Friday, September 30, 2016

Waziri Mkuu apokea msaada wa Waathirika wa tetemeko la ardhi Kagera

Waziri Mkuu akipokea hundi ya Shilingi milioni 80 ikiwa ni msaada kutoka Serikali y Pakstan uliokabidhiwa na Kaimu Balozi wa Nchi hiyo Nchini Bw. Amir Khan kwa waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera.Hafla iliyofanyika Hotel ya Hyatt Jijini Dar es Salaam. Wengine katika picha ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga na Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Mhe. Prof. Joyce Ndalichako.
Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga na Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Mhe. Prof. Joyce Ndalichako wakipokea hundi ya shilingi Milioni 60 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa yaliyoathiriwa na tetemeko la ardhi Mkoani Kagera kutoka Kampuni ya Simu ya Huawei ya nchini China. Wakwanza kushoto ni Mkurugezi wa Kampuni hiyo Nchini Bw. Bruce Zhang
Kaimu Balozi wa Pakstan nchini, Bw. Amir Khan akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi misaada ya wahanga wa tetemeko la ardhi Mkoani Kagera
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akizungumza katika hafla hiyo
Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na Mawaziri, Mabalozi na wadau wengine waliohudhuria makabidhiano hayo
Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia ,Balozi Mbelwa Kairuki akifuatilia hafla ya makabidhiano ya msaada wa wahanga wa tetemeko la  ardhi Mkoani Kagera iliyofanyika katika Hoteli ya Hyatt Jijini Dar es Salaam


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.