Sunday, February 12, 2012

Waziri Membe ahudhuria Mkutano wa Helsinki+10


Mhe. Waziri Bernard K. Membe (kushoto), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akiwa katika maongezi na Mhe. Dkt. Asha-Rose Migiro (katikati), Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN) na Mhe. Mary Robinson (kulia), Rais Mstaafu wa Ireland, katika VIP ya uwanja wa ndege wa kimataifa jijini Helsinki, Finland leo tarehe 12 Februari, 2012.
Waziri Membe yuko nchini Finland kuhudhuria Mkutano wa Helsinki+10, ambapo Mhe. Membe ni Mwenyekiti Mwenza wa Mchakato huo.


Mhe. Mary Robinson (kulia), Rais Mstaafu wa Ireland akiwa katika maongezi na jambo na Waziri Bernard K. Membe (2-kushoto), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Asha-Rose Migiro (2-kulia), Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN) na Mhe. Balozi Muhammed Mwinyi Haji Mzale, Balozi wa Tanzania nchini Sweden na Finland.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.