Wednesday, March 13, 2013

Mhe. Membe akutana kwa mazungumzo na Waziri wa Biashara wa Ireland


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb), akizungumza na Waziri wa Nchi wa Ireland anayeshughulikia masuala ya Biashara na Maendeleo, Mhe. Joe Costello alipofika Wizarani kwa mazungumzo na Mhe. Waziri Membe kuhusu kukuza  ushirikiano kati ya nchi hizi mbili na pia kuimarisha ushirikiano katika masuala ya biashara na uwekezaji.

Mhe. Membe akiendelea na mazungumzo na Mhe. Costello. Wengine katika picha ni Balozi Dora Msechu (kushoto), Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Balozi Naimi Aziz (kulia), Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda.

Mhe. Membe katika mazungumzo na Mhe. Costello. Wengine katika picha ni ujumbe uliofuatana na Waziri huyo wa Ireland akiwemo Balozi wa Ireland hapa nchini, Mhe. Fionnuala Gilsenan (wa kwanza kulia)

Mhe. Costello akifafanua jambo kwa Mhe. Membe.

Ujumbe wa Ireland wakati wa mazungumzo.

Balozi Msechu (kushoto),  Balozi Naimi (katikati) pamoja na Bi. Zainabu Angovi (kulia) wakisikiliza mazungumzo kati ya Mhe. Membe na Mhe. Costello (hawapo pichani)

Mhe. Membe akijadili jambo na Mhe.  Fionnuala Gilsenan, Balozi wa Ireland hapa nchini huku Mhe. Costello akisikiliza.

Mhe. Membe akiagana na Mhe. Costello mara baada ya mazungumzo yao.

Tuesday, March 12, 2013

Tanzania to host the African Institute of International Law


Hon. Bernard K. Membe (MP), Minister for Foreign Affairs and International Co-operation today met with Ambassador Sani L. Mohammed, Project Coordinator of the the African Institute of International (AIIL) in his office in Dar es Salaam.  AILL was established in January 2002 by the Regional International Institution through the African Union.   

Hon. Membe signs an Agreement on behalf of the Government of the United Republic of Tanzania together with Ambassador Mohammed, who signs as a Project Coordinator of the soon to be established the African Institute of International Law (AIIL) in Arusha region.  Ambassador Mohammed formerly served as a Principal Diplomat of the Republic of Nigeria to the United States and a former Nigerian Ambassador in Egypt.  

Hon. Membe and Ambassador Mohammed holding signed Agreements of the African Institute of International Law (AIIL) to be built in Arusha region. 

Early discussion between the Honorable Minister Membe (center), Ambassador Mohammed (left) and Ambassador Irene Kasyanju (right), Director of Legal Affairs Unit in the Ministry of Foreign Affairs and International Co-operation. 

Hon. Bernard K. Membe (MP), expressing his views about the AIIL as aspired to be an institute of excellence which will attract people from all areas including SADC region.  

Hon. Bernard K. Membe (MP), Minister for Foreign Affairs and International Co-operation congratulates Ambassador Sani L. Mohammed, Projector Coordinator for the establishment of the African Institute of International Law (AIIL).

Hon. Minister Membe congratulates Ambassador Kasyanju after the signing of the Agreements of the African Institute of International Law (AIIL).

Hon. Membe congratulates Mr. Ali Ubwa (left), Foreign Service Officer in the Ministry of Foreign Affairs, while Ambassador Mohammed witnessing the occasion. 

A group photo with Hon. Minister Membe who is expressing his excitement about the establishment of the African Institute of International Law (AIIL) in Arusha. 

Ambassador Kasyanju arranging the Agreements thoroughly before handing them over to Ambassador Mohammed (center).  Other in the photo is Mr. Ali Ubwa, Foreign Service Officer in the Ministry of Foreign Affairs. 

Ambassador Irene Kasyanju, Director of Legal Affairs Unit in the Ministry of Foreign Affairs and International Co-operation in discussion with Ambassador Sani L. Mohammed, Project Coordinator of the African Institute of International Law (AIIL).



All photos by Tagie Daisy Mwakawago 



Saturday, March 9, 2013

Rais Kikwete atuma Salamu za Pongezi kwa Rais Mteule wa Kenya


Rais Mteule wa Kenya, Mhe. Uhuru Kenyatta (kulia) akiwa pamoja na Mhe. William Ruto wakishangilia ushindi.



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais Kikwete amtumia salamu za pongezi Rais Mteule wa Kenya, Mheshimiwa Uhuru Kenyatta
        

       Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia salamu za pongezi nyingi Rais Mteule wa Jamhuri ya Kenya, Mheshimiwa Uhuru Kenyatta.

Katika salamu hizo zilizotumwa leo, Jumamosi, Machi 9, 2013, saa chache baada ya kuthibitishwa rasmi kuwa Mheshimiwa Kenyatta ameshinda Uchaguzi Mkuu wa Kenya uliofanyika mwanzoni mwa wiki hii Jumatatu, Machi 4, 2013, Rais Kikwete amemwambia Mheshimiwa Uhuru Kenyatta:

“Mpendwa Rais Mteule na Kaka, ilikuwa ni furaha kubwa kwangu kupokea taarifa ya ushindi wako wa kuchaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Kenya. Niruhusu, kwa niaba ya Serikali na Wananchi wa Tanzania, na kwa hakika, kwa niaba yangu binafsi kukupogenza kwa dhati ya moyo wangu kwa mafanikio haya makubwa ya kuchaguliwa kwako.”

Ameongeza Rais Kikwete: “ Ushindi huu ni ushahidi na ishara ya wazi kabisa ya imani na matumaini ambayo wananchi wa Kenya waliyonayo katika uongozi wako. Huu ni utambuzi wa kazi yako maridadi na mchango wako mkubwa ambao umeutoa katika nafasi mbali mbali za uongozi katika siku za nyuma katika jitihada zako za kuleta maendeleo ya kiuchumi na kijamii na ustawi wa nchi yako na wananchi wake.”

Amesisitiza Rais Kikwete: “Wakati unajiandaa kuchukua madaraka ya juu zaidi katika nchi yako, napenda kukuhakikishia msimamo wangu binafsi pamoja na ule wa Serikali yangu wa  kuunga mkono Serikali yako. Ni imani yangu kubwa kwamba pamoja tutaweza kuendelea kusukuma mbele zaidi maendeleo ya nchi zetu – Kenya na Tanzania na pia utengamano wa Afrika Mashariki kwa manufaa ya nchi zetu na wananchi wake.”


Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,

IKULU

DAR ES SALAAM

9 Machi, 2013




Waziri Mkuu wa Denmark amaliza ziara yake hapa nchini

Waziri Mkuu wa Denmark, Mhe. Helle Thorning-Schmidt akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika Hospitali ya Wilaya ya Mbulu, Mkoani Manyara alipotembelea Hospitalini hapo kujionea shughuli mbalimbali.

Mhe. Thorning-Schmidt akipata maelezo kutoka kwa mmoja wa Madaktari katika Hospitali ya Wilaya ya Mbulu alipotembelea Wadi ya Watoto hospitalini hapo. Mwingine katika picha ni Mhe. Mary Nagu (Mb.), Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji na Uwezeshaji ambaye amefuatana na Mhe. Helle katika ziara yake mkoani humo.

Mhe. Thorning-Schmidt akizungumza na mmoja wa kina mama waliolazwa hospitalini hapo kuhusu maendeleo ya afya ya mtoto wake.

Mhe. Thorning-Schmidt akiwa amembeba mtoto mmoja alipotemebelea Wadi ya Watoto katika Hospitali ya Wilaya ya Mbulu

Mhe. Thorning-Schmidt akisikiliza maelezo kuhusu Chuo cha Mafunzo ya Afya kilichopo katika Hospitali ya Wialaya ya Mbulu. Wengine katika picha ni Mhe. Waziri Nagu na Mhe. Eraston Mbwilo, Mkuu wa Mkoa wa Manyara.

Mhe. Thorning-Schmidt akizungumza na wanafunzi wa Chuo cha Mafunzo ya Afya kilichopo katika Hospitali ya Wilaya ya Mbulu.

Wanafunzi wa Chuo hicho wakimsikiliza Mhe. Thorning-Schmidt (hayupo pichani) alipozungumza nao.

Mhe. Thorning-Schmidt akizungumza na wafanyakazi wa Hospitali ya Wilaya ya Mbulu.

Baadhi ya Wafanyakazi wa Hospitali ya Wilaya ya Mbulu wakimsikiliza Mhe. Thorning-Schmidt alipozungumza nao

Mhe. Thorning-Schmidt akisalimiana na Dkt. Richard Sezibera, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) mara baadaya kuwasili Makao Makuu ya Jumuiya hiyo jijini Arusha.

Picha ya Pamoja kati ya Mhe. Thorning-Schmidt, Mhe. Waziri Nagu, Wafanyakazi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na baadhi ya wajumbe aliofuatana nao katika ziara yake.

Mhe. Thorning-Schmidt akipokea maelezo kutoka kwa Mkuu wa Kituo cha Mafunzo cha TCDC kilichopo Usa River mkoani Arusha. Kituo hicho kinafadhiliwa na Denmark na kilianzishwa miaka 40 iliyopita.

Mhe. Thorning-Schmidt akiagana na Mhe. Waziri Nagu mara baada ya kuhitimisha ziara yake mkoani Arusha.

Mhe. Thorning-Schmidt akiagana na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Magesa Mulongo mara baada ya kuhitimisha ziara yake mkoani humo.

Mhe. Thorning-Schmidt akiagana na viongozi mbalimbali waliofika kumsindikiza.

Mhe. Thorning-Schmidt akiagana na Balozi wa Denmark hapa nchini Mhe. Johnny Flento mara baada ya kuhitimisha ziara yake.

Mhe. Thorning-Schmidt akielekea kupanda ndege tayari kwa kuondoka nchini.

Friday, March 8, 2013

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI



UTEUZI WA BODI YA KITUO CHA MIKUTANO CHA KIMATAIFA ARUSHA (AICC)


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete amemteua kwa kipindi kingine Balozi Christopher Liundi kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Kituo cha Mikutano cha Kimataifa-Arusha (AICC).

Aidha, kufuatia uteuzi huo, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard Kamillius Membe (Mb.) amewateua Wajumbe wa Bodi hiyo kama ifuatavyo:-


1.    Bw. Aggrey Mlimuka

2.    Bw. Dash-Hood Mndeme

3.   Dkt. Ali Mndali

4.   Mhe. Balozi Abdi Mshangama (Mstaafu)

5.   Mhe. Faith Mtambo (Mbunge wa Viti Maalum)

6.   Mhe. Dkt. Hamis Kigwangala (Mbunge wa Nzega)

7.  Mhe. Mary Chatanda (Mbunge wa Viti Maalum)

8.  Mhe. Ali Mzee Ali, (Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi - Zanzibar)

9.   Bw. Wilson Masilingi (Mbunge Mstaafu)


Uteuzi wa Mwenyekiti na Wajumbe hao ni kwa kipindi cha miaka mitatu (3) kuanzia tarehe 06 Machi, 2013.


   
IMETOLEWA NA: WIZARA YA MAMBO YA NJE

NA

USHIRIKIANO WA KIMATAIFA, DAR ES SALAAM


8 MACHI, 2013