Tuesday, October 13, 2015

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI





Taarifa zaidi kuhusu Mahujaji kutoka Tanzania waliofariki na kujeruhiwa huko Saudi Arabia



Mahujaji wengine wanane kutoka Tanzania ambao walikuwa hawaonekani tokea ajali ya kukanyagana kwa mahujaji ilipotokea Makkah nchini Saudi Arabia tarehe 24 Septemba 2015 wametambuliwa kuwa, ni miongoni mwa mahujaji waliofariki  dunia. Kutambuliwa kwa mahujaji hao kunafanya idadi ya mahujaji wa Tanzania walipoteza maisha katika ajali hiyo kufikia ishirini (20). Majina kamili ya mahujaji hao na vikundi vilivyowasafirisha kwenda Makkah katika mabano ni Hamida Llyas Ibrahim (Khidmat Islamiya), Farida Khamis Mahinda (Ahlu Daawa), Archelaus Anatory Rutayulungwa (Khidmat Islamiya) na Said Abdulhabib Ferej (Ahlu Daawa).


Wengine ni Awadh Saleh Magram (Khidmat Islamiya), Salama Rajab Mwamba (Khidmat Islamiya), Nuru Omar Karama (Ahlu Daawa) na Saida Awaadh Ali (Ahlu Daawa).

Serikali ya Saudi Arabia inaendelea kutoa taarifa zaidi za  mahujaji waliofariki dunia au kujeruhiwa katika ajali hiyo na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa itaendelea kutoa taarifa kwa umma kuhusu wahanga wa ajali hiyo kadri itakapokuwa inazipokea.



Imetolewa na:

Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,

Dar es Salaam

13 Oktoba, 2015

Waziri Membe aongoza Siku ya Kilele cha Umoja wa Mataifa.

Mgeni Rasmi wa siku ya kilele cha maadhimisho ya miaka 70 ya Umoja wa Mataifa,Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard Kamillius Membe (Mb.), akitoa hotuba baada ya kupandishwa kwa Bendera ya Umoja wa Mataifa, maadhimisho ambayo hufanyika kila mwaka tarehe 24-10-2015.
Mgeni Rasmi Mhe Bernard Membe, akisikiliza wimbo wa Taifa kabla ya kukagua gwaride la heshima lililoandaliwa kwaajili ya maadhimisho hayo.
Mgeni Rasmi wa siku ya kilele cha maadhimisho ya miaka 70 ya Umoja wa Mataifa,Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard Kamilius Membe,akikagua gwaride la heshima kabla ya kupandishwa kwa bendera ya Umoja wa Mataifa.
Askari akipandisha bendera ya Umoja wa Mataifa katika maadhimisho hayo yaliyofanyika leo tarehe 13-10-2015 katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam. Maadhimisho ya mwaka huu yamefanyika siky 11 kabla ya tarehe halisi kwa sababu ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 utakaofanyika tarehe 25 Oktoba 2015.
Askari wakiwa wamesimama wima huku wakishuhudia Bendera ya Umoja wa Mataifa ikipandishwa.
Bendera ya Umoja wa Mataifa ikiwa tayari imepandishwa na kupepea pamoja na Bendera ya Tanzania.
 Rais Mstaafu wa awamu ya Tatu, Mhe. Benjamin William Mkapa akiwasili katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam,tayari kwa kuhudhuria siku ya kilele cha Umoja wa Mataifa.

Rais Mkapa akisalimiana na baadhi ya maofisa wa Umoja wa Mataifa mara tu baada ya kuwasili viwanjani hapo.
Mgeni Rasmi wa siku ya kilele cha maadhimisho ya miaka 70 ya Umoja wa Mataifa,Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard Kamilius Membe (Mb), akiwasili katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam,tayari kwa kuongoza kilele cha sherehe za kuzaliwa kwa Umoja wa Mataifa.

Mhe. Bernard Membe akisalimiana na baadhi ya maofisa wa Umoja wa Mataifa mara tu baada ya kuwasili viwanjani hapo.
 Mhe. Membe akisalimiana na Rais Mstaafu Mhe. Benjamin Mkapa, mara alipowasili meza kuu.

Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa, Bw. Alvaro Rodriguez, akimkaribisha  Mgeni rasmi, Mhe. Bernard Membe.
 Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, akitangaza utaratibu wa sherehe fupi za maadhimisho hayo.


Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhadi Mussa Salim, akiomba dua kabla ya shughuli rasmi kuanza. 
Mwakilishi wa madhehebu ya KKKT, akifanya maombi kabla ya kuanza rasmi kwa shughuli za kilele hicho cha miaka 70 ya Umoja wa Mataifa.

Mgeni Rasmi wa siku ya kilele cha maadhimisho ya miaka 70 ya Umoja wa Mataifa,Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard Kamilius Membe (Mb), akitoa hotuba kwenye maadhimisho ambayo hufanyika kila mwaka tarehe 24-10-2015.

Rais Mstaafu wa awamu ya Tatu, Mhe. Benjamin William Mkapa akitoa hotuba katika siku ya kilele cha maadhimisho ya kuzaliwa kwa Umoja wa Mataifa.Maadhimisho hayo yamelazimika kufanyika leo tarehe 13-10-2015 ili kupisha Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika tarehe 25-10-2015.
 Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa, Bw. Alvaro Rodriguez,akitoa hotuba yake kwenye maadhimisho ambayo hufanyika kila mwaka tarehe 24-10-2015.

Wanafunzi wa shule maalumu ya watoto wenye ulemavu wa kusikia, wakicheza wimbo maalumu kama ujumbe wao kwa Umoja wa Mataifa.
 Wanafunzi wa shule ya Sekondari Jitegemee pamoja na shule nyingine za hapa mjini Dar es salaam nao wakiimba wimbo maalumu wa kuelezea malengo mapya ya maendeleo endelevu yaliyozinduliwa Septemba 2015 mwaka huu Jijini New York Marekani.
 Wanafunzi hao wa shule ya Sekondari Jitegemee, wakitoa heshima kwa Mgeni rasmi pamoja na jukwaa kuu kwaujumla baada ya kumaliza kuwasilisha ujumbe wao kwa Umoja wa Mataifa.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, akiendelea kuongoza sherehe hizo
 Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa, Bw. Alvaro Rodriguez, akimkabidhi zawadi Mgeni Rasmi wa siku ya kilele cha maadhimisho ya miaka 70 ya Umoja wa Mataifa,Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard Kamilius Membe, kwa kutambua mchango na ushirikiano wake uliotukuka kwa kipindi chote alichofanya kazi kama Waziri  wa Mambo ya Nje.
 Mhe. Membe akimshukuru Bw. Alvaro kwa zawadi hiyo.
 Waziri Membe alitumia siku ya kilele hicho kuwashukuru Mabalozi wote  kwa ushirikiano wao waliompatia kwa kipindi chote alichofanya nao kazi na kuwaaga rasmi kama Waziri wa Mambo ya Nje.
Mgeni rasmi akiwa katika picha ya pamoja na Meza kuu pamoja na Viongozi wa dini, mara baada ya kumalizika kwa maadhimisho ya siku hiyo ya Kilele cha Umoja wa Mataifa. 

Mgeni rasmi akiwa katika picha ya pamoja na Meza kuu pamoja na Wakuu wa Mashirika mbalimbali ya Umoja wa Mataifa yaliyopo hapa nchini, mara baada ya kumalizika kwa maadhimisho ya siku hiyo ya Kilele cha Umoja wa Mataifa. 

Mgeni rasmi akiwa katika picha ya pamoja na Meza kuu pamoja na Waheshimiwa Mabalozi mbalimbali wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini, mara baada ya kumalizika kwa maadhimisho ya siku hiyo ya kuzaliwa  Umoja wa Mataifa. 

Mgeni rasmi akiwa katika picha ya pamoja na Meza kuu pamoja na Maofisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, mara baada ya kumalizika kwa maadhimisho hayo. 
Mgeni rasmi akiwa katika picha ya pamoja na Meza kuu pamoja na Maofisa wa Umoja wa Mataifa, mara baada ya kumalizika kwa maadhimisho ya siku ya Umoja wa Mataifa.
 Mgeni rasmi akiwa katika picha ya pamoja na Meza kuu pamoja na Wanafunzi, mara baada ya kumalizika kwa maadhimisho hayo. 
========================
PICHA NA REUBEN MCHOME. 
========================

STATEMENT BY HONOURABLE BERNARD K. MEMBE (MP) MINISTER FOR FOREIGN AFFAIRS AND INTERNATIONAL COOPERATION

Guest of Honor and Minister for Foreign Affairs and International Cooperation Hon. Bernard K. Membe delivering his statement of the day.
STATEMENT BY HONOURABLE BERNARD K. MEMBE (MP)
MINISTER FOR FOREIGN AFFAIRS AND INTERNATIONAL COOPERATION DURING THE FLAG RAISING CEREMONY IN COMMEMORATION OF 70TH ANNIVERSARY OF THE UNITED NATIONS, MNAZI MMOJA GROUNDS, 
13TH OCTOBER 2015

Your Excellency, Benjamin William Mkapa, Former President of the United Republic of Tanzania;

Your Excellency Juma Alfani Mpango, Ambassador of the DRC and Dean of the Diplomatic Corps;

Mr. Alvaro Rodriguez, UN Resident Coordinator and UNDP Resident Representative in Tanzania;

Ambassador Filberto Sebrigondi, Head of the European Delegation to Tanzania;

Excellencies Ambassadors, High Commissioners and Other Members of the Diplomatic Corp; 

Heads of the UN Specialized Agencies, Funds and Programmes;

Permanent Secretaries and other Government Officials;

Religious Leaders;

Members of the Press;

Distinguished Guests;

Ladies and Gentlemen.

Good Morning!!

I am greatly honoured to welcome you all to this auspicious occasion as we celebrate the 70th Anniversary of the United Nations. This occasion gives us yet another opportunity to reflect on the organisation’s achievements and also revisit the areas we need to put more efforts thus to meet the prevailing global challenges. 

On 24th October every year, the world commemorates the inception of this noble universal body. 

This year however, the climax of our celebrations in Tanzania has come a little earlier as we pave way for the general elections which will be held on 25th October.

Distinguished guests,
Ladies and Gentlemen,

You may recall on 25th September 2015, the Heads of State and Government adopted a new global agenda titled “Transforming Our World: The 2030 Agenda for Sustainable Development. This agenda coincidentally correlates with the Secretary General’s global theme for UN Day this year, Strong UN: Better World. To give it a deeper emphasis, we in Tanzania have derived our theme as “One World, Seven Billion People, Protecting Environment is our Responsibility”.

These themes put together reflect People, Planet, Prosperity, Peace and Partnership, commonly known as 5Ps, which summarises the seventeen (17) Sustainable Development Goals in the preamble of the 2030 Agenda for Sustainable Development.

Excellencies, 
Ladies and Gentlemen;
Prior to this occasion, there were series of other events which were part of the celebrations of the UN at 70. These events which reaffirmed our national theme included: planting trees on the slopes of Mount Kilimanjaro; visiting UNDP financed biogas project in Kilema Seminary Secondary School in Moshi; and building toilets at Kiboroloni Primary School, one of ten beneficiary primary schools in Kilimanjaro region. Other activities conducted were cleaning the Temeke Sterio Market to indicate the importance of urban sanitation; and just yesterday, we had a very vibrant and insightful two hours Symposium with the Youth under the theme “UN at 70, Addressing Global Challenges”. Today’s flag raising ceremony is therefore the culmination of all these activities. 

On behalf of my Ministry and the UN in Tanzania, I would like to thank you, your Excellency Former President for your continued dedication on matters that aim to develop not only Tanzania, but world at large. I am confident that the youth and every other participant to the symposium benefitted from your wisdom and candid reflections.  

Your Excellency Former President,

The public may wish to note, you were among the Members of the Secretary General’s High-level Panel on UN System-wide 
Coherence, which among other things, recommended the establishment of the Delivering as One (DaO) Initiative. 

Tanzania took a bold step to be a pilot country under this Initiative, which eventually resulted in the establishment of the United Nations Development Assistance Plan (UNDAP), an important tripartite working plan between Government, UN Organisations and other Development Partners. I am glad to inform you and everyone present here, we have successfully accomplished three out of four pillars of DaO. We now have One Leader who is the Resident Coordinator (RC), One Budget running at the same circle as that of Government, and One Programme as UNDAP. Moving forward, we are to implement the fourth and last pillar, One Office. So far, the Government has secured one acre of land in Masaki area. We have formed a team of experts to advise on different options of financing and expediting the implementation of the project. 

Guest Speaker;
Excellencies;
Ladies and Gentlemen;
As we celebrate the 70th Anniversary of the United Nations, we are reminded that this noble Organisation was created out of ashes of two world wars. Its primary responsibility was to maintain peace and security by preventing the occurrence of another war of the same scale. We can undoubtedly say that at its 70 years of existence, the UN has succeeded in preventing major conflicts and in building peace. 

However, peace and security situation around the world remain fragile and most pressing challenge to the UN. The world continues to witness the rise, widespread and unending intra-state and inter-state wars and conflicts, and at the same time, experience the deadly scourges of terrorism and violent extremism. With these going on, the world is certainly not at absolute peace. 

We all know too well what is going on in Syria, Iraq, Somalia, Libya, Afghanistan, Yemen, Central African Republic to mention a few. Recurring conflicts and wars, and increasing terrorism and extremism, have caused too many deaths, human sufferings, and too much untold sorrow to mankind. This is unacceptable.

Excellencies,
Ladies and Gentlemen;

According to the United Nations High Commission for Refugees, the number of refugees and internally displaced people has reached its highest point since World War II. In 2005, globally, it was estimated that refugees, asylum seekers and Internally Displaced Persons (IDPs) were 38 million. In 2015, just a period of 10 years, the number has gone up by 22 million, reaching 60 million, the highest ever. This means that, one in every 122 persons is now either a refugee, internally displaced, or seeking asylum. Regrettably, this number continues to increase unabatedly. 

Excellencies,
Ladies and Gentlemen;

As of this month, Tanzania continues to host more than 169, 874 refugees. Sadly, this number has increased, just after Tanzania granted naturalization and issued citizenship certificates to more than 162,000 refugees in October 2014. By September this year, we have received more than 90,000 new refugees. This indeed is a setback to our efforts to ensure people remain in their countries of domicile and participate in development activities.

Excellencies,
Distinguished Guests,
Ladies and Gentlemen;

As it was discussed during the symposium yesterday, most of the Organs of the UN have remained with the same status quo for the past 70 years ago. So far, there have not been tangible reforms of the General Assembly (GA), Economic and Social Council (ECOSOC) and the Security Council. For the UN to remain inclusive and credible, these reforms must be discussed openly and adhered to. The General Assembly and Economic and Social Council have continued to adopt countless resolutions and decisions that are not fully implemented. These key Organs on economic and social development cannot enforce implementation of their decisions by the UN Member States. This is not the UN we want at 70. 

Ladies and Gentlemen, 
You will agree with me that, it is high time the demands of the majority of the membership of the United Nations are heard and heeded too.  The Security Council must be reformed now to reflect the realities and needs of the contemporary world. Despite the fact that Africa is the region with the largest membership in the UN; and most peacekeeping operations are happening in Africa, ironically, the continent has no permanent seat in the Security Council. Africa therefore deserves better and fair representation and treatment in the Security Council. We cannot afford to have decisions committed by the Security Council on African affairs without permanent representation of the African countries 

Excellencies, 
Ladies and Gentlemen;
I am pleased to note that, the SDGs have taken on board the unfinished business of the MDGs. One can actually call the SDGs - MDGs-Plus. SDGs 1 to 6 are a continuation of MDGs 1 to 6; SDGs 11 to 15 are expanded form of MDG 7; and SDG 17 which addresses the means of implementation and Global Partnership IS MDG 8. 

Apart from those generic goals of MDGs, there are also new SDGs which aim at accelerating economic growth and sustainable development, particularly in developing countries. The new goals are on agriculture; energy sustainability; economic growth; infrastructure development and sustainable industrialisation; reduce inequality within and among nations; 
and good governance.  These SDGs are critical in transforming our economies to middle income. It is my hope that, this time we will walk the talk!

Excellencies;
Ladies and Gentlemen;
It is at this juncture, I wish to acknowledge commendable job done so far by Mr. Alvaro Radriguez, since he joined us 13 
months ago as the new UN Resident Coordinator. Your bottom-up approach, from rural to the urban has proven to be a workable strategy. We therefore hope, you will be fully involved in the implementation of the New Global Agenda in order to bring a transformative change in Tanzania. 
Excellencies, 
Ladies and Gentlemen;
We are 12 days away. Tanzanians will be casting their ballot for the President, Parliamentarians and Councilors. Since independence, we have witnessed transfer of power peacefully from one President to another in four consecutive terms. We are regarded as one of Africa’s most peaceful countries since independence and among the continent’s strong democratic countries.
I appeal to my fellow Tanzanians particularly the leaders of various groups and political parties to hold this legacy close to their hearts.  We should remember that there is no development without peace and tranquillity; Despite our political affiliations and ideological differences, we are still one nation, and one people.  

On behalf of the Government of the United Republic of Tanzania, I wish to convey my sincerely gratitude to the UN particularly UNDP and other Development Partners who through the Democratic Empowerment Project have provided support of USD 22.5 million for the General Elections. This is another instance that UN’s role in promoting democracy and good governance is indisputable.

Excellencies, 
Distinguished Guests, 

Before I invite H.E. Benjamin William Mkapa, Former President to adress to this gathering, allow me to express Ministry’s appreciation to the Heads of Social Security Funds, Azam and IPP Media for their support in ensuring the success of these commemorations. We thank you most sincerely!!
I now have the honour on behalf of His Excellency President Jakaya Mrisho Kikwete, his entire Government and the People of the United Republic of Tanzania to wish the UN all over the world a Happy 70th Birthday. We congratulate the Secretary General, UN staff  serving around the world and all Member States of the UN for the commemoration of the 70th Anniversary of the United Nations. 


Mheshimiwa Rais Mstaafu;
Baada ya maelezo yangu hayo, kwa heshima na taadhima kubwa ninaomba sasa kukukaribisha uzungumze kidogo na hadhara hii. Karibu sana Mheshimiwa!!

REMARKS BY H.E. BENJAMIN WILLIAM MKAPA, FORMER PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA, AT THE UN FLAG RAISING CEREMONY TO MARK THE CLIMAX OF THE UN 70TH ANNIVERSARY CELEBRATIONS

Former President Benjamin Mkapa delivering his remarks

THEME   
THE UN AT 70: HOW PEACEFUL AND SECURE IS
OUR WORLD TODAY?

A birthday is normally an occasion for celebration. This is also the time for the global community (as we do in our personal lives, and nations do in their history) to make a sober reflection on our journey since birth: What have been the experiences and lessons learnt? And the prospects for the future ahead? The same can be said for global institutions such as the United Nations whose 70th birthday we celebrate this month.

When in the aftermath of the Second World War, 51 countries met in San Francisco, to establish the UN. There were only 4 African countries (Liberia, Ethiopia, Egypt and South Africa). The principal objectives for the new global institution they sought to establish were:

·        To maintain international peace and security
·        To develop friendly relations among nations based on respect for the principle of equal rights and the self-determination of peoples, and to take other appropriate measures to strengthen universal peace;
·        To step up international co-operation in solving international problems of an economic, social, cultural, or humanitarian character, and to promote and encourage respect for human rights and respect for the fundamental freedoms for all without distinction as to race, sex, language, or religion; and
·        To be a center for harmonizing the actions of nations in the attainment of these common ends.

Today, 70 years later, with 54 African countries as members of United Nations and its specialized agencies such as the World Bank, IMF, ILO, UNCTAD, WTO etc. we should ask the question: “As Africa and Africans, how peaceful and secure is our world today?”

I do not intend to give a details and comprehensive assessment of the contribution of the organization and its various constituent agencies over these past 70 years, but will highlight in a selective way these dimensions of the narrative that have more or less significantly affected our continent, and its people.

Firstly, there is no doubt that through various Councils and Committees, the United Nations has been an important forum for the liberation of our continent from colonialism and imperialism. Tanzania’s own path to freedom is an example of this experience. Yet I will argue that the removal of imperial domination of our continent in every aspect i.e. economic, social, cultural, etc. was achieved primarily through the unrelenting struggles of our own people as well as vision and tenacity of our fathers, be these through negotiations and/or armed struggles. Some may debate this assertion but this is my view.

With respect to the third original objective, the experiences for most developing nation’s to-date is a mixed one. For us as Africans there is no doubt that a lot has been achieved a recent global efforts to eliminate object poverty as the scorecard for achievements under the Millennium Development Goals (MDG). According to the MDG Report 2015, the number of people living in extreme poverty has reduced from 1.9 billion in 1990 to 836 in 2015 that is a decline of more than half. Again, number of out-of-school children has declined by 43% from 100 million in 2000 to 57 million in 2015 whilst the literacy gap between men and women has narrowed Moreover, global under-five mortality has dropped by more than half between 1990 and 2015. There has been phenomenal progress in technology which really has been the driver of growth and development in the 21st century. As at 20115, about 3.2 billion people are connected to a global internet of content and applications. For example, the plans under the adopted Sustainable Development Goals (SDG) that was declared at the recent UN General Assembly Summit indicate with continued global cooperation in the next 15 years, much will be achieved in the health, education, food security, gender equality and other social sectors.

The agenda ahead clearly also shows that because large inequalities persist, especially in our continent, much remains yet to be done. In my view the role of the specialized agencies of the UN will remain key and pivotal for Africa and Africans. In the area of health, the achievement of the WHO in dealing with pandemic diseases such as Polio, HIV/AIDS, Ebola, etc. have been commendable. Much remains to be done however in strengthening national level delivery system. The international Labour Organization (ILO) has made considerable strides in establishing progressive workers standards. However, weaknesses in national capacities militate against implements action of standards such as the promotion of fair wages, gender equalities in the work place, child labour, elimination of dangerous working conditions etc. These remain major challenges despite some progress.

The FAO has done much in stimulating agricultural revolution in many parts of the developing world. Nonetheless, agriculture remains the Achilles heel for many in Africa. Despite abundant arable land the continent remain challenged in producing adequate food for its rapid expanding population Land tenure systems are a disincentive production units too unfeasible and technology in agriculture remains backwards. Many of these constraints are also considerably aggravated by challenges of climate change and environmental degradation. Finally I believe strongly that if the UN system is to deliver on several of its foundation objectives, many reforms will be necessary in its governance architecture, especially representation within the Security Council of the General Assembly and voting rights in the Bretton Woods Institutions; the IMF and the World Bank Group. The situation at present in these areas makes nonsense of the equality of sovereignty and democracy. The domination of these institutions by very few developed countries based on history is unfair. The dominance of their …………….. Interest and those of their private corporations remains unjustifiable in current evolving economic and political realities. The result often is that their actions and interest promote the greatest threat to peace and security in the world, the first and fundamental objective of the UN.

Much of the political and economic crises in recent decades at the global level can be traced considerably to dominant nation state and corporate interests, for example, as they seek control of natural resources e.g. energy in the Middle East or minerals and other natural resources in Africa. The widespread political instabilities that these interest cause tend to become triggers of massive population relocations as are currently taking place in the Middle East and in Africa. Africa has been the regime of massive population dislocation caused by conflicts started by economic interests in the past five decades, more than three quarter the life span of the UN! We have examples in our neighbourhood – The Great Lakes Region. Tanzania has been a destination for many refugees in Central and Southern Africa regions. I say with pride that even though a relatively poor nation. Tanzania has coped with floods of refugees, integrating millions of them because of compassion, solidarity and visionary leadership. Today as the world watches with horror the plight of thousands of refugees from Sahilian and North Africa as well as the Middle East who are on the move to safety and in search of peace in Europe; the world can learn from Tanzania’s experience. For a long time the world remained relatively silent when it was mainly Black Africans who were on the move some away from civil conflict and others seeking better economic prospects in Europe. Many ended up in watery graves of the Mediterranean Sea. Today we see massive movement from Syria, Iraq, Lebanon and other parts of the Middle East across to Europe in face of expanding global terrorism. Yet dealing with this problem has become stalemated because of the persisting lack of democracy in the UN governance. Similarly despite affirmation and recognition of the State of Palestine and the rights of the Palestinian people, the undemocratic representation, architecture of the UN system has continued to deny them their humanitarian rights and the right to sovereignty. So, ladies and gentlemen, the UN has ev3ery reason to celebrate it 70” birthday. My judgement is that its achievements though commendable in a number of areas present a mixed picture. True and lasting peace and security in the world can only be possible if the global community, all of us together accept some major reform in the governance of its International institutions. It is only then that the key challenges of today and the near future, namely terrorism, extremism, abject poverty and inequalities can be overcome. As we press for climate change in the physical environment let us recognise a principal driver of change will be ………. in equitable political, economic and egalitarian environment. In that spirit let the UN member states wish each other a Happy 70th Birthday.


Thank you for your attention. 

Monday, October 12, 2015

Katibu Mtendaji wa SADC amtembelea Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje.

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula akimkaribisha Katibu Mtendaji wa SADC, Bi. Stergomena Tax, ofisini kwake kwa mazungumzo kuhusu ujio wa timu ya waangalizi wa uchaguzi wa SADC itakayoongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Msumbiji.
 Katibu Mkuu akisisitiza jambo katika mazungumzo hayo.

Katibu Mtendaji wa SADEC, Bi. Stergomena, akisisitiza jambo katika mazungumzo hayo.
Mazungumzo yakiendelea.
 Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda Balozi Innocent Shio (kushoto) na Afisa Mambo ya Nje Bw. Ally Ubwa wakifuatilia mazungumzo hayo.
 Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula akiagana na Katibu Mtendaji wa SADC, Bi. Stergomena Tax, mara baada ya mazungumzo kuhusu ujio wa timu ya waangalizi wa SADEC itakayoongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Msumbiji.
========================
PICHA NA: REUBEN MCHOME.

UNDP Yatoa Msaada kwa Wizara ya Mambo ya Nje.

 Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa, Bw. Alvaro Rodrigues (kushoto) akimkabidhi Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy msaada wa Vifaa vya mawasiliano (Cameras, printers na Computers) kwa ajili ya kitengo cha Mawasiliano ya Serikali cha Wizara ya Mambo ya Nje.

Balozi Celestine Mushy, akizungumza na Bw. Alvaro Rodrigues muda mfupi kabla ya makabidhiano ya vifaa hivyo kufanyika. Balozi Mushy alishukuru msaada huo ambao alisema umekuja wakati mwafaka ambapo Serikali ipo katika mikakati ya kuboresha mawasiliano na wadau wake.

Mazungumzo yakiendelea....
 Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy, akisaini nyaraka ya makabidhiano kama ishara ya kupokea msaada huo.
Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa Bw. Alvaro Rodrigues naye akiweka sahihi kweye nyaraka ya makabidhiano kama ishara ya kukabidhi rasmi msaada huo wa vifaa mbalimbali kwa ajili ya kitengo cha mawasiliano ya serikali cha Wizara ya Mambo ya Nje.
 Balozi Celestine Mushy akiwa ameshikilia moja ya vifaa vya msaada huo huku baadhi ya Maofisa kutoka Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali wakishuhudia.
 Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bi. Mindi Kasiga, akipokea msaada huo kutoka kwa Balozi Mushy.
Balozi Mushy akiwa ameshikilia Video Camera iliyotolewa msaada na UNDP.
=======================
PICHA NA: REUBEN MCHOME.