Wednesday, September 28, 2016

Mhe. Rais apokea Hati za Utambulisho za Balozi wa Uingereza nchini

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Uingereza nchini, Mhe. Sarah Catherine Cooke, Ikulu Jijini Dar es Salaam
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba akisalimiana na Mhe. Balozi Sarah Catherine Cooke mara baada ya kuwasilisha hati za utambulisho.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Aziz Mlima akisalimiana na Mhe. Balozi Sarah Catherine Cooke mara baada ya kuwasilisha hati za utambulisho.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na Mhe. Balozi Sarah Catherine Cooke. Katika mazungumzo yao Mhe. Balozi amewasilisha ahadi ya  Uingereza ya kuchangia kiasi cha paundi milioni 2.3 kwa ajili ya waathirika wa tetemeko la Ardhi Mkoani Kagera.
Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika Balozi Joseph Sokoine akisalimiana na Mhe. Balozi Sarah Catherine Cooke mara baada ya kuwasilisha hati ya utambulisho
Balozi wa Uingereza nchini, Mhe. Sarah Catherine Cooke  akitoa heshima wakati wimbo wa Taifa lake ukipigwa mara baada ya kuwasili Ikulu Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuwasilisha hati za utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt John Pombe Magufuli. Kulia ni Kaimu Mkuu wa Itifaki, Bw. James Bwana
Mhe.Rais John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Viongozi na Watendaji wa Serikali, Mhe. Balozi Sarah Catherine Cooke na baadhi ya Maofisa kutoka ubalozi wa Uingereza Nchini

Ubalozi wa China nchini waadhimisha miaka 67 ya Taifa lao

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage akizungumza katika hafla ya kuadhimisha miaka 67 ya Taifa la Jamhuri ya Watu wa China. Katika hotuba yake Mhe. Mwijage aliipongeza Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China kwa kuendeleza mahusiano mazuri baina ya Tanzania na nchi yao pia kuendelea kushirikiana katika kuboresha sekta mbalimbali nchini. Hafla hiyo imefanyika katika Ubalozi wa Jamhuri ya Watu wa China Jijini Dar es Salaam.
Naibu Balozi wa Ubalozi wa China hapa nchini naye akizungumza na kuwakaribisha wageni waalikwa wote.
Sehemu ya Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini walioshiriki maadhimisho hayo
Naibu Balozi akiendelea kuzungumza huku wageni waalikwa wakimsikiliza.
Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Balozi Mbelwa Kairuki (kushoto), akizungumza na kubadilishana mawazo na wageni waalikwa waliohudhuria hafla hiyo
Waziri wa Nishati na Madini, Mhe. Sospeter Mhongo (kulia), akimsikiliza Balozi wa Kenya hapa nchini Mhe. Chirau Ali Mwakwere alipokuwa akizungumza nae walipokutana katika hafla hiyo

Tuesday, September 27, 2016

OMAN YAONESHA NIA YA KUKARABATI “HOUSE OF WONDERS” -ZANZIBAR

Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Sultanate of Oman, Dkt Augustine Mahiga ( kushoto) na Yusuf bin Alawi bin Abdullah wakizungumzia kuhusu namna ya kuendelea kuimarisha uhusiano mzuri baina ya nchi hizo mbili. Katika mazungumzo hayo Waziri Mahiga ameiomba serikali ya Oman kupitia Waziri Abdullah kuangalia uwezekano wa kushirikiana katika uhifadhi ya nyaraka na kumbukumbu muhimu pamoja na ukarabati ya jengo la House of Wonders lilojengwa na ufalma wa Oman mwaka 1883.

Jengo maarufu la Beit Al Jaib ( House of Wonders) ambalo Serikali ya Tanzania inaiomba Serikali ya Oman kuangalia uwezekano wa kulikarabati kama sehemu ya mradi wa kuhifadhi nyaraka, kumbukumbu na majengoa ya kihistoria visiwani Zanzibar
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mshariki, Augustine Mahiga akizungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani anayehusika na masuala ya Afrika, Mazungumzo yao yalijielekeza zaidi katika uhusiano na ushirikiano kati ya nchi hizi mbili.

=================================

Na Mwandishi Maalum, New  York

Ufalme wa Oman umeonesha nia ya  kukarabati  majengo  ya makubusho ya kale   ya  Beit Al Jaib  maarufu kama “ House  of  Wonders” yaliyopo  mjini  Unguja – Zanzibar.

Nia hiyo imeoneshwa na   Waziri wa Mambo ya   Nje wa  Oman,  Bw. Yusuf bin Alawi bin Addullah wakati   alipokutana na kufanya  mazugumzo na  Waziri wa Mambo ya Nje  na  Ushirikiano wa  Afrika Mashariki, Dkt, Augustine Mahiga.

Mazungumzo  baina ya  viongozi  hao wawili  yalifanyika  pembezoni mwa  Mkutano wa 71 wa  Baraza Kuu la  Umoja wa Mataifa, ambapo  Mawaziri hao walikuwa wakiongoza ujumbe wa Nchi  zao.

Mazungumzo   ya   Mawaziri  hao  yalijikita  katika   uimarishwaji wa uhusiano  na ushirikiano mzuri  uliopo  baina ya  Oman na  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Katika majadilaino hayo ambapo   pamoja  na  mambo mengine,  Waziri  Mahinga  aliomba  serikali ya Oman kuangalia uwezekano  wa kuanzishwa  kwa miradi wa kutunza mambo ya kale zikiwamo nyaraka muhimu zinazohusu uhusiano  baina ya nchi  hizo mbili.

Waziri Mahiga  alieelezea  pia hali uchakavu wa  majengo ya   Beit Al Jaib ( House of wonders)   majengo yaliyokuwa  Ikulu ya  utawala wa Kifalme, Zanzibar.  Makubusho hayo  yamesheheni historia ya  uhusiano  na ushirikiano kati  ya  Zanzibar na   Sultanate of Oman na  Afrika  Mashariki kwa Ujumla.

Na kutokana na historia hiyo na  umuhimu wa  jengo hilo ambalo limejengwa mwaka 1883, Waziri ameiomba  Serikali ya  Oman kuangalia  uwezekano wa kulihifadhi jingo hilo ambalo pia ni kivutio kikubwa cha utalii.

Akijibu  ombi  hilo na  mengine yaliyowasilishwa na   Waziri Mahinga,  Waziria wa Mambo ya Nje wa Oman,  Bw .   Yusuf bin Alawi bin Addullah amemtaka  Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa  Afrika   Mashariki kuandaa andiko  na  kuliwasilisha  katika Serikali ya  Oman ili  pendekezo  hilo liweze  kufanyiwa kazi pamoja na mapendekezo mengine.

Katika  hatua nyingine,  Waziri wa Mambo ya Nje  na  Ushirikiano wa   Afrika Mashariki,  Augustine  Mahiga amekuwa na   kuwa  na mazungumgo na   Bi. Linda Thomas Greenfield,   Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani anayehusika na  masuala ya   Afrika.

Mazungumzo ya  Waziri Mahinga na   Bi.  Linda Greenfield yalijikita zaidi  katika uhusiano na  ushirikiano  baina ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Marekani.