Monday, March 29, 2021
MABALOZI WANAOIWAKILISHA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA NJE YA NCHI WAHIMIZWA KUONGEZA JUHUDI ZA KUTAFUTA MASOKO
Friday, March 26, 2021
RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA AONGOZA VIONGOZI, WANANCHI KUMUAGA HAYATI JPM
Habari picha za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiongoza viongozi mbalimbali wa Serikali, taasisi binafsi, mashirika ya kimataifa, dini na wananchi kutoka Chato na mikoa jirani katika mazishi ya aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kijijini kwake Chato mkoani Geita.
Thursday, March 25, 2021
MAKAMU WA PILI WA RAIS ZANZIBAR AONGOZA WAKAZI WA GEITA NA MIKOA JIRANI KUMUAGA JPM
Na Mwandishi Wetu, Geita
Makamu
wa pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdullah amewaongoza wakazi wa
Geita na mikoa jirani kuaga mwili wa
aliyekuwa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati John Pombe
Magufuli katika uwanja wa Magufuli Chato mkoani Geita.
Akizungumza katika shughuli hiyo ya
kuuaga mwili wa hayati Magufuli Wilayani Chato, Makamu wa pili wa Rais wa
Zanzibar ambaye pia ni mwenyekiti mwenza wa kamati ya mazishi kitaifa amewasihi
Watanzania kuendelea kushikamana katika kulijenga taifa, ambalo Magufuli
ameliacha salama na lenye heshima.
Makamu
wa pili wa Rais wa Zanzibar, amesema ni wajibu wa viongozi na Watanzania
kuungana kuenzi mazuri yote aliyofanya Hayati Magufuli na kuendeleza sera zake
za kuchapa kazi, kupiga vita rushwa na ubadhirifu na kuweka mbele uzalendo na
maslahi ya taifa.
Mazishi
ya Hayati Dkt. Magufuli yatafanyika Ijumaa Machi 26, 2021 katika makaburi ya
familia kijijini kwake Chato mkoani Geita.
Mawaziri
mbalimbali pamoja na viongozi waandamizi wa Serikali wakiwa katika uwanja wa
Magufuli tayari kwa zoezi la kuaga mwili wa aliyekuwa Rais wa Tano wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli katika uwanja wa
Magufuli Chato mkoani Geita
Katibu
wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi-Zanzibar, Mhandisi Zena Ahmed
Said akiteta jambo na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika
Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge katika uwanja wa Magufuli wakati
wa zoezi la kuaga mwili wa aliyekuwa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli Chato mkoani Geita
Katibu
Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Bashiru Ally akiteta jambo na Waziri wa Mambo ya Nje
na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) katika
uwanja wa Magufuli wakati wa zoezi la kuaga mwili wa aliyekuwa Rais wa Tano wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli Chato mkoani
Geita
Katibu
Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia
Jenerali Wilbert Ibuge akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa aliyekuwa Rais wa
Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli Chato
mkoani Geita
Katibu
Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia
Jenerali Wilbert Ibuge akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Ofisi
ya Mkuu wa Wilaya ya Chato kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Tano wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli Chato mkoani Geita
Katibu
Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia
Jenerali Wilbert Ibuge akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa aliyekuwa Rais wa
Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli Chato
mkoani Geita
Waziri
wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John
Kabudi (Mb) akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Wilaya
ya Chato kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli Chato mkoani Geita
Waziri
wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John
Kabudi (Mb) akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Wilaya
ya Chato kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli Chato mkoani Geita
Wednesday, March 24, 2021
MSAFARA WA HAYATI MAGUFULI KUELEKEA GEITA - CHATO
Picha mbalimbali za msafara
wa aliyekuwa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John
Pombe Magufuli ukielekea Chato mkoani Geita leo tarehe 24 Machi 2021
VIONGOZI WAKUU WA NCHI NA SERIKALI DUNIANI WASAINI KITABU CHA MAOMBOLEZO YA JPM
Rais
wa Burundi Mhe. Èvariste Ndayishimiye akisaini kitabu cha maombolezo katika
ubalozi wa Tanzania nchini Burundi kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli
Rais wa Ethiopia Mhe. Sahle-Work Zewde akisaini kitabu cha maombolezo katika ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli
WAZIRI MKUU AONGOZA WAKAZI WA MWANZA KUMUAGA JPM
Na
Mwandishi wetu, Mwanza
Waziri
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa ameongoza maelfu
ya wakazi wa Jiji la Mwanza na mikoa jirani kuaga mwili wa aliyekuwa Rais wa
awamu ya tano hayati Dkt. John Pombe Magufuli.
Waombolezaji
walianza kuingia uwanjani leo alfajiri na wengine wakiwa wamejipanga barabarani
kuulaki msafara wa mwili wa Hayati Magufuli ukitokea Zanzibar.
Mhe.
Majaliwa aliongozana na mawaziri, naibu mawaziri, makatibu wakuu na viongozi wa
taasisi za umma na binafsi katika hafla ya kutoa heshima za mwisho kwa kwa
hayati Dkt. Magufuli anayetarajiwa kuzikwa nyumbani kwake Chato Machi 26, 2021.
Wengine waliohudhuria ni pamoja na wakuu wote wa vyombo vya ulinzi na usalama wakiongozwa na Mkuu wa Majeshi Jenerali Venance Mabeyo.
Waziri
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akitoa salamu za
pole kwa wananchi wa Mwanza katika hafla kuaga mwili wa aliyekuwa Rais wa awamu
ya tano hayati Dkt. John Pombe Magufuli
Makamu
wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla
akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof.
Palamagamba John Kabudi (Mb) wakati alipowasili katika uwanja wa CCM Kirumba
Jijini Mwanza katika hafla kuaga mwili wa aliyekuwa Rais wa awamu ya tano hayati
Dkt. John Pombe Magufuli
Makamu
wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla
akitoa heshima za mwisho katika uwanja wa CCM Kirumba wakati wa kuaga mwili wa
aliyekuwa Rais wa awamu ya tano hayati Dkt. John Pombe Magufuli
Balozi
wa Tanzania nchini Sweden, Mhe. Dkt. Wilbroad Slaa akitoa heshima za mwisho kwa
aliyekuwa Rais wa awamu ya tano hayati Dkt. John Pombe Magufuli katika uwanja
wa CCM Kirumba
Wananchi
wa Jiji la Mwanza wakiwa barabarani kushuhudia msafara uliobeba mwili wa aliyekuwa
Rais wa awamu ya tano hayati Dkt. John Pombe Magufuli |