Tuesday, November 17, 2015

Katibu Mkuu Mambo ya Nje atembelea Makumbusho ya Taifa

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Liberata Mulamula akiweka saini kwenye kitabu cha wageni mara baada ya kutembelea Jumba la Makumbusho la Taifa lililopo jijini Dar es Salaam. Pembeni yake pichani ni Mkurugenzi wa Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni Bw. Achiles Bufure (kushoto) akiwa na mgeni wake. 
Balozi Mulamula (wa tatu kutoka kushoto), akitizama moja ya hati zilizotolewa na  Malkia Elizabeth wakati wa uhuru. Pichani ni Mtaalam wa Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni Dkt. Amandus Kweka (wa kwanza kulia), Bw. Bufure (wa pili kutoka kushoto).
Dkt. Kweka akiendelea kuelezea chimbuko la mwanadamu na Fuvu lililopo kushoto kwenye sanduku lililo nakshiwa na dhahabu ni la Zinjanthropus lililogunduliwa  huko Olduvai Ngorongoro kwenye miaka ya 1959. 
Bw. Bufure akimwonyesha Balozi Mulamula Mti wa Kihistoria haupo pichani.
Balozi Mulamula (wa pili kutoka kushoto), akipata maelezo ya Mchoro wa maisha ya Binadamu wa Kwanza iliyopo mbele yao kutoka kwa Mtaalam wa Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni Bi. Agnes Gidna (wa kwanza kulia).
Bi. Agnes Gidna akiendelea kuelezea michoro ya mapangoni kwa Balozi Mulamula (kushoto)
Balozi Mulamula akieendelea na ziara yake na kujionea mambo mbalimbali yaliyopo katika Jumba la Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni jijini Dar es Salaam
Balozi Mulamula akiwa kwenye moja ya sehemu maalumu kwa ajili ya  simulizi za Hadithi za watoto wadogo. 
Balozi Mulamula (kushoto) wakizungumza na Bw. Bufure mara baada ya kumaliza ziara yake kwenye Jumba la Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni na tayari kwaajili ya kuendelea na majukumu mengine ya kitaifa.

Picha na Reginald Philip.

Friday, November 13, 2015

MAREKEBISHO YA BARAZA KUU LA USALAMA YATAONGEZA TIJA- TANZANIA

Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Ramadhan Mwinyi akizugumza siku ya Alhamis wakati Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa lilipokuwa likijadili Taarifa ya mwaka ya Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa.
Na Mwandishi Maalum, New  York


Tanzania imekaribisha  juhudi zinazochuliwa na  Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa za kuboresha uwazi na utendaji wenye tija wa chombo hicho juhudi ambazo pia  zinahusisha mijadala ya wazi.

Hayo yameelezwa na  Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Ramadhan Mwinyi wakati  Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa,  lilipokuwa likijadili Taarifa ya  Mwaka  ya Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa.

 Taarifa hiyo    iliwasilishwa siku ya  alhamisi na   Mwakilishi wa Kudumu wa Uingereza,  Balozi Matthew Rycroft ambaye nchi yake  ndiye Rais wa  Baraza Kuu la  Usalama kwa  mwezi huu wa  Novemba.

Taaria hiyo ambayo ni  ya  kuanzia  Agosti Mosi 2014 hadi Julai 31 2015 imeanisha mikutano  ya wazi na  ya ndani iliyofanywa na Baraza kwa kipindi hicho, maazimio yaliyopitishwa, taarifa za rais wa Baraza kwa  mwezi, na   ziara za kikazi zilizofanywa   na wajumbe wa Baraza. ambaye ni  Mwakilishi wa Kudumu wa Uingereza Balozi katika Umoja wa Mataifa.

Balozi Mwinyi,  amesema  mijadala  ya wazi inayoandaliwa na  Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa  inatoa fursa na kufungua milango kwa  nchi nyingi zaidi kushiriki nje ya wajumbe  15 wa Baraza  na kwamba Tanzania ni kati ya nchi ambazo zimekuwa ikishiriki mijadala hiyo ya wazi.

 Pamoja na  kupongeza juhudi hizo,  Mwakilishi huyo wa Tanzania, amesema,  ni matumaini ya Tanzania   kuwa  katika  siku za usoni,  Baraza Kuu la litaanda mijadala katika namna ambayo itawezesha wajumbe kuzingatia hoja zilizotolewa na  washiriki wengine kabla ya kupitisha matokoe ya mijadala hiyo.

Vilevile  Balozi Mwinyi amesema, juhudi zinazochukuliwa na  wadau mbalimbali za kudhibiti matumizi ya kura ya turufu hasa katika kuzuia mauaji ya halaiki, ni  juhudi sahihi na zinazopashwa kuugwa mkono.

Akizungumzia zaidi  matumizi ya kura ya turufu, Balozi Ramadhan Mwinyi ametoa wito kwa  mataifa yenye hadhi ya kutumia kura hiyo  kuhakikisha kwamba wanaitumia pale tu inapobidi na kwa kuzingatia matakwa na mamlaka zilizoainishwa  Katiba ya Umoja wa Mataifa.

“ Tuna toa wito wa Baraza kuu la Usalama la Umoja wa mataifa, kuingiza katika taarifa zake za baadaye kwa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa,  tathmini ya   matokeo ya maamuzi  pale kura ya turufu ilipotumika na matokeo ya pale  ambapo kura ya turufu haikutumika katika maamuzi yaliyofikiwa” akasisitiza Balozi  Mwinyi.

Kuhusu  yaliyomo katika taarifa hiyo, Balozi  amesema,  Tanzania inaungana  na  nchi nyingine katika kutaka taarifa hizo  ziwe na uchambuzi wa kina na  zilizo  makini badala ya kuorothesha  kazi za Baraza hilo kama ilivyo sasa.

Tanzania pia   kupitia  Mwakilisihi wake ,  imekaribisha  namna ambavyo Baraza Kuu la Usalama linavyopanua wigo wa majadiliano na  Vyombo  vingine  zikiwamo Asasi  za kijamii na wanazuoni katika  kujadilia masuala mtambuka.

“ Hata hivyo tumegundua  kuwa  baadhi ya mada zinazojadiliwa siyo tu  zimekuwa  zikiwagawa washiriki lakini pia zinakuwa nje ya mamlaka ya Baraza. Tunaomba tukumbushe kwamba  Baraza Kuu la Usalama kama Chombo wakilishi cha  Baraza Kuu la  Umoja wa Mataifa, Baraza linatakiwa kujiepusha  mada ambazo  hazina tija”.

Baadhi ya wazungumzaji wengine waliochangia  taarifa hiyo ya Baraza Kuu la Usalama,  wameelezea kwamba  licha ya  utekelezaji  wa  mamlaka ya Baraza hilo katika kusimamia  Amani na usalama wa kimataifa,  Baraza limeshindwa kabisa kumaliza  baadhi ya migogoro kama  ule wa Syria ambao  umedumu  kwa muda mrefu.

Thursday, November 12, 2015

Head of Delegation of the EU to Tanzania visits Ministry of Foreign Affairs.

Head of Delegation of the EU to Tanzania, Ambassador Filiberto Sebregondi (L) listens careful to the Permanent Secretary at the Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation, Amb. Liberata Mulamula when the two met today at the Ministry's Office to discuss Burundi's post election events.
A section of Ambassadors of the European Union countries to Tanzania who attended the Meeting between H.E Sebregondi and Amb. Mulamula follow carefully the conversation.
Officials from the embassies of European Union countries to Tanzania.
Head of Departments in the Ministry of Foreign Affairs and Internationa Cooperation. From right is Ambassador Joseph Sokoine, Director of  Europe and Americas, Ambassador Innocent Shiyo, Director of Regional Cooperation and Ambassador Samuel Shelukindo, Director of Africa 
Officials from the Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation, From right is Ms. Felista Rugambwa, Mr. Ally Kondo and Mr. Medadi Ngaiza.
Permanent Secretary at the Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation, Amb. Liberata Mulamula shakes hands with the Ambassadors of the European Union Countries to Tanzania after finishing their meeting.

Photos by Reginald Philip

Task Force Coordinator, Registry, ICC Visits Ministry of Foreign Affairs


Task Force Coordinator, Registry, ICC, Ms. Jelena Vukasinovic who is based in Kenya empasizes a point when she met for conversation with the Director of Legal Affairs Unit in the Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation, Amb. Baraka Luvanda. Ms. Vukasinovic informed Amb. Luvanda that International Criminal Court (ICC) will conduct a Second Regional Seminar of Councel and Legal Profession in Arusha early next year.


Amb. Luvanda (R) makes an interruption point  at the going on conversation with the ICC Officials. Left in the photo is Mr. Gerhard Van Rooyen, Head of Protection Sub-Unit  Chef - ICC.


Conversation is in progress.
Photos by Reginald Philp

WANAFUNZI WA ISS WAMTEMBELEA BALOZI MPYA WA TANZANIA, UHOLANZI


 Kutoka kushoto ni Ndg. Shamy Chamicha,  Ndg. Jackosn Bulili, Mhe. Balozi Kasyanju, Ndg. Florence Chakina na Ndg. Hofman Sanga.



Mhe. Irene F. M. Kasyanju, Balozi wa Tanzania, Uholanzi amekutana na wanafunzi wanne (4) kati ya watano (5) wa Kitanzania wanaosoma shahada tofauti katika Taasisi iitwayo “International Institute of Social Studies (ISS)”,ya Chuo Kikuu cha Erasmus, Rotterdam ambao walifika Ubalozini kwa lengo la kumsalimu na kufahamiana.



Pamoja na mambo mengine wanafunzi hao wamewasilisha ombi lao kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia kwa Mhe. Balozi wa kuiomba isaidie kuhakikisha kuwa idadi ya “Scholarships” kwa Tanzania kwenye Chuo hicho inaongezeka.  Hii ni kutokana na idadi ya Watanzania wanojiunga na ISS kupungua sana ukilinganisha na nchi zingine za Afrika hususan za Afrika Mashariki, tofauti na ilivyokuwa zamani.



Balozi kwa upande wake alipokea ombi lao na kuahidi kulifanyia kazi ipasavyo. Aliwashukuru wanafunzi hao kwa kufika Ubalozini kujitambulisha na akawaahidi ushirikiano wakati wote watakaokuwepo Uholanzi.