya Itifaki Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akiwa na Profesa Mohammed Janabi na wageni wengine waalikwa wakifuatilia sherehe hizo zilizofanyika kwenye Hoteli ya Marriott jijini Washington DC.

Balozi Joseph Sokoine, Mkuu wa Idara ya Ulaya na Marekani akiwa na Wasaidiza wa Rais na Wawakilishi wa Exxonmobil (wanaowekeza pia Tanzania) wakifuatilia sherehe hizo.
Baadhi ya watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimatiafa  wakiwa kwenye sherehe za Usiku wa Jakaya

Mhe. Bernard Membe, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwenye picha na Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Chakula na Dawa Tanzania Bw. Hiiti B. Sillo, baada ya sherehe za kumpongeza Rais Kikwete zilizoandaliwa na Watanzania wanaoishi nchini Marekani. 

Mhe. Bernard Membe akimpongeza Balozi wa Heshima Ahmed Issa baada ya sherehe za kumpongeza Rais Kikwete zilizoandaliwa na Wanadiaspora wa Tanzania nchini Marekani. 

Friday, September 19, 2014

Makamu wa Rais akutana kwa mazungumzo na Mwenyekiti wa Shirika la Nyumba la Dubai

Makamu wa Rais  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bilal akisalimiana na Mwenyekiti wa Shirika la Nyumba la  Dubai, Mhe. Ali Rashid Ahmed Lootah alipofika   Ofisi kwake kumsalimia na kufanya nae mazungumzo. Mhe. Lootah alimwelezea Makamu wa Rais dhumuni la ziara yake nchini Tanzania kuwa ni kuangalia nafasi ya uwekezaji katika Sekta ya Utalii, Ujenzi wa Nyumba na Makazi ya watu.
Mwenyekiti wa Shirika la Nyumba la  Dubai, Mhe. Lootah akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili Ofisi ya Makamu wa Rais
Mhe. Dkt. Bilal akizungumza na Mhe. Lootah
Makamu wa Rais, Mhe. Dkt. Bilal akimsikiliza Mhe. Lootah alipokuwa akizungumza naye Ofisini kwake. Kulia kwa Mhe. Dkt. Bilal ni Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mmabo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Simba Yahya.

Mazungumzo yakiendelea.
Makamu wa Rais, Mhe. Dkt. Gharib Bilal akiagana na Mwenyekiti wa Shirika la Nyumba la Serikali ya Dubai  mara baada ya mazungumzo yao
Wakiwa katika picha ya pamoja.

Picha na Reginald Philip

Mwenyekiti wa Shirika la Nyumba la Dubai atembelea Wizara ya Maliasili na Utalii

Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Bi Maimuna Tarishi akisalimiana na Mwenyekiti wa Shirika la Nyumba la Serikali ya Dubai, Mhe. Ali Rashid Ahmed Lootah alipowasili Wizarani hapo na kufanya mazungumzo na baadhi ya viongozi katika Wizara hiyo, Mhe. Lootah katika mazungumzo yake aligusia suala zima la utunzaji vivutio vya utalii na uboreshaji wa miundombinu kwa lengo la kukuza sekta ya Utalii.
Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Bi. Maimuna Tarishi akisalimiana na Balozi Mdogo wa Tanzania, Dubai Mhe. Omar Mjenga 
Bi. Maimuna Tarishi akielezea juu ya vivutio mbalimbali vilivyopo nchini na sifa za vivutio hivyo katika mazungumzo na Mhe. Lootah pamoja na ujumbe alioambata nao pia aliwahamasisha Dubai kuja kuwekeza Tanzania katika Sekta ya Utalii 
Mazungumzo yakiendelea
Kulia ni Mkurugenzi wa Sera na Mipango katika Wizara ya Maliasili na Utalii, Bw Iddi Mfunda  akichangia katika mazungumzo.
Balozi Mdogo,  Omar Mjenga akichangia jambo katika mazungumzo hayo yaliyofanyika Wizara ya Maliasili na Utalii
Mhe. Lootah akichangia jambo wakati wa mazungumzo huku wajumbe wengine wakimsikiliza


Picha ya pamoja



Reginald Philip







Thursday, September 18, 2014

Mwenyekiti wa Shirika la Nyumba la Serikali ya Dubai atembelea mradi wa nyumba za gharama nafuu Kigamboni


Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba ncini Tanzania Mhe. Nehemia Mchechu (wakwanza kushoto), watatu kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Shirika la Nyumba la Serikali ya Dubai Mhe. Ali Rashid Ahmed Lootah, wapili kutoka kulia ni Bwa. Issack Peter, na wakwanza kutoka kulia ni Balozi Mdogo Mhe. Omar Mjenga, watembelea mradi wa nyumba za gharama nafuu za Kigamboni zilizojengwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) mapema leo asubuhi jijini Dar es salaam. 
Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa Mhe. Nehemia Mchechu akimwelezea Mhe. Lootah ubora wa nyumba za mradi wa gharama nafuu (hazipo pichani) zilizojengwa katika eneo hilo la Kigamboni jijini Dar es Salaam
Baadhi ya Nyumba za mradi za gharama nafuu zilizojengwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) katika eneo la Kigamboni.
Balozi Mdogo wa Tanzania, Dubai Mhe. Omar Mjenga akizungumza mara baada ya kumaliza kuangalia mradi wa nyumba hizo za gharama.

Picha na Reginald Philip