Monday, October 28, 2013

MLINZI WA AMANI MTANZANIA APOTEZA MAISHA DRC


Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon ametuma salam za rambirambi kwa Familia na kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kufuatia kifo cha Mlinzi wa Amani Mtanzania ambaye amepoteza maisha siku ya jumapili baada ya kushambuliwa na kundi la waasi la M23 katika eneo la Kiwanja- Rushuru kilimita 25 magharibi ya mji wa Goma. katika shambulio hilo, Mlinzi mwingine ambaye pia ni Mtanzania amejeruhiwa. kumekuwapo na mapigano kati ya Majeshi ya Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (FARDC) na Kundi la M23.

Luteni Rajabu Ahmad Mlima Enzi ya Uhai Wake


Na Mwandishi Maalum

Kwa   mara nyingine  Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban  Ki Moon, amelaani vikali  tukio la kuuawa kwa mwanajeshi  wa kitanzania  aliyekuwa akihudumu katika Misheni ya  Umoja wa Mataifa ya  Kutuliza Amani katika Jamhuri ya  Kidemokrasia ya Kongo (MONUSCO).

Kifo cha mwanajeshi huyo mtanzania   kimetokea jana jumapili baada ya kushambuliwa na kundi la M23 ambalo linapigana na majeshi ya Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya KONGO ( FARDC).

Katika salamu zake  rambirambi kwa  familia ya  marehemu  na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Mkuu   huyo wa Umoja wa Mataifa, ameelaani vikali mauaji hayo na kuahidi kwamba  Umoja wa Mataifa utaendelea kutekeleza  majukumu yake ikiwa  ni pamoja na kuchukua  hatua   zote muhimu kuwalinda raia wa DRC.

“Ninalaani vikali mauaji ya  mlinda amani kutoka Tanzania ambaye alishambuliwa  na kundi la M23 katika eneo la    Mashariki ya  DRC, ninatoa  salamu zangu za  rambirambi kwa familia ya marehemu,  na  kwa Serikali ya  Jamhuri ya Muungano wa  Tanzania ” ananukuliwa Katibu Mkuu akisema.

Kwa mujibu wa taarifa zilizoufikia Uwakilishi wa Kudumu wa Tanzania  katika  Umoja wa Mataifa,   siku  ya jumapili , zinaeleza kwamba Mlinzi huyo wa  amani aliyepoteza maisha  na ambaye jina lake linahifadhiwa kwa sasa   anacheo cha  Luteni na kwamba alishambuliwa wakati  kikosi chake kikiwa katika harakati za kutoa ulinzi wa  raia katika eneo la Kiwanja- Rutushura  kilomita 25 kutoka  Magharibi mwa  mji wa Goma.

Katika mashambuli hayo mlinzi mwingine wa amani ambaye pia ni mtanzania amejeruhiwa.

 Aidha  taarifa iliyotolewa na msemaji wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,  inaeleza kwamba Umoja wa Mataifa utachukua  hatua zote muhimu kwa mujibu wa Azimio namba 2098 ( 2013 )  kutimiza wajibu wake .

Ni kupitia Azimio hilo ambalo lilipitishwa mwezi Marchi  mwaka huu,  Baraza  Kuu la Usalama liliridhia kuanzishwa kwa Brigedi Maalum ( FIB) ambayo pamoja na mambo mengine imepewa  jukumu la kutumia nguvu pale inapobidi ikiwa  ni pamoja na kuwapokonya silaha makundi ya wanagambo wenye silaha likiwamo kundi  hilo la M23 na makundi mengine ambayo yamekuwa yakiendesha mapigano na machafuko katika DRC.

Mapigano yanayoendelea hivi sasa kati ya majeshi  ya serikali ya Kongo na kundi la M23 yamefuatia kuvunjia hivi  karibuni  kwa mazungumzo ya  Kampla  yaliyokuwa yakiendelea  kati ya pande  mbili. Hali inayolifanya eneo hilo la Mashariki ya Kongo kuzidi  kuwa tete.




New Ambassador of Tanzania to Nigeria gets sworn-in



The newly appointed Ambassador of the United Republic of Tanzania to the Federal Republic of Nigeria, H.E. Daniel O. Njolaay (right), in a discussion with other appointees today at the State House, in Dar es Salaam.  From left is Ms. Tamika I. Mwakahesya, Secretary to the Public Service Renumeration and Productivity Board, Mr. Raphael Leyani Daluti (2nd left), Deputy Permanent Secretary of the Ministry for Agriculture, Food Security and Cooperation, and Dr. Bashir Mrindoko, Permanent Secretary of the Ministry of Water.

Dr. Mohammed Gharib Bilal, Vice President of the United Republic of Tanzania in a discussion with Hon. Stephen M. Wassira (MP), Minister of State - President's Office Civil Society Relations and Coordination.

Also in attendance were Mr. John M. Haule, Permanent Secretary of the Ministry of Foreign Affairs and International Co-operation together with Ambassador Dora Msechu (center), Director of the Department of Europe and Americas and Mr. Bilauri, Foreign Service Officer in the Ministry of Foreign Affairs and International Co-operation.

Mr. Lumbila Fyataga, Deputy Private Assistant to the President congratulates newly appointed Ambassador Daniel O. Njolaay. 

Family and Friends during the ceremony.

Ambassador Daniel O. Njolaay of the United Republic of Tanzania to the Federal Republic of Nigeria swears-in before H.E. President Jakaya Mrisho Kikwete. 

Dr. Bashir Mrindoko, new Permanent Secretary of the Ministry of Water witnesses President Kikwete as he attest his sworn-in Statement during the ceremony. 

Ms. Tamika I. Mwakahesya, Secretary to the Public Service Renumeration and Productivity Board swears-in before President Kikwete. 

Group photo of President Kikwete and Vice President Dr. Bilal together with the newly sworn-in Permanent Secretary of the Ministry of Water Mr. Mrindoko (2nd right), Deputy Permanent Secretary of the Ministry of Agriculture, Food Security and Cooperation Mr. Daluti (right), Tanzania Ambassador to Nigeria H.E. Njolaay (right) and Secretary to the Public Service Renumeration and Productivity Board Ms. Mwakahesya (2nd right).

President Kikwete in a photo with Ambassador Daniel O. Njolaay, newly appointed Ambassador of the United Republic of Tanzania to the Federal Republic of Nigeria. 

President Kikwete holds a beautiful baby belongs to the family of Mr. Bashir Mrindoko (left), newly sworn-in Permanent Secretary of the Ministry of Water.

H.E. President Jakaya Mrisho Kikwete in a discussion with his Vice President Dr. Mohammed Gharib Bilal. 

President Kikwete in a candid conversation with Vice President Dr. Bilal and Ambassador Njolaay.

Permanent Secretary Mr. Haule of Ministry of Foreign Affairs shares a laughter with Dr. L. Ndumbaro,   Personal Assistant to the President (Political Affairs) and Ambassador Dora Msechu, Director of the Department of Europe and Americas in the Ministry of Foreign Affairs. 

Permanent Secretary Mr. John M. Haule of the Ministry of Foreign Affairs and International Co-operation in a group photo with Ambassador Daniel O. Njolaay, newly sworn-in Ambassador of the United Republic of Tanzania to the Federal Republic of Nigeria and his family. 

Permanent Secretary Mr. Haule of the Ministry of Foreign Affairs in a conversation with Ambassador Njolaay. 

Ambassador Dora Msechu, Director of the Department of Europe and Americas in a photo with Ms. Tamika I. Mwakahesya, Secretary to the Public Service Renumeration and Productivity Board.



All photos by Tagie Daisy Mwakawago 



Saturday, October 26, 2013

Maadhimisho ya Siku ya Umoja wa Mataifa yafana

Mkurugenzi na Mkuu wa Itifaki, Balozi Mohammed Maharage Juma akimkaribisha Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi Khamis Kagasheki mara baada ya kuwasili kwenye Viwanja vya Karimjee, Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kushiriki katika Maadhimisho ya Miaka 68 ya Umoja wa Mataifa. Maadhimisho hayo hufanyika tarehe 24 Oktoba ya kila mwaka. Mhe. Kagasheki alimwakilisha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) kwenye maadhimisho hayo.

Mhe. Kagasheki akisalimiana na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa hapa nchini, Dkt. Alberic Kacou mara baada ya kuwasili.

Mhe. Kagasheki akilakiwa na Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy mara baada ya kuwasili kwenye Viwanja vya Karimjee kwa ajili ya maadhimisho ya miaka 68 ya Umoja wa Mataifa.

Mhe. Kagasheki akifuatana na Mkuu wa Itifaki, Balozi Maharage, Dkt. Kacou na Balozi Mushy kuelekea kwenye Jukwaa Kuu. (picha na Zainul Mzige wa dewjiblog.com)
Mhe. Kagasheki akisalimiana na Wakuu wa Mashirika mbalimbali ya Umoja wa Mataifa yaliyopo hapa nchini mara baada ya kuwasili.
Mhe. Kagasheki akisikiliza Wimbo wa Taifa ukipigwa kuashiria ufunguzi wa maadhimisho hayo.
Gwaride la Heshima
Mhe. Kagasheki akikagua Gwaride la Heshima kwa ajili ya kuadhimisha miaka 68 ya Umoja wa Mataifa (picha hii na Bw. Zainul Mzige wa dewjiblog.com)
Mshereheshaji (MC) wa siku hiyo Bw. Macocha Tembele, Afisa Mambo ya Nje akiwa kazini
Viongozi wa Dini waliokuwepo uwanjani hapo.
Mabalozi na Wageni waalikwa mbalimbali pia walikuwepo.
Mabalozi
Kiongozi wa Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini ambaye pia ni Balozi wa DRC, Mhe. Juma Khalfan Mpango na Mwakilishi wa Mkuu wa Majeshi wakifuatilia kwa makini maadhimisho ya Umoja wa Mataifa.
Wageni waalikwa
Dua kuiombea amani dunia ikisomwa
Maombi yakitolewa
Sala ikitolewa 
Burudani kutoka Brass Band ya Jitegemee ikitolewa


Dkt. Kacou akisoma ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuadhimisha siku hiyo.


Wageni waalikwa wakimsiliza Dkt. Kacou (hayupo pichani)

Mhe. Kagasheki akihutubia

Dkt. Kacou na Balozi Mushy wakimsikiliza Mhe. Kagasheki (hayupo pichani)
Maafisa Mambo ya Nje wakimsikiliza Mgeni Rasmi (hayupo pichani). Kushoto ni Bw. Lucas Mayenga, Bw. Amos Tengu na Bw. Tembele.

Maafisa wengine wakifuatilia maadhimisho hayo kwa furaha. Kutoka kulia ni Bi. Asha Mkuja, Bi. Ramla Khamis na Bi. Jubilata Shao.

Meza Kuu.

Mhe. Kagasheki akikata utepe kuashiria ufunguzi wa Maonesho yaliyoandaliwa mahsusi kwa ajili ya kuadhimisha miaka 68 ya Umoja wa Mataifa

Mhe. Kagasheki akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili katika Banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Taasisi zake.

Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Bw. Mkumbwa Ally akitoa maelezo kuhusu majukumu ya Wizara kwa Mhe. Kagasheki alipotembelea Banda la Wizara.

Mmoja wa Maafisa kutoka Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC), Bw. Rodney Thadeus akitoa maelezo kwa Mhe. Kagasheki kuhusu utendaji wa kituo hicho.

Mkufunzi Mwandamizi kutoka Chuo cha Diplomasia, Bw. Ali Masabo nae akimweleza Mgeni Rasmi, Mhe. Kagasheki majukumu ya chuo hicho

Bi. Praxida kutoka Taasisi ya APRM akimhudumia Balozi wa Msumbiji hapa nchini alipotembelea Banda la Wizara.

Mhe. Kagasheki akipata maelezo kutoka kwa Afisa wa Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa, Bi. Usia Nkoma alipotemebelea mabanda mbalimbali Viwanjani hapo.

Dkt. Kacou akifurahia jambo na Balozi Mpango pamoja na Mkuu wa Itifaki, Balozi Maharage.

Balozi Mushy akisisitiza jambo kwa Dkt. Kacou.