Sunday, July 8, 2018

Waziri Mahiga atembelea maonesho ya 42 ya biashara ya kimataifa (Sabasaba)



Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akisaini kitabu cha wageni, alipotembelea banda la Wizara hiyo kwenye maonesho ya 42 ya biashara ya kimataifa yanayoendea katika viwanja vya sabasaba jijini Dar es Salaam.
Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (katikati) akisikiliza maelezo kutoka kwa Bi. Mindi Kasiga Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Wizara ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, alipotembelea banda la Wizara.

Mhe. Balozi Dkt. Mahiga akiwa katika mahojiano na wanahabari kwenye maonesho ya biashara kimataifa maarufa sabasaba yanayofanyika jijini Dar  es Salaam
Mhe.Waziri akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watumishi wa Wizara alipotembelea banda la Wizara kwenye maonesho ya sabasaba

Mhe. Mahiga akisikiliza maelezo kutoka kwa watumishi wa Wizara kwenye maonesho ya biashara ya kimataifa ya sabasaba

Thursday, July 5, 2018

Naibu Waziri atembelea maonesho ya 42 ya biashara ya kimataifa (sabasaba)



Mhe. Dkt. Susan Kolimba Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,  akisaini kitabu cha wageni kwenye banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

 Wa kwanza kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje Bi. Mindi Kasiga pamoja na watumishi wa Wizara. 

Dkt. Kolimba alifurahishwa na ushiriki wa Wizara  kwenye maonyesho ya sabasaba, ambapo aliwasisitiza watumishi wa Wizara kuendelea kutumia fursa hiyo kutoa elimu kwa umma kuhusu shughuli mbalimbali zinazofanywa na Wizara. 
 Mhe.Dkt. Kolimba akipata maelezo kutoka kwa Bi. Mindi Kasiga

Mhe. Dkt. Susan Kolimba akizungumza na watumishi alipotembelea banda la Wizara kwenye maonesho ya sabasaba

Mkurugenzi wa Masomo wa Chuo cha Diplomasia Prof. Watengere Kitojo  akizungumza na watumishi alipotembelea Banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwenye maonesho ya sabasaba .
Wanafunzi kutoka Chuo cha Diplomasia wakipata maelezo kutoka kwa watumishi wa Wizara walipotembelea bandala kwenye maonesho ya saba.Wanafunzi hao walipata fursa ya kuelezwa kuhusu masuala mbalimbali ya ushirikiano wa kikanda na kimataifa sambamba na fursa na faida zinazopatikana.
Bw. Teodos Komba Afisa Mawasilino, akielezea jambo kwa wananchi waliojitokeza  kwenye banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Bw. Hassan Mnondwa akielezea jambo kwa wananchi waliotembelea banda la Wizara.

Mhe.Dkt. Susan Kolimba akiwa katika Picha ya pamoja na Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki alipotembelea banda la Wizara

Tuesday, July 3, 2018

Wananchi waendelea kujitokeza katika banda la Wizara kwenye maonesho ya sabasaba


Mama Anna Mkapa Mke wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mhe. Benjamin William Mkapa, akiangalia moja ya machapisho yanayopatikana katika banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwenye maonesho ya biashara ya sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam.

Wananchi wengi wameendelea kujitokeza kwenye banda la Wizara ili kuongeza  uelewa  juu ya shughuli mbalimbali zinazofanywa na Wizara, ikiwemo namna Wizara inavyosimamia na kuteleza sera ya mambo ya nje ya nchi,  faida  na hatua mbalimbali za mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki lipo katika jengo la sabasaba hall.Wananchi  wote wanakaribishwa 
Maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (kushoto) wakizungumza na wananchi waliojitokeza kwenye banda la Wizara (kulia)



Sehemu nyingine ya watumishi wa Wizara wakihudumia wananchi

Sehemu nyingine ya wananchi wakiuliza masuala mbalimbali kwa watumishi wa Wizara
Sehemu nyingine ya wananchi wakipata maelezo kutoka kwa watumishi wa Wizara

Sehemu nyingine ya wananchi wakipewa maelezo na mtumishi wa Wizara

Friday, June 29, 2018

Mkutano wa 15 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Uchukuzi, Mawasiliano na Hali ya Hewa wafikia tamati


Mhe. Prof. Makame Mbarawa  Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, akizungumza kwenye Mkutano wa 15 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Uchukuzi, Mawasiliano na Hali ya Hewa la Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika jijini Arusha katika ukumbi wa mikutano wa Makao Makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Mhe. Prof.Mbarawa akizungumza katika mkutano huo amezisihi nchi wananchama za Jumuiya ya Afrika Mashariki kuongeza kasi ya kutekeleza miradi inayopangwa katika ngazi ya Jumuiya kwa kuzingatia ukomo wa tarehe.


Mhe. Prof. Makame Mbarawa  Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano akisaini taarifa ya mkutano mara baada ya  majadiliano

Kutoka kushoto  Bibi. Zaina Ibrahim Mwalukuta Mkurugenzi wa Viwanja vya Ndege Zanzibar (ZAA), Dkt. Leonard Chamuriho Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Sekta ya Uchukuzi, Dkt. Maria Sassabo Katibu Mkuu Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano na Mhandisi Happiness Mgalula Mkurugenzi wa barabara, Wizara ya Ujuenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Sekta ya Ujenzi wakifuatilia mkutano

Meza kuu ikiongoza mjadala wakati wa mkutano

Sehemu ya wajumbe wakifuatilia mkutano


Mhe. Prof. Mbarawa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano akizungumza wakati wa mkutano

JAJI IMANI ABOUD ASHINDA UCHAGUZI WA MAJAJI WA MAHAKAMA YA AFRIKA YA HAKI ZA BINADAMU NA WATU


Jaji Imani Aboud wa Tanzania


JAJI IMANI ABOUD WA TANZANIA ASHINDA UCHAGUZI WA MAJAJI WA MAHAKAMA YA AFRIKA YA HAKI ZA BINADAMU NA WATU


Mkutano wa 33 wa Baraza la Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Umoja wa Afrika unaoendelea Jijini Nouakchott, Mauritania kwa siku mbili, leo tarehe 29 Juni, 2018 umefanya uchaguzi wa Majaji wanne wa Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu.
Mgombea wa Tanzania Mhe. Jaji Imani D. Aboud ameshinda uchaguzi huo kwa kura 47 kati ya kura 50 zilizopigwa na kufanikiwa kuchukua nafasi ya Jaji Solomy Balungi Bossa wa Uganda aliyejiuzulu nafasi hiyo kabla ya kumaliza kipindi chake.
Kwa ushindi huo, Mhe. Jaji Aboud atakuwa Jaji wa Mahakama hiyo akiwakilisha Kanda ya Afrika Mashariki kwa kipindi cha miaka miwili.
Majaji wengine walioshinda kwenye uchaguzi huo ni pamoja na Jaji Kioko Ben (Kenya), Jaji Tchikaye Balise (Jamhuri ya Congo), na Jaji Anukam Stella Isibhkhomen (Nigeria).
Ushindi huu unadhihirisha uwezo mkubwa alionao Mhe. Jaji Aboud na heshima kubwa iliyonayo nchi yetu katika Bara la Afrika.
-Mwisho-


Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dar es Salaam, 29 Juni, 2018

Ziara ya Rais Mnangagwa katika picha

Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa akizungumza jambo na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi CCM Dkt. Edmund Mndolwa mara baada ya kuwasili katika Chuo cha Kilimo na Mifugo cha Kaole Bagamoyo mkoani Pwani. Rais huyo wa Zimbabwe alisoma Shuleni hapo mwaka 1963 pamoja na wapigania Uhuru wa Chama cha FRELIMO na ilijulikana kama Shule ya Mafunzo ya Ufundi ya  Wapigania Uhuru wa Chama cha FRELIMO.
Rais wa Zimbabwe Mhe. Emmerson Mnangagwa akizungumza na wafanyakazi pamoja na wanafunzi wanaosoma katika Chuo cha Kilimo na Mifugo cha Kaole (hawapo pichani).
 Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa akiangalia moja ya sufuria waliokuwa wakiitumia kila siku miaka ya sitini, wakati wakisoma katika Shule ya Mafunzo ya Ufundi ya wapigani Uhuru ya Chama cha FRELIMO.
Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa akitoka katika moja ya mabweni yaliyotumika katika mwaka 1963 wakati wakiwa katika Shule ya Mafunzo ya Ufundi ya wapigani Uhuru ya Chama cha FRELIMO ambacho sasa kinajulikana kama Chuo cha Kilimo na Mifugo cha Kaole Bagamoyo mkoani Pwani.
Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa akimsikiliza Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi mara baada ya kumaliza kukagua baadhi ya madarasa na mabweni waliyokuwa wakiyatumia katika Shule ya Mafunzo ya Ufundi ya wapigani Uhuru ya Chama cha FRELIMO ambacho sasa kinajulikana kama Chuo cha Kilimo na Mifugo cha Kaole Bagamoyo mkoani Pwani.
Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa akiwa katika picha na Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi CCM Dkt. Edmund Mndolwa, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Susan Kolimba (Mb.) (wa nne kutoka kushoto mstari wa pili), viongozi wengine wa Tanzania na Zimbabwe pamoja na wanafunzi wanaosoma katika Chuo cha Kilimo na Mifugo cha Kaole Bagamoyo mkoani Pwani

Thursday, June 28, 2018

Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe Mh. Emmerson Mnangagwa afanya ziara nchini.

Ndege iliyombeba Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe Mhe. Emmerson Dambudzo Mnangagwa ikiwasili uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es salaam, tarehe 28 Juni 2018. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akimkaribisha mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe Mhe. Emmerson Dambudzo Mnangagwa mara baada ya kuwasili uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam.


Mhe. Rais Mnangagwa akiwapungia mkono wananchi waliofurika kumlaki katika uwanja wa ndege Dar es salaam.
Mhe. Rais Magufuli akiwa na mgeni wake Mhe. Rais Mnangagwa mara baada ya kukagua vikundi vya ngoma vilivyokuwa vikitumbuiza  uwanjani hapo.

Wednesday, June 27, 2018

Katika picha; Taswira ya jengo la Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja Mpakani (OSBP) cha Tunduma


Mwonekano wa jengo la Tunduma OSBP kwa upande mbele (upande wa kuingilia)
Mwonekano wa jengo la Tunduma OSBP kwa upande wa kuingilia
Mwonekano wa jengo la Tunduma OSBP kwa upande wa kutokea (kuelekea Nakonde, Zambia)

Mwonekano wa jengo la Tunduma OSBP kwa ndani





Baadhi ya vifaa vya ujenzi vikiwa kazini.

Kamati ya ujenzi wa Tunduma OSBP ikiwa kwenye kikao cha kutathimini maendeleo ya ujenzi kilichofanyika katika moja ya ukumbi wa mikutano uliopo kwenye jengo hilo hivi karibuni.

Kamati ya ujenzi ikitembelea sehemu ya eneo la kuegesha magari ambalo ujenzi wake bado unaendelea
Kamati ya ujenzi ikiangalia maendeleo ya ujenzi wa ghala la kuhifadhia bidhaa katika kituo hicho.
Mradi wa ujenzi wa Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja Mpakani (OSBP) cha Tunduma, mpaka kati ya Tanzania na Zambia umekamilika kwa takribani 95%. 

Ujenzi wa Kituo hiki unatarajiwa kuboresha mazingira ya biashara baina ya nchi hizi mbili (Tanzania/Zambia). 

Ujenzi wa mradi huu ulioanza mwaka 2016 umechukua ukubwa wa eneo linalokadiriwa kuwa na takriban kilomita za mraba 43,000.

Ujenzi wa mradi huu unafadhiliwa na shirika la TradeMark  East Afrika.

Mkutano wa 16 wa Majadiliano ya Kisiasa kati ya Tanzania na Korea Kusini wafanyika jijini Dar

 Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Astralasia Bibi Yusta Nyange (wa pili kutoka kushoto) akifurahia jambo kwenye majadiliano ya 16 ya Kisiasa kati ya Tanzania na Jamhuri ya Korea, yaliyofanyika tarehe 27 Juni 2018 , katika ukumbi wa mikutano wa Julius Nyerere(JNICC), Dar es salaam.
Wengine katika picha ni Maafisa kutoka Wizarani  Emmanuel Luangisa(wa mwisho kulia), Ramla Hamisi(wa kwanza kulia) na anayefuata ni Bi Blandina Kasagama wakifuatilia majadiliano hayo.
Pamoja na mambo mengine majadiliano hayo yalijikita katika kuzungumzia namna ya kuimarisha mahusiano yaliyopo kati ya Tanzania na Korea katika maeneo mbalimbali.
 Mkutano ukiendelea
Naibu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika na Mashariki ya Kati, Bw. KOH Kyung-sok(wa pili kushoto), akiwa na ujumbe wake kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Korea na Ubalozi wa Korea nchini wakiwa katika majadiliano hayo.
 Bibi Yusta Nyange(kulia) akipokea zawadi kutoka kwa Bw.
KOH Kyung-sok baada ya Mkutano.
Bibi Yusta Nyange(kulia) akimkabidhi zawadi Bw. KOH Kyung-sok baada ya Mkutano.
Picha ya Pamoja baada ya Mkutano