Wednesday, September 28, 2016

Ubalozi wa China nchini waadhimisha miaka 67 ya Taifa lao

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage akizungumza katika hafla ya kuadhimisha miaka 67 ya Taifa la Jamhuri ya Watu wa China. Katika hotuba yake Mhe. Mwijage aliipongeza Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China kwa kuendeleza mahusiano mazuri baina ya Tanzania na nchi yao pia kuendelea kushirikiana katika kuboresha sekta mbalimbali nchini. Hafla hiyo imefanyika katika Ubalozi wa Jamhuri ya Watu wa China Jijini Dar es Salaam.
Naibu Balozi wa Ubalozi wa China hapa nchini naye akizungumza na kuwakaribisha wageni waalikwa wote.
Sehemu ya Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini walioshiriki maadhimisho hayo
Naibu Balozi akiendelea kuzungumza huku wageni waalikwa wakimsikiliza.
Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Balozi Mbelwa Kairuki (kushoto), akizungumza na kubadilishana mawazo na wageni waalikwa waliohudhuria hafla hiyo
Waziri wa Nishati na Madini, Mhe. Sospeter Mhongo (kulia), akimsikiliza Balozi wa Kenya hapa nchini Mhe. Chirau Ali Mwakwere alipokuwa akizungumza nae walipokutana katika hafla hiyo

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.