Tuesday, April 10, 2018

Balozi Mwinyi azungumza na Wajumbe wa Mkutano wa 8 wa Kijani Zanzibar

Naibu Katibu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Ramadhan Mwinyi Muombwa akizungumza kwenye mkutano wa 8 wa wiki ya Kijani ambao umeingia siku ya pili leo, ambapo katika mkutano wa leo wadau wamejadili kuhusu athari za mionzi itokanayo na vyombo chakavu vya kielektroniki. 
Sehemu ya wajumbe wa Mkutano huo wakimsikiliza Balozi Mwinyi akitoa hotuba yake. 
Balozi Mwinyi akiendelea kuzungumza kwenye Mkutano huo wa 8 wa Wiki ya Kijani unaoendelea kwenye Hoteli ya Sea Cliff Zanzibar, Tanzania.
Dkt. Chaesub Lee naye akizungumza jambo kabla ya wataalamu kuanza kudajili athari za matumizi ya vyombo chakavu vya kielektroniki kwenye Mkutano wa 8 wa Wiki ya Kijani.

Sehemu ya wataalamu wakiendelea na mijadala mbalimbali kwenye mkutano wa 8 wa wiki ya Kijani







OPENING REMARKS BY AMBASSADOR RAMADHANI M. MWINYI,

DEPUTY PERMANENT SECRETARY FOR THE MINISTRY OF FOREIGN AFFAIRS AND EAST AFRICAN COOPERATION,

DURING THE 8TH GREEN STANDARDS WEEK DURING THE
FORUM & TRAINING ON WITH ICTs EVERYWHERE – “HOW SAFE IS EMF?”
SEA CLIFF HOTEL, ZANZIBAR

10TH APRIL, 2018
___________________________

Dr. Maria Sassabo, Permanent Secretary, Ministry of Works, Transportation and Communication;
Dr. Chaesub Lee, Director, Telecommunication Standardization Bureau, ITU;
Distinguished Participants;
Ladies and Gentlemen;

It is my pleasure to welcome you all to a second day of the 8th Green Standard Week. The topic for today’s discussion is very impressive.  We are going to see how safe is the Exposure to Electromagnetic Fields (EMF).  We are lucky to have experts who will make presentations on the topic, including activities of the ITU on Human Exposure to EMFs.   I wish to thank all the experts gathered here today and the organizers for a job well done.

Distinguished participants; as you are all aware exposure to human made   electromagnetic fields have increased over the past years. The deployment of different sources of EMF to cater for the telecommunication and ICT needs of the population has developed very rapidly; the use of mobile phones and other wireless system is expanding rapidly all over the world.  This is because of strong competition, quality of service requirements, network coverage extension and introduction of new technologies. 

ITU estimates that 95 percent of the global population lives in an area that is covered by a mobile –cellular network. For the case of Tanzania, there are almost over 45 million mobile – cellular subscribers.

While this expansion provides the opportunity for advances in public and personal safety, education, medicine and the economy, it also brings new responsibilities and challenges to all of us.

It is undeniable fact that the widespread use of EFM sources has possible adverse effects of prolonged exposure to emissions on people’s health. Unfortunately, the EFM is unknown and undetectable for the people; there is lack or limited regulations; and also there is rare mechanism to inform the people.  That’s why ITU as an institution remains extremely relevant in the world today and in the future in designing activities to mitigate effects of EFM due to radio systems and mobile equipment to human beings.

There is a need for the ITU to come up with a global framework and standard that will help to facilitate compliance with international standards; strengthening international technical cooperation and capacity building as well as strengthening collaboration among stakeholders like the World Health Organization.

Distinguished participants; I do understand that the health impact of electromagnetic fields similarly falls within the mandate of the World Health Organization (WHO) in the area of environmental health. The WHO came up with EMF project to respond to the general concern over health effects of EMF exposure in 1996.  That’s why today we are going to hear from the WHO representative on EMF research and future needs.
I wish to welcome you all to openly discuss, share and exchange experiences, knowledge, challenges and possible solutions. It is through these discussions that will enable ITU to come with the standards and framework we are aspiring too.

Before I handover to our moderator to proceed, on behalf of us all, I want to say KARIBUNI SANA. It is a pleasure to see so many of you here. I wish you all successful deliberations in this Forum and Training.


ASANTENI SANA…!!!!

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI



ZIARA YA WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA POLAND NCHINI 11-13 APRILI 2018

Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Poland, Mhe. Prof. Jacek Craputowicz atafanya ziara ya kikazi nchini Tanzania kuanzia tarehe 11 hadi 13 Aprili 2018.  Katika ziara hiyo, Prof. Craputowicz pamoja na mambo mengine, atafanya mazungumzo na mwenyeji wake, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb) Jijini Dar Es Salaam tarehe 12 Aprili 2018.  Viongozi hao watajadili namna ya kuboresha mahusiano na mashirikiano ya kidiplomasia baina ya Tanzania na Poland, hususan katika eneo la uwekezaji na biashara.   

Poland ni moja ya nchi zinazounga mkono Sera ya Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ya kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda ifikapo mwaka 2020. Katika kuunga mkono Sera hiyo, Serikali ya Poland imetoa mkopo wa masharti nafuu wa Dola za Marekani milioni 110 kwa Serikali ya Tanzania.

Kati ya fedha hizo, Dola za Marekani milioni 55 zimetumika kujenga kiwanda cha kuunganisha matrekta Wilayani Kibaha, Mkoani Pwani ambacho kimeshaanza kazi na Dola za Marekani milioni 55 ni kwa ajili ya kujenga maghala ya kuhifadhia mazao ya kilimo katika mikoa minane ya Rukwa, Katavi, Manyara, Ruvuma, Dodoma, Shinyanga, Njombe na Songwe.

Prof. Craputowicz na mwenyeji wake watashiriki hafla fupi ya uzinduzi rasmi wa ofisi ya Ubalozi wa nchi hiyo zilizopo nyumba namba 15, mtaa wa Mtwara, Masaki Jijini Dar es Salaam tarehe 12 Aprili 2018. Poland ilifungua upya Ubalozi wake nchini mwaka 2017 baada ya kuufunga mwaka 2008 na kabla ya hapo nchi hiyo ilikuwa inawakilishwa kutokea Nairobi, Kenya.

Baada ya ufunguzi viongozi hao watafanya mkutano na waandishi wa habari kwenye ofisi hizo saa tano asubuhi. 

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dar es Salaam
 10 Aprili, 2018

Naibu Waziri akutana na kufanya mazungumzo na Mabalozi

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Susan Kolimba (kulia) akiwa katika mazungumzo na Mhe. Balozi Lt. Jen Wynjones Matthew aliyekuwa akihudumu Ubalozi wa Tanzania Moscow, Urusi. Mhe. Balozi Matthew amerejea nchini baada ya kumaliza muda wake. Mhe. Naibu Waziri amekutana na Mabalozi hao Ofisini kwake mjini Dodoma ambapo walijadili masuala mbalimbali ya namna kudumisha uhusiano wa kidiplomasia na nchi husika ambazo Mabalozi hao wanaiwakilisha nchi, sambamba na kuibua maeneo mapya ya ushirikiano na nchi hizo.

Naibu Waziri Mhe.Dkt. Kolimba akiwa katika mazungumzo na Mabalozi wanaotarajia kwenda kuripoti kwenye vituo vyao vya uwakilishi hivi karibuni. Kulia ni Inspekta Jenerali mstaafu Mhe. Balozi Ernest Jumbe Mangu anayetarajiwa kwenda kuiwakilisha Tanzania Kigali, Rwanda hivi karibuni na kushoto ni Meja Jenerali Mstaafu Mhe. Balozi Mumwi Simoni anayekwenda kuiwalisha Tanzania Moscow,Urusi

Monday, April 9, 2018

Minister Mbarawa's Speech at the 8th Green Standards Week, April 9-12, 2018 Zanzibar, Tanzania

Hon. Prof. Makame Mnyaa Mbarawa (MP.), Minister for Works, Transport and Communication of the United Republic of Tanzania delivering key note address to the 8th Green Standards Week, 9-12 April, 2018 at Sea Cliff Zanzibar Tanzania.


Honourable Dr. Sira Ubwa Mwamboya, Minister for Infrastructure, Transport and Communication, Revolutionary Government of Zanzibar;
Dr. Maria Sasabo, Permanent Secretary (Communication), Ministry of Works, Transport and Communication;
Ambassador Ramadhan Mwinyi, Deputy Permanent Secretary, Ministry of foreign Affairs and East African Cooperation;
Dr. Chaesub Lee, Director, Telecommunication Standardization Bureau, ITU;
Eng. James Kilaba, Director General, Tanzania Communications Regulatory Authority;
Eng. Peter Ulanga, Chief Executive Officer, Universal Communications Service Access Fund (UCSAF);
Your Excellencies;
Distinguished Delegates,
Member of the press;
Ladies and Gentlemen,

It is the utmost honour to the United Republic of Tanzania to welcome all participants as a host country of the 8th Green Standards Week. Allow me on behalf of the Government of the United Republic of Tanzania to commend the work done by the ITU, UN Habitat, United Nations University (UNU), United Nations Industrial Development Organization​(UNIDO), Basel Convention and UN Environment, Universal Communications Service Access Fund (UCSAF), Tanzania Communications Regulatory Authority (TCRA) and the organizing committee for preparation of this important meeting; and I once again welcome you all in this beautiful Zanzibar, Tanzania.  Karibuni sana.

Ladies and gentlemen,
Since the Green Standards Week is a global platform for discussion and knowledge-sharing; I would like each participant to use this forum to raise awareness on importance and opportunities for using information and communication technologies (ICTs) to protect the environment, unlock the potential of circular economy and expedite the transition to smart sustainable cities.  As ICT stakeholders, therefore, our main task should be to ensure that ICT support efforts of environmental conservation and that no one is left behind when it comes to effective utilization of ICT for eradication of negative impacts associated with use of ICT including; Carbon emissions, radiation and e-waste. This year’s theme “Linking of Circular economy and industry 4.0” has come at the right time when Tanzania is embracing nationwide policy “Nurturing Industrialization for Economic Transformation and Human Development”.

Ladies and gentlemen,
Allow me to share briefly Tanzania’s efforts and experiences towards the development of ICT and facilitation of Linking Circular Economy and Industry 4.0.   The Government of the United Republic of Tanzania recognizes the important role of ICT for rapid socio-economic growth in its aspiration to become a middle-income economy by 2025 and attain the Government policy on industrialization. To facilitate effective adoption and utilization of ICTs, the Government has been setting pro-ICT policies and supportive legal, regulatory and institutional frameworks.
The National ICT Policy 2016 provides a comprehensive framework for guiding the development and growth of the sector to ensure optimal benefits to the nation and its citizens. This policy addresses a wide range of issues including of e-waste management, environment conservation, ICT safety, ICT Human Capital Development and raising awareness to the public on different matters pertaining to ICTs. Specifically, the Policy states “the Government shall put in place appropriate mechanisms for electronic waste (e-waste) management for safety of people and environment protection”. In addition, National Environment Policy (1997) and associated regulations sets overall framework for environmental management issues in the country that includes e-waste management.
In total, the National policies, legal, regulatory, institutional and converged licensing framework has served as a catalyst for stimulating the ICT development and economic growth.

Ladies and Gentlemen,
To promote growth in ICT, Tanzania adopted a technology neutral license framework.   This resulted in Construction of broadband infrastructures with over 25,000 Km Optic Fiber Cable connects all regions, link to neighbouring countries as well as to the undersea cables of Seacom and Eassy landing on the shores. Tanzanians are already enjoying the benefits, as prices of Internet access and core transmission have dropped significantly. Furthermore, the licencing of nine mobile network operators in the country has proven to be an important tool in bridging the digital gap between rural and urban areas. We are working hard to make sure the few remaining unconnected areas will be connected soon as we need to see all people in the country participate fully in the digital economy.

Ladies and gentlemen,
Accompanying the deployment and utilization of ICTs within the economy and society we have experienced some challenges in the areas of e-Waste, security safety and health related risks from radiation. With a highly competition environment, erection of towers and related equipment are not avoidable.  From the rapid change of technologies, including migration to digital TV transmission, evolvement of mobile phone from analogue in the beginning of 2000 to Internet IP based smart gadgets within a short period has left a number of unused electronic equipment.  
Frequent changes is seen as Providing a safe environment for digital participation is crucial in facilitating effective use of ICT for sustainable development.  Moreover, Frequent change in technology provide little time for field testing before mass marketing and  if not closely monitored may result in health related risk, while wide capabilities of tools may infringe the security and safety if not well managed.   These challenges becomes of high concern for developing countries that depend on imports for most of ICT solutions.

Ladies and Gentlemen,
Provision of a safe environment for digital participation is crucial in facilitating effective use of ICT for sustainable development.  Efforts that the Government of Tanzania has taken to address these issues include putting in place Electronic and Postal Communications Regulations on Equipment Standards and establishment of Central Equipment Identification Register (CEIR). Furthermore, The quality of service regulations addresses radiation Protection. The Government has banned usage in Tanzania of counterfeit equipment from 2016 to address for security, safety and environment concerns.
Despite these efforts and commitments, there are still challenges such as public understanding of e-waste management and safety related issues; lack of appropriate frameworks that address disposing electronic products after its use; and information treatment; with the industrialization initiative being implemented, we look forward to establish recycling industries and building necessary capacity for e-waste management so as to curb the situation.     

Ladies and Gentlemen
We look forward in this forum to share experience and expertise and through networking and discussions. I urge the forum to contemplate on how we could establish a centralized resource in the region for efficient utilization of resources to a viable project in e-waste management.


Ladies and Gentlemen,
In line with all the above, It is crucial to increase local skilled and competent ICT human resources base in our countries. The skills will lead to; Innovation and Entrepreneurship in ICTs; Research and Development in ICT; Development of industries to manufacture and assemble ICT products; and Proper policies for adoption of new emerging technologies and solutions like Internet of Things (IoT) and Over the Top (OTT).
It is through the ITU that we will continue to get a frameworks and standards.  All that is required is to be ready to collaborate and share experiences with the ITU and each other member in order to make the initiatives a reality.                
Ladies and Gentlemen,
This forum is important for deliberating and knowledge sharing in raising awareness on environmental protection, circular economy and the transition to smart sustainable cities. It is my great expectation that as a team the experiences we share will help in implementation of the UN 2030 Agenda for Sustainable Development as well as the ITU’s Connect 2020 Agenda for Global Telecommunication /ICT Development and the National and sector specific policies in our countries. I believe, these will be attainable through (i) Human and institutional capacity development; (ii) Fostering innovation and industrialization especially in developing countries.

Ladies and gentlemen,
Finally, I wish to reiterate Tanzania’s commitment to co-operate with other members and the ITU in enhancing socio-economic development of all member states through ICT.  Once again, on behalf of the Government and people of Tanzania, I would like to express profound gratitude to the ITU for considering the United Republic of Tanzania as a host of this remarkable 8th Green Standards Week, and wish you success in all the deliberations.

Asante sana


Mkutano wa Kimataifa wa Nane wa Wiki ya Kijani

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa (Mb.) akihutubia kwenye Mkutano wa Nane wa Wiki ya Kijani, unaowakutanisha wadau mbalimbali wanao simamia na kutengeneza vifaa na miundombinu mbalimbali ya Tehama. Mkutano huo unatarajia kuangalia namna mbalimbali za kupambana na matumizi ya Tehama yanayochafua mazingira;  umehudhuriwa na viongozi mbalimbali kutoka Serikalini ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, akiwemo Waziri wa Ujenzi, Usafirishaji na Mawasiliano Zanzibar Dkt. Sira Ubwa (Mb.), Katibu Mkuu (Mawasiliano) Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Dkt. Maria Sasabo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Ramadhan Mwinyi, Mkurugenzi wa ITU (International Telecomunication Union), Dkt. Chaesub Lee, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania, Mhandisi Kilaba. Mkutono huo unafanyika katika Hoteli ya Sea Clif Mangapwani, Zanzibar kuanzia tarehe 9-12, Aprili 2018.
Waziri wa Ujenzi, Usafirishaji na Mawasiliano Zanzibar, Dkt. Sira Ubwa, akiwakaribisha wajumbe wa mkutano huo visiwani Zanzibar na kuelezea faida ya mkutano kufanyikia Unguja. Alisema kwa mazingira ya sasa, changamoto iliyopo mbele yetu ni kushirikiana kwa pamoja ili kuziepusha nchi zetu na uharibifu utokanao na matumizi ya vifaa chakavu vya kielektroniki. Mhe. Dkt. Sira alitumia fursa hiyo kuwapongeza kwa mjadala muhimu utakaoendelea wa utunzaji wa mazingira na kuwasihi wasiache kutembelea vivutio vya asilia vilivyopo visiwani humo.   
Mkurugenzi wa International Telecommunication Union (ITU) Dkt. Lee akizungumza kuhusu mjadala na maazimio ya mkutano huo muhimu wa kimataifa wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa 8 wa Wiki ya Kijani.


(Juu na Chini) Sehemu ya wajumbe na washiriki mbalimbali wa mkutano huo wakifuatilia kwa makini hotuba za viongozi wakati wa ufunguzi wa mkutano.


Mkutano ukiendelea
Waziri wa Ujenzi, Usafirishaji na Mawasiliano Zanzibar, Dkt. Sira Ubwa, akifurahia jambo na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakati wa vikao vya pembezoni wakati wa Mkutano wa Nane wa Wiki ya Kijani.
Balozi Mwinyi akielezea jambo huku Dkt. Ubwa na Dkt. Sasabo wakimsikiliza.
Picha ya pamoja mara baada ya kumalizika kwa ufunguzi wa Mkutano wa 8 wa Wiki ya Kijani, unaoendelea kwenye Hoteli ya Sea Cliff Zanzibar tarehe 9-12, Aprili, 2018.