Tuesday, September 20, 2016

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje apokea Nakala za Utambulisho za Balozi Mteule wa Sudan nchini

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Sudan nchini, Mhe.Mahjoub Ahmed Abdallah Sharfi. Tukio hilo lilifanyika Wizarani tarehe 20 Septemba, 2016.
Mhe. Dkt. Kolimba akizungumza na Balozi Sharfi mara baada ya Balozi huyo kuwasilisha Nakala zake za utambulisho
Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samuel Shelukindo akiwa pamoja na Afisa Mambo ya Nje wakifuatilia mazungumzo kati ya Naibu Waziri, Mhe. Dkt. Kolimba na Balozi Mteule wa Sudan, Mhe. Sharif (hawapo pichani).


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.