Wednesday, September 28, 2016

Mhe. Rais apokea Hati za Utambulisho za Balozi wa Uingereza nchini

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Uingereza nchini, Mhe. Sarah Catherine Cooke, Ikulu Jijini Dar es Salaam
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba akisalimiana na Mhe. Balozi Sarah Catherine Cooke mara baada ya kuwasilisha hati za utambulisho.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Aziz Mlima akisalimiana na Mhe. Balozi Sarah Catherine Cooke mara baada ya kuwasilisha hati za utambulisho.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na Mhe. Balozi Sarah Catherine Cooke. Katika mazungumzo yao Mhe. Balozi amewasilisha ahadi ya  Uingereza ya kuchangia kiasi cha paundi milioni 2.3 kwa ajili ya waathirika wa tetemeko la Ardhi Mkoani Kagera.
Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika Balozi Joseph Sokoine akisalimiana na Mhe. Balozi Sarah Catherine Cooke mara baada ya kuwasilisha hati ya utambulisho
Balozi wa Uingereza nchini, Mhe. Sarah Catherine Cooke  akitoa heshima wakati wimbo wa Taifa lake ukipigwa mara baada ya kuwasili Ikulu Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuwasilisha hati za utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt John Pombe Magufuli. Kulia ni Kaimu Mkuu wa Itifaki, Bw. James Bwana
Mhe.Rais John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Viongozi na Watendaji wa Serikali, Mhe. Balozi Sarah Catherine Cooke na baadhi ya Maofisa kutoka ubalozi wa Uingereza Nchini

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.