Thursday, November 12, 2015

WANAFUNZI WA ISS WAMTEMBELEA BALOZI MPYA WA TANZANIA, UHOLANZI


 Kutoka kushoto ni Ndg. Shamy Chamicha,  Ndg. Jackosn Bulili, Mhe. Balozi Kasyanju, Ndg. Florence Chakina na Ndg. Hofman Sanga.



Mhe. Irene F. M. Kasyanju, Balozi wa Tanzania, Uholanzi amekutana na wanafunzi wanne (4) kati ya watano (5) wa Kitanzania wanaosoma shahada tofauti katika Taasisi iitwayo “International Institute of Social Studies (ISS)”,ya Chuo Kikuu cha Erasmus, Rotterdam ambao walifika Ubalozini kwa lengo la kumsalimu na kufahamiana.



Pamoja na mambo mengine wanafunzi hao wamewasilisha ombi lao kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia kwa Mhe. Balozi wa kuiomba isaidie kuhakikisha kuwa idadi ya “Scholarships” kwa Tanzania kwenye Chuo hicho inaongezeka.  Hii ni kutokana na idadi ya Watanzania wanojiunga na ISS kupungua sana ukilinganisha na nchi zingine za Afrika hususan za Afrika Mashariki, tofauti na ilivyokuwa zamani.



Balozi kwa upande wake alipokea ombi lao na kuahidi kulifanyia kazi ipasavyo. Aliwashukuru wanafunzi hao kwa kufika Ubalozini kujitambulisha na akawaahidi ushirikiano wakati wote watakaokuwepo Uholanzi.










Wednesday, November 11, 2015

Wizara ya Mambo ya Nje yamuaga rasmi Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula (kushoto), akimkabidhi picha ya kuchora kama zawadi ya ukumbusho kutoka Tanzania Balozi anayemaliza muda wa uwakilishi wa Umoja wa Ulaya hapa nchini Mhe. Filiberto Sebregondi, katika hafla ya kumuaga iliyofanyika katika Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam tarehe 11 Novemba, 2015
Balozi Sebregondi akifurahia picha hiyo huku Mabalozi na Wageni waalikwa nao wakichukua picha za ukumbusho wa tukio hilo
Balozi Mulamula akitoa neno la shukrani kwa Balozi Sebregond, kwa niaba ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakati wa hafla hiyo
Sehemu ya Wageni waalikwa wakimsikiliza kwa makini wakati Balozi Mulamula (hayupo pichani) alipokuwa akitoa neno la shukrani
Balozi Mulamula akiendelea kuzungumza katika hafla hiyo
Balozi Filiberto Sebregondi naye alipata nafasi ya kutoa shukrani kwa ushirikiano aliokuwa akipata kutoka kwa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Watanzania kwa ujumla wakati wa kutimiza majukumu yake akiwa kama mwakilishi wa Umoja wa Ulaya hapa nchini. 
Balozi Liberata Mulamula (kushoto) kwa pamoja na  Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo hapa nchini Mhe. Juma Mpango (katikati) na Naibu Katibu Mkuu  wa Wizara ya Fedha Dkt. Hamis Mwinyimvua (kulia) kwa pamoja wakimsikiliza Balozi Sebregondi (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza wakati wa hafla ya kumuaga.
Maafisa Mambo ya Nje nao wakisikiliza kwa makini wakati Balozi Sebregondi (hayupo pichani) akizungumza. 
Balozi Mulamula na Balozi Sebregondi wakitakiana afya njema
Wageni waalikwa nao wakitakiana afya njema
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Mindi Kasiga akizungumza katika hafla ya kumuaga Balozi Sebregondi (hayupo pichani). 
Balozi Liberata Mulamula akiwa katika picha ya pamoja na Balozi anayewakilisha Umoja wa Ulaya hapa nchini Mhe. Filiberto Sebregondi
Picha ya pamoja.
 Picha na Reginald Philip.



Tuesday, November 10, 2015

Press Release

H.E. Jose Eduardo dos Santos, President of Angola

PRESS RELEASE

H. E. John Pombe Joseph Magufuli, President of the United republic of Tanzania, has sent a congratulatory message to H. E. Jose Eduardo dos SANTOS, President of the Republic of Angola on the occasion of the 40th Anniversary of Angolan National Day on the 11th November, 2015.

The message reads as follows:

“H.E. Jose Eduardo Dos Santos,
President of the Republic of Angola,
LUANDA.

Your Excellency and Dear Brother,

It gives me great pleasure on behalf of the Government and People of the United Republic of Tanzania and indeed, on my own behalf, to extend to Your Excellency and through you to the Government and People of the Republic of Angola, our heartfelt and warmest congratulations on the occasion of celebrating the 40th Anniversary of the independence of your great nation on 11th November 2015.


As we join you in celebrating this auspicious and historic occasion, I wish to express my satisfaction with the cordial and brotherly bilateral relations that so happily exist between our two brotherly countries. Tanzania reaffirms its commitment to continue strengthening these relations through closer cooperation in social–political and economic fields for the mutual benefit of our two countries and peoples.


While wishing you a successful celebration, please accept, Your Excellency and Dear Brother, the assurance of my highest esteem as well as prosperity for the people of the Republic of Angola”.


Issued by: THE MINISTRY OF FOREIGN AFFAIRS AND INTERNATIONAL COOPERATION, DAR ES SALAAM.
10TH NOVEMBER, 2015






Monday, November 9, 2015

Amb. Mulamula meets Vice President of Africa Analysis

Permanent Secretary to the Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation, Amb. Liberata Mulamula (R) exchanges views with the Vice President of Africa Analysis, Mr. Mark Schroeder today at the Ministry's Office. Mr. Schroeder commended the Tanzania Gaovernment for conducting free, fair and transparent election and peaceful transition of power.

The Conversation between Amb. Mulamula and Mr. Schroeder is in progress.


Director of Europe and Americas in the Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation, Amb. Joseph Sokoine (third right), Foreign Services Officer, Mr. Lucas Mayenga (second right) and Information Officer, Mr. Ally Kondo follow the conversation attentively.

 Group photo.

Friday, November 6, 2015

Balozi Mulamula akutana na Wageni mbalimbali Wizarani

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula (kulia) na Waziri wa Mambo ya Nje wa Burundi Mhe. Alain Aime Nyamitwe, walikutana leo na kufanya mazungumzo hapa Wizarani, Mazungumzo yao yalijikita katika kukuza na kuimarisha Ushirikiano kati ya Tanzania na Burundi katika sekta mbalimbali
Balozi wa Tanzania nchini Burundi, Mhe. Rajab Gamah (wa kwanza kushoto), Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje, Balozi Samweli Shelukindo (katikati) na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bi. Mindi Kasiga nao wakifuatilia kwa makini mazungumzo yaliyo kuwa yakiendelea kati ya Baozi Mulamula na Waziri Nyamwite (hawapo pichani).  
Waziri Nyamitwe hakusita kuelezea furaha yake ya kupata fursa ya kuhudhuria sherehe za Uapisho wa Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli hapo jana.
Mazungumzo yakiendelea kati ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Balozi Mulamula (wa tatu kushoto) na Waziri wa Mambo ya Nje wa Burundi (wa pili kutoka kushoto), na wakwanza kushoto ni Balozi wa Burundi nchini Mhe. Issa Ntambuka

=====================
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula (kulia) amekutana kwa mazungumzo na Balozi wa Ubelgiji nchini Tanzania, Mhe. Paul A. Cartier. Viongozi walijadiliana namna ya kuboresha  mahusiano kati ya Tanzania na Ubekgiji katika sekta za Kiuchumia, Biashara na Kijamii

Balozi Mulmula akizungumza huku Balozi Cartier (wa kwanza kushoto) akimsikiliza. Mwingine katika picha ni Afisa Mambo ya Nje, Bi. Felista Rugambwa
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na UShirikiano wa Kiamataifa, Balozi Liberata Mulamula akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola Mhe. Dkt. Josephine Ojiambo (kushoto) aliyeiwakilisha Jumuiya hiyo kwenye sherehe za uapisho wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli hapo jana 
Balozi Mulamula akizungumza na Dkt. Ojiambo alipotembelea Wizarani leo
Balozi Liberata Mulamula akiwa katika picha ya pamoja na Dkt. Ojiambo
Picha ya pamoja


Picha na Reginald Philip

Balozi Mulamula awasindikiza Rais wa DRC na Msumbiji


Rais wa Jamuhuri ya Demokrasia ya Kongo, Mhe. Joseph Kabila (wa kwanza kushoto) pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula wakitizama Kikundi cha Ngoma kilichokuwa kikitoa Burudani kwenye Uwanja wa Ndege, Rais Kabila alikuja nchini kuhudhuria Sherehe za uapisho wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli iliyofanyika hapo jana katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
Rais Kabila (katikati) akielekea kwenye ndege, kulia ni Balozi Mulamula na kushoto ni Balozi wa Kongo nchini Mhe. Khalifani Mpango 
Mhe. Rais Kabila akipita kwenye gwaride la heshima lililoandaliwa na Jeshi la wananchi Tanzania
Katibu Mkuu Mhe. Balozi Liberata Mulamula (kulia) akiagana na Rais Joseph Kabila tayari kwa kuanza safari ya kuelekea nchini kwake. 

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula (mwenye pochi mkononi) akiagana na Rais wa Msumbiji Mhe. Filipe Nyusi 
Rais Nyusi akiagana na Balozi wa Tanzania nchini Msumbiji, Mhe. Shamimu Nyanduga.
Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa ambaye  anawakilisha pia nchini Algeria, Mhe. Begun Taj akimsindikiza Waziri wa  Nchi anayeshughulikia masuala ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Algeria, Mhe. Ramtane Lamamra. Mhe. Lamamra alikuja nchini kwa ajili ya kuhudhiria Sherehe za uapisho wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John Pombe Magufuli.
Mhe. Lamamra akipanda kwenye ndege tayari kabisa kuanza safari ya kurejea nchini Algeria


Picha na Reginald Philip