Monday, March 29, 2021

MABALOZI WANAOIWAKILISHA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA NJE YA NCHI WAHIMIZWA KUONGEZA JUHUDI ZA KUTAFUTA MASOKO

Mabalozi wanaoiwakilisha Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nje ya Nchi wameelekezwa kujipanga, kushiriki na kutafuta fursa zitakazowezesha bidhaa mbalimbali za Tanzania kupata masoko ya uhakika katika nchi walizopo.

Agizo hilo limetolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi wakati akizungumza na mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania nje ya nchi na kuongeza kuwa , Ilani ya Chama cha Mapinduzi inatamka bayana juu ya diplomasia ya uchumi sambamba na kuimarisha sauti ya Tanzania na taswira yake katika medani ya uhusiano wa kikanda na kimataifa. 

Prof. Kabudi ameongeza kuwa ili kufanikisha hilo Balozi zinapaswa kuimarisha ushiriki wa Tanzania katika jumuiya nyingine za kimataifa zikiwemo, Indian Ocean Rim Association, Indian Ocean Tuna Commission, South South Commission, South West Indian Ocean Fisheries Commission.

Aidha amewataka Mabalozi hao kuzingatia maelekezo ya Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi aliyoyatoa wakati akizundua Baraza la Wawakilishi ya kutaka Uchumi wa Bluu kupitia uvuvi wa Bahari Kuu unakuwa na manufaa kwa Wananchi hususani katika kuongeza mapato, ajira na kukuza uchumi kwa kuzingatia kuwa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ni ya Muungano. 

Pia Prof. Kabudi amesema Serikali inatambua na kuthamini mchango unaotolewa na Watanzania waishio nje ya nchi (Diaspora) katika maendeleo ya Taifa na kuzielekeza Balozi zianze na ziboreshe kanzi data ya Diapora ikiwa ni pamoja na kuwahimiza kuanzisha Jumuiya zao. 

“Natambua kazi hiyo inaendelea na kwa sasa tuna data za diaspora takriban 98,658 na kuna jumuiya 77 za diaspora. Nichukue fursa kusisitiza umuhimu wa Balozi zetu kuboresha na kuharakisha zoezi hili kwa kubuni njia mbalimbali za kuwaandikisha”. Amesema Prof. Kabudi

Mkutano huo wa Prof. Palamagamba John Kabudi, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania nje ya nchi umehudhuriwa pia na Naibu Waziri, Mhe William Tate Ole Nasha, Katibu Mkuu Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge, Wakurugenzi na Wakuu wa Idara na Vitengo wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palagamba John Kabudi (Mb) akisisitiza jambo kwenye Kikao kazi na Mabalozi wanaoiwakilisha Jamhuri ya Muungano wa Tanzania sehemu mbalimbali Duniani pamoja na Wakuu wa Idara na Vitengo kilichofanyika jijini Dodoma

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.  William Tate Olenasha (Mb) akizungumza na Mabalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wanaoiwakilisha nchi sehemu mbalimbali Duniani pamoja na Wakuu wa Idara na Vitengo kwenye kikoa kazi kilichofanyika jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Brigedia Jenerali Wilbert A. Ibuge akisisitiza jambo katika Kikao kazi katika ya Mhe. Prof Kabudi na Mabalozi wanaoiwakilisha Jamhuri ya Muungano wa Tanzania sehemu mbalimbali Duniani pamoja na Wakuu wa Idara na Vitengo kilichofanyika jijini Dodoma.

Sehemu ya Mabalozi na Wakuu wa Idara na Vitengo wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palagamba John Kabudi (Mb) kwenye Kikao Kazi kilichofanyika jijini Dodoma. 

Sehemu nyingine ya Mabalozi na Wakuu wa Idara na Vitengo wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palagamba John Kabudi (Mb) kwenye Kikao Kazi.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palagamba John Kabudi (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi wanaoiwakilisha Jamhuri ya Muungano wa Tanzania sehemu mbalimbali Duniani mara baada ya Kikao kazi kilichofanyika jijini Dodoma.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palagamba John Kabudi (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Idara na Vitengo baada ya Kikao Kazi kilichofanyika jijini Dodoma
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palagamba John Kabudi (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi wanaoiwakilisha Jamhuri ya Muungano wa Tanzania sehemu mbalimbali Duniani mara baada ya kuhitimisha Kikao kazi kilichofanyika jijini Dodoma.

TANGAZO LA FURSA ZA UFADHILI WA MASOMO




 

VACANCY ANNOUNCEMENT


 

Friday, March 26, 2021

RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA AONGOZA VIONGOZI, WANANCHI KUMUAGA HAYATI JPM

 Habari picha za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiongoza viongozi mbalimbali wa Serikali, taasisi binafsi, mashirika ya kimataifa, dini na wananchi kutoka Chato na mikoa jirani katika mazishi ya aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kijijini kwake Chato mkoani Geita.































Thursday, March 25, 2021

MAKAMU WA PILI WA RAIS ZANZIBAR AONGOZA WAKAZI WA GEITA NA MIKOA JIRANI KUMUAGA JPM

 Na Mwandishi Wetu, Geita

Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdullah amewaongoza wakazi wa Geita na mikoa jirani kuaga mwili wa aliyekuwa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati John Pombe Magufuli katika uwanja wa Magufuli Chato mkoani Geita.

 

Akizungumza katika shughuli hiyo ya kuuaga mwili wa hayati Magufuli Wilayani Chato, Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar ambaye pia ni mwenyekiti mwenza wa kamati ya mazishi kitaifa amewasihi Watanzania kuendelea kushikamana katika kulijenga taifa, ambalo Magufuli ameliacha salama na lenye heshima.

Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar, amesema ni wajibu wa viongozi na Watanzania kuungana kuenzi mazuri yote aliyofanya Hayati Magufuli na kuendeleza sera zake za kuchapa kazi, kupiga vita rushwa na ubadhirifu na kuweka mbele uzalendo na maslahi ya taifa.

Mazishi ya Hayati Dkt. Magufuli yatafanyika Ijumaa Machi 26, 2021 katika makaburi ya familia kijijini kwake Chato mkoani Geita.

Mawaziri mbalimbali pamoja na viongozi waandamizi wa Serikali wakiwa katika uwanja wa Magufuli tayari kwa zoezi la kuaga mwili wa aliyekuwa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli katika uwanja wa Magufuli Chato mkoani Geita


Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi-Zanzibar, Mhandisi Zena Ahmed Said akiteta jambo na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge katika uwanja wa Magufuli wakati wa zoezi la kuaga mwili wa aliyekuwa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli Chato mkoani Geita


Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Bashiru Ally akiteta jambo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) katika uwanja wa Magufuli wakati wa zoezi la kuaga mwili wa aliyekuwa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli Chato mkoani Geita


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa aliyekuwa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli Chato mkoani Geita


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Chato kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli Chato mkoani Geita


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa aliyekuwa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli Chato mkoani Geita


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Chato kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli Chato mkoani Geita


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Chato kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli Chato mkoani Geita



Wednesday, March 24, 2021

WAZIRI MKUU WA INDIA NA JAPAN PAMOJA NA NAIBU WAZIRI MKUU WA OMAN WAANDIKIA BARUA YA KISERIKALI KWA RAIS MHE. SAMIA SULUHU HASSAN KWA SALAMU ZA RAMBIRAMBI NA PONGEZI



 

MSAFARA WA HAYATI MAGUFULI KUELEKEA GEITA - CHATO

Picha mbalimbali za msafara wa aliyekuwa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli ukielekea Chato mkoani Geita leo tarehe 24 Machi 2021














VIONGOZI WAKUU WA NCHI NA SERIKALI DUNIANI WASAINI KITABU CHA MAOMBOLEZO YA JPM

 

Rais wa Burundi Mhe. Èvariste Ndayishimiye akisaini kitabu cha maombolezo katika ubalozi wa Tanzania nchini Burundi kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli 


Rais wa Ethiopia Mhe. Sahle-Work Zewde akisaini kitabu cha maombolezo katika ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli

Naibu Waziri Mkuu anayeshughulikia Masuala ya Ulinzi wa Serikali ya Oman, Mtukufu Sayyid Shihab bin Tarik bin Taimur Al-Said, akisaini kitabu cha maombolezo ya msiba wa aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli 

 


WAZIRI MKUU AONGOZA WAKAZI WA MWANZA KUMUAGA JPM

Na Mwandishi wetu, Mwanza

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa ameongoza maelfu ya wakazi wa Jiji la Mwanza na mikoa jirani kuaga mwili wa aliyekuwa Rais wa awamu ya tano hayati Dkt. John Pombe Magufuli.

Waombolezaji walianza kuingia uwanjani leo alfajiri na wengine wakiwa wamejipanga barabarani kuulaki msafara wa mwili wa Hayati Magufuli ukitokea Zanzibar.

Mhe. Majaliwa aliongozana na mawaziri, naibu mawaziri, makatibu wakuu na viongozi wa taasisi za umma na binafsi katika hafla ya kutoa heshima za mwisho kwa kwa hayati Dkt. Magufuli anayetarajiwa kuzikwa nyumbani kwake Chato Machi 26, 2021.

Wengine waliohudhuria ni pamoja na wakuu wote wa vyombo vya ulinzi na usalama wakiongozwa na Mkuu wa Majeshi Jenerali Venance Mabeyo.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akitoa salamu za pole kwa wananchi wa Mwanza katika hafla kuaga mwili wa aliyekuwa Rais wa awamu ya tano hayati Dkt. John Pombe Magufuli


Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) wakati alipowasili katika uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza katika hafla kuaga mwili wa aliyekuwa Rais wa awamu ya tano hayati Dkt. John Pombe Magufuli


Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla akitoa heshima za mwisho katika uwanja wa CCM Kirumba wakati wa kuaga mwili wa aliyekuwa Rais wa awamu ya tano hayati Dkt. John Pombe Magufuli


Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mhe. Dkt. Wilbroad Slaa akitoa heshima za mwisho kwa aliyekuwa Rais wa awamu ya tano hayati Dkt. John Pombe Magufuli katika uwanja wa CCM Kirumba    

Wananchi wa Jiji la Mwanza wakiwa barabarani kushuhudia msafara uliobeba mwili wa aliyekuwa Rais wa awamu ya tano hayati Dkt. John Pombe Magufuli