Friday, March 12, 2021

TANZANIA YAJIVUNIA MIAKA 40 YA MAFANIKO SADC

 Na Mwandishi wetu,

Tanzania imejivunia mafanikio iliyoyapata katika kipindi cha  miaka 40 ya uanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) ameyataja mafanikio hayo kuwa ni pamoja na miaka 40 ya uanachama wa SADC tangu 1979, lugha ya kiswahili kutumika katika mikutano yote ya kisekta ya SADC pamoja na kutengenzwa sanamu maalumu ya Hayati Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere.  

“Pamoja na mambo mengine, mkutano wetu wa leo wa Baraza la Mawaziri wa SADC tunategemea kujadili masuala mbalimbali anayohusu jumuiya hiyo likiwemo suala la matumizi ya lugha ya Kiswahili katika mikutano yote ya kisekta,” Amesema Prof. Kabudi.

Mambo mengine yatakayojadiliwa ni pamoja na suala la kutengeneza sanamu maalumu ya Hayati Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere ambapo sanamu hiyo itawekwa katika jengo la Amani Addis Ababa nchini Ethiopia, pamoja na maadhimisho ya miaka 40 ya SADC.

“Hivyo kupitia mkutano huu tutakamilisha mchakato wa kumpata mtu atakae ifua sanamu hiyo ya Mwl. Nyerere ambapo itawekwa katika jingo la Amani Ethiopia,” Amesema Prof. Kabudi

Prof. Kabudi ameendelea kueleza kuwa katika mkutano huo suala la maadhimisho ya miaka 40 ya SADC pia limejadiliwa ikiashiria umoja wa SADC kudumu kwa miaka 40.

“Miaka 40 ya SADC ina umuhimu mkubwa sana kwa Tanzania kwa sababu miongoni mwa viongozi nane walioasisi sadc ni Mwl. Julius Nyerere katika mkutano uliofanyika mwaka 1979 mkoani Arusha ambapo Tanzania iliamua kuingia rasmi katika jumuiya hiyo,” Ameongeza Prof. Kabudi 

Tanzania itakuwa inasherekea miaka 40 ya SADC ikiwa tayari Kiswahili ni moja ya lugha rasmi za jumuiya hiyo, lakini pia ikiwa na sanamu maalumu ya kumuenzi na kumheshimu baba wa Taifa na Muasisi wa SADC Mwl. Julius Nyerere.

Hivyo Ujumbe wa Tanzania katika mkutano huo unaongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb), Waziri wa Afya wa Zanzibar, Mhe. Nassor Ahmed Mazrui, Waziri wa Fedha na Mipango – Zanzibar Mhe. Jamal Kassim Ali, Waziri wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda Mhe. Omar Said Shaaba, Naibu Waziri Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto, Dkt. Godwin Mollel, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na UShirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge pamoja na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Amina Khamis Shaban.

Februari 27, 2021 katika mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) ulifanyika kwa njia ya Mtandao, wakuu wan chi waliridhia lugha ya Kiswahili iwe lugha ya tatu katika shughuli za jumuiya hiyo sambamba na lugha ya kifaransa kuwa lugha ya nne.

Kadhalika, Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC katika mkutano wao wa 39 uliofanyika jijini Dar es Salaam mwezi Augusti, 2019 waliridhia na kuipitisha kiswahili nne ya mawasiliano, ikiungana na lugha za Kifaransa, Kiingereza na Kireno zinazotumika katika jumuiya hiyo.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akifuatilia Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb), katikati pamoja na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge na Kaimu Mkurugenzi, Idara ya Ushirikiano wa Kikanda, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Agnes Kayola wakifuatilia mkutano


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiteta jambo na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge wakati wa mkutano wa baraza la mawaziri  


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (anaesoma taarifa) na Waziri wa Afya wa Zanzibar, Mhe. Nassor Ahmed Mazrui (kulia) pamoja na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge (kushoto) wakifuatilia mkutano  


Ujumbe wa Tanzania ukiendelea kufuatilia mkutano wa Baraza la Mawaziri SADC


Ujumbe wa Tanzania ukiendelea kufuatilia mkutano wa Baraza la Mawaziri SADC

Mkutano ukiendelea  


Wednesday, March 10, 2021

TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI

 


MAKATIBU WAKUU SADC WAENDELEA NA KIKAO

 Na Mwandishi wetu,

Makatibu Wakuu wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) wameendelea na kikao chao kwa siku ya pili ikiwa ni maandalizi ya mkutano wa baraza la mawaziri wa SADC unaotarajiwa kufanyika tarehe 12 – 13 Machi, 2021 kwa njia ya mtandao jijini Dar es Salaam.  

Ujumbe wa Tanzania katika kikao hicho unaongozwa na Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge pamoja na Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Amina Shaban.   

Mkutano wa Baraza la Mawaziri ujumbe wa Tanzania utaongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Africa Masahariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) ataongoza ujumbe wa Tanzania.

Mwenyekiti wa Sasa katika Jumuiya ya SADC ni msumbiji na ndiye atakayeongoza majadiliano ya Mkutano huu.

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge akiwasilisha mada katika kikao cha Makatibu Wakuu wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kinachoendelea jijini Dar es Salaam kwa njia ya mtandao. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Amina Shaban. Kikao hicho ni maandalizi ya Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC utakafanyika tarehe 12 - 13, Machi 2021 kwa njia ya mtandao jijini Dar es Salaam. 


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge akiwasilisha mada katika kikao cha Makatibu Wakuu wa SADC kinachoendelea jijini Dar es Salaam kwa njia ya mtandao. Kikao hicho ni maandalizi ya Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC utakafanyika tarehe 12, Machi kwa njia ya mtandao jijini Dar es Salaam. 


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge, akiongoza ujumbe wa Tanzania katika kikao cha makatibu wakuu wa SADC, kushoto ni Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Amina Shaban pamoja na Kaimu Mkurugenzi, Idara ya Ushirikiano wa Kikanda, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Agnes Kayola


Washiriki wa kikao cha makatibu wakuu wakifuatilia kikao kinachoendelea kwa njia ya mtandao jijini Dar es Salaam


Washiriki wa kikao cha makatibu wakuu wakifuatilia kikao kinachoendelea kwa njia ya mtandao jijini Dar es Salaam


Kikao kikiendelea  



Monday, March 8, 2021

KISWAHILI CHAPENDEKEZWA KUTUMIKA RASMI SADC

 Na Mwandishi wetu, Dar es Salaam

Lugha ya Kiswahili imependekezwa kuanza kutumika rasmi katika majadiliano kwenye vikao vya ngazi ya baraza la mawaziri na katika utendaji wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).

Pendekezo hilo limewasilishwa na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge katika kikao cha Makatibu Wakuu wa SADC kilichofanyika leo jijini Dar es Salaam kwa njia ya mtandao.

“Sisi kama Tanzania tumependekeza suala la lugha ya Kiswahili kutoka kwenye lugha ya kazi kwenye ngazi ya baraza la mawaziri hadi wakuu wa nchi na serikali wa SADC linabadilika na kuiwezesha lugha ya Kiswahili kuwa lugha rasmi kwenye utendaji wa SADC,” Amesema Balozi Ibuge.

Balozi Ibuge ameongeza kuwa, SADC wamekuwa wakitumia lugha za kikoloni kwa muda mrefu na kwa busara za wakuu wa nchi na Serikali wameamua kuanza kwa mpangilio ambapo lugha ya Kiswahili itaanza kutumika katika ngazi ya baraza la mawaziri pamoja na  vikao vya wakuu wa nchi, na kuishusha lugha hiyo kwenye sekta na kuingia rasmi katika matumizi ya SADC.

Kikao hicho ni maandalizi ya Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC unaotegemewa kufanyika tarehe 12, Machi jijini Dar es Salaam kwa njia ya mtandao.

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge akiwasilisha mada katika kikao cha Makatibu Wakuu wa SADC kilichofanyika leo jijini Dar es Salaam kwa njia ya mtandao


Mkutano ukiendelea 


Mkutano ukiendelea 



UFARANSA KUENDELEZA AWAMU YA TANO YA MRADI WA MABASI YA MWENDOKASI

 Na Mwandishi wetu,

Serikali ya Ufaransa imeahidi kutoa Euro milioni 150 sawa na shilingi za kitanzania bilioni 413 kwa ajili ya kuendeleza mradi wa awamu ya tano wa ujenzi wa mradi wa mabasi ya mwendokasi jijini Dar es Salaam.

Ahadi hiyo imetolewa na Balozi wa Ufaransa hapa nchini, Mhe. Frederic Clavier wakati alipokutana kwa mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi, (Mb) katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.

Prof. Kabudi amesema kuwa mazungumzo yake na Mhe. Clavie yalijikita katika utekelezaji wa mambo waliyokubaliana wakati alipofanya ziara ya kikazi mwezi Februari nchini Ufaransa.

“Leo katika mazungumzo yangu mimi na Mhe. Balozi tumejadili mambo mbalimbali likiwemo suala la Shirika la Maendeleo la Ufaransa kutoa fedha kwa ajali ya kuendeleza mradi wa awamu ya tano wa ujenzi wa mradi wa mabasi ya mwendokasi jijini Dar es Salaam,” Amesema Prof. Kabudi

Pamoja na mambo mengine, Prof. Kabudi amesema kuwa wamejadili kuhusu miradi ya maendeleo katika sekta ya nishati, maji, afya na kilimo.

“Pia tumejadili kuhusu ushiriki wa Ufaransa katika kuisaidia Tanzania katika uchumi wa buluu, ambapo Shirika la Maendeleo la Ufaransa limeahidi kusaidia Tanzania bara na Zanzibar katika kuendeleza uchumi wa buluu na hasa kuongeza uwezo wa Tanzania kuvua na kuchakata samaki,” Ameongeza Prof. Kabudi.

Kwa upande wake Balozi wa Ufaransa Nchini, Mhe. Frederic Clavier amesema kuwa kikao chake na Mhe. Waziri ni mwanzo wa hatua mpya ya ushirikiano kati ya Tanzania na Ufaransa.

“Nchi ya Tanzania ni nchi ya demokrasia na amani,ambapo inatoa fursa ya kuwekeza katika miradi ya maendeleo, Ufaransa itaendelea kuwa pamoja na Tanzania katika kuhakikisha kuwa inasonga mbele kimaendeleo,” Amesema Balozi Clavie 

Katika tukio jingine Prof. Kabudi amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Umoja wa Ulaya hapa nchini, Mhe. Manfredo Fanti na kujadili mambo mbalimbali ya kuboresha ushirikiano kati ya Umoja wa Ulaya na Tanzania hasa kufuatia utiaji saini wa miradi sita itakayopata uhisani wa fedha kutoka Umoja wa Ulaya.

“Tumekubaliana kuimarisha uhusiano wetu katika maeneo mbalimbali ikiwemo, maeneo ya viwanda, na kuboresha mazingira ya uwekezaji na biashara Tanzania, katika masuala ya mabadiliko ya tabia nchi, kilimo, maji, miundombinu katika kuhakikisha kuwa Tanzania inaongeza uwezo wake wa kuazilisha Nnishati.

Kwa upande wa, Balozi wa Umoja wa Ulaya Mhe. Fanti amesema kuwa pamoja na mambo mengine, wamejadili mambo ya kuboresha uhusiano wa kidiplomasia uliopa baina Umoja wa Ulaya na Tanzania. 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akimkaribisha Balozi wa Ufaransa hapa nchini, Mhe. Frederic Clavier wakati walipokutana kwa mazungumzo katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akimuelezea jambo Balozi wa Ufaransa hapa nchini, Mhe. Frederic Clavier wakati walipokutana kwa mazungumzo katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam


Balozi wa Umoja wa Ulaya hapa nchini, Mhe. Manfredo Fanti akimuelezea jambo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) wakati walipokutana kwa mazungumzo katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam


 

Saturday, March 6, 2021

PROF. KABUDI ATEMBELEA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA NA SERIKALI MKOANI KIGOMA

Serikali ya Tanzania itaendelea kutekeleza ujenzi na ukamilishaji wa miradi mbalimbali ya kimkakati ikiwemo ile iliyopo katika mikoa inayopakana na nchi jirani ili kuharakisha maendeleo ya maeneo hayo.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi,  alipowaongoza Wajumbe wa mkutano wa sita wa tume ya pamoja ya kudumu kati ya Tanzania na Burundi kutembelea miradi mbalimbali ya kimkakati inayotekelezwa na Serikali katika mkoa wa  Kigoma.

Miradi iliyotembelewa ni pamoja na Eneo  Maalum la Uwekezaji wa Kigoma (Kigoma Special Economic Zone-KiSEZ); Uwanja wa Ndege wa Kigoma, Bandari Kavu ya Katosho na Bandari ya Kigoma pamoja  na Kituo cha Pamoja cha Kutoa huduma Mpakani (OSBP) kinachotarajiwa kujengwa katika eneo la Manyovu mkoani Kigoma.

Akiwa kwenye eneo Maalum la Uwekezaji, Prof. Kabudi na Wajumbe wengine walijionea uwekezaji mkubwa uliofanywa kwenye eneo hilo na Kampuni ijulikanayo kama Next Gen Solar wa kuzalisha umeme wa jua wa megawati tano ambao utaanza kusambazwa rasmi kwa wakazi wa Kigoma mwezi Aprili 2021. Upatikanaji wa nishati hiyo ya umeme unatarajiwa kuwanufaisha wakazi wa mkoa huo kiuchumi.

Kadhalika Mhe. Prof. Kabudi na Wajumbe wengine walipata fursa ya kutembelea kampuni ya Third Man Limited inayozalisha Asali ijulikanayo kama Upendo (Upendo Honey) ambayo nayo imewekeza kwenye eneo hilo maalum la KiSEZ. Katika maelezo yake kwa Mawaziri, Mkurugenzi wa Kampuni hiyo Bw. Alex Scovic alisema kuwa Kampuni yake  ambayo inachakata asali inayozalishwa bila kutumia kemikali (organic) inanunua asali hiyo kutoka kwa wafugaji wa nyuki zaidi ya 3,000 waliopo Kigoma na mikoa jirani kama Tabora, Katavi, na Rukwa na baadaye kuiuza asali hiyo nje nchi hususan nchini Marekani.

“Kampuni yetu ni ya kwanza kuwekeza kwenye eneo hili. Tunazalisha Asali safi isiyo na kemikali ambayo ina soko kubwa nje ya nchi hususan nchini Marekani. Biadhaa zetu tunazitangaza kuwa zimetoka Tanzania” alisema.

Pia alijulisha kuwa, Kampuni yake imeajiri zaidi ya vijana 60 wa kitanzania na kwamba mbali na kuchakata asali, kampuni hiyo inazalisha nta ambayo huuzwa nchini Ujerumani ambao huitumia kwa ajili ya kutengeneza vipodozi. Kampuni ya upendo huzalisha zaidi ya tani 4,000 za asali kwa mwaka.

Katika ziara yao kwenye eneo la Bandari Kavu la Kitosho, Mawaziri na Viongozi wengine walijulishwa kuwa eneo hilo limeanzishwa maalum kwa ajili ya kurahisisha usafirishaji na uhifadhi wa mizigo na bidhaa mbalimbali zinazokwenda Burundi kutokea Bandari za Tanzania. Tayari eneo hilo limepata mzabuni atakayeanza ujenzi mwaka huu. Pia Mawaziri hao walitembelea Bandari ya Kigoma na kupata fursa ya kujionea meli kongwe na ya kihistoria ya MV Liemba ambayo ina miaka 108 tangu itengenezwe, MV Mwongozo na MV Sangara ambazo zote zitaanza kufanyiwa ukarabati ili kuziwezesha kuendelea kutoa huduma kwa wananchi wa Kigoma na kutoka nchi jirani.

Wakiendelea na ziara ujumbe huo ulitembelea Uwanja wa Ndege wa Kigoma ambapo ulipata maelezo kutoka kwa Meneja wa TANROAD wa Mkoa wa Kigoma, Mhandisi Narcis Choma kuwa, mradi huo unalenga kupanua na kukarabati maeneo mbalimbali ya Uwanja huo ikiwa ni pamoja na kuongeza urefu wa barabara ya kuruka na kutua ndege ambayo awali ilikuwa na urefu wa mita 1800 na sasa mita 1,300 zitaongezwa ili kuwezesha ndege kubwa kutua. Pia mradi unalenga kujenga jengo la abiria, maegesho ya ndege, usimikaji wa taa na mitambo ya kuongozea ndege, ujenzi wa jengo la kuongozea ndege, maegesho ya magari pamoja na uzio wa usalama.

Mhe. Prof. Kabudi pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje wa Burundi, Mhe. Balozi Albert Shingiro walihitimisha ziara yao kwa kutembelea eneo kitakapojengwa Kituo cha Kutoa Huduma kwa Pamoja Mpakani (OSBP) cha Manyovu na Mugina kwa upande wa Burundi. Wakiwa Manyovu waliweza kutembelea maeneo ambayo vituo hivyo vitajengwa kwa upande wa Tanzania na upande wa Burundi pamoja na kupokea taarifa ya mradi huo ambapo  walijulishwa kwamba tayari usanifu wa ujenzi wa kituo hicho cha Manyovu ambacho kitakuwa cha aina yake umeanza na utakamilishwa mwishoni mwa mwezi Machi 2021.

Akitoa hotuba kuhitimisha ziara kwenye miradi hiyo, Prof. Kabudi alisema Tanzania inawekeza kwenye miradi hiyo ili kurahisisha ufanyaji biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na nchi mbalimbalii inazopakana nazo ikiwemo Burundi. Kwa upande wake, Mhe. Balozi Shingiro alipongeza jitihada hizo za Tanzania na kuahidi kutumia fursa za miradi hiyo ambayo mingi inalenga kuimarisha ushirikiano baina ya Tanzania na Burundi.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akiwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Burundi,Mhe. Balozi Albert Shingiro wakimsikilizaMkurugenzi wa Eneo Maalum la Uwekezaji la Kigoma (KiSEZ), Bw. Omar walipotembelea eneo hilo ili kujionea miradi ya uwekezaji iliyopo. Ziara hiyoilifanyika tarehe 6 Machi 2021 ikiwa ni sehemu ya kuhitimisha mkuatano wa sita wa tume ya pamoja ya kudumu uliofanyika kati ya Tanzania Burundi Mkoani Kigoma tarehe 3 hadi 5 Machi 2021.

Mmoja wa Wataalam  katika kampuni ya kufua umeme wa jua ya ...akitoa maelezo kuhusu mitambo mbalimbali inayotumika kufua umeme huo.

Mtaalam wa umeme wa jua akitoa maelezo kwa Mhe. Prof. Kabudi  walipotembelea eneo maalum la uwekezaji ili kujionea mradi huo ambao ukikamilika utazalisha megawati 5 zitakazosambazwa kwa wakazi wa mkoa wa Kigoma

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Generali Wibert Ibuge akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Mhe. Thobias Andengenye wakati waliposhiriki ziara ya Mawaziri wa Mambo ya Nje kwenye maeneo mbalimbali.

Mhe. Prof. Kabudi akiwa na Mhe. Balozi Shingiro pamoja na Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Dkt. Leonard Chamuriho wakimsikiliza Mkurugenzi wa Kampuni ya Asali ya Third Man Limited inayozalisha ijulikanayo kama Upendo, Bw. Alex Scovic  akifafanua kuhusu Kampuni yake ambayo imewekeza kwenye Eneo Maalum la Uwekezaji la Kigoma,

Prof. Kabudi kwa pamoja na Mhe. Balozi Shingiro wakiangalia Asali inayozalishwa na Kampuni ya Upendo

Mhe. Pfof. Kabudi kwa pamoja na Mhe. Balozi Shingiro wakiangalia mapipa ambayo hutumika kusafirisha Asali nje

Mhe. Prof. Kabudi akiangalia nta iliyokuwepo kwenye Kampuni ya Asali ya Upendo

Mhe. Prof. Kabudi kwa pamoja na Mhe. Balozi Shingiro wakimsikiliza Mkurugenzi wa TANROAD-Kigoma, Mhandisi  Narcis Choma alipokuwa akitoa taarifa fupi kuhus ukarabati wa Uwanja wa Ndege wa Kigoma

Mhe. Prof. Kabudi akionesha eneo ambalo  mita 1300 za barabara ya kurushia na kutua ndege zitaongezwa 



Mhe. Prof. Kabudi kwa pamoja  na Mhe Balozi Shingiro wakiwasili kwenye eneo la Kitosho mjini Kigoma itakapojengwa Bandari Kavu kwa ajili ya kupokea, kuhifadhi na kusafirisha shehena mbalimbali zinazokwenda nchini Burundi kutokea Tanzania

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania, Mhandisi Deusdedit Kakoko akitoa maelezo kuhusu Bandari Kavu hiyo 

Mawaziri wakimsikiliza Mhandisi Kakoko walipowasili kwenye Bandari ya Kigoma

Mhe. Dkt. Chamuriho naye akizungumza kuhusu masuala ya uchukuzi bandarini hapo

Mhe. Prof. Kabudi akisaini kitabu ca wageni mara baada ya kutembelea Meli Kongwe ya Mv Liemba. Meli hiyo ambayo ina historia ya muda mrefu ilitengenezwa mwaka 1913. Serikali inao mpango wa kuikarabati meli hiyo ili iendelee kutoa huduma kwenye Ziwa Taznganyika. Kulia ni Mhe. Dkt. Chamuriho na kushoto ni Nahodha wa Meli hiyo , Bw. Titus Mnyanyi

Nahodha Mnyanyi akitoa maelezo kuhus meli ya MV Liemba

Balozi Ibuge nae akisaini kitabi cha wageni kwenye Meli ya MV Liemba

Mhe. Prof.Kabudi akiwa kwenye chumba cha nahodha huku akionesha namna meli hiyo inavyoendeshwa

Mhe. Balozi Shingiro nae akijaribu usukani wa meli hiyo kongwe nchini

Waheshimiwa viongozi wakifurahia kuwa ndani ya meli hiyo yenye historia kubwa

Mhe. Prof. Kabudi akiwa ameongozana na Mhe. Balozi Shingiro wakiteremka kutoka kwenye Meli ya MV Liemba baada ya kutembelea meli hiyo

Mhe. Prof. Kabudi kwa pamoja na Mhe. Balozi Shingiro wakisaini kitabu cha wageni walipowasili kwenye Ofisi za Forodha za Tanzaniazilizopo  katika eneo la Mpaka wa Manyovu. Mhe. Prof. Kabudi alifika eneo hilo kwa ajili ya kukagua mahali kitakapojengwa Kituo cha Pamoja cha Kutoa Huduma Mpakani /(OSBP)

Makatibu Wakuu wakiwa kwenye Ofisi za Forodha za Tanzania mpakani Manyovu

Mhe. Prof. Kabudi akionesha eneo ambalo Kituo cha OSBP kitajengwa

Balozi wa Tanzania nchini Burundi, Mhe. Jilly Maleko akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Mhe. Thobias Andengenye na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika, Bw. Frank Mwega wakati wa ziara huko Manyovu

Mhe. Prof. Kabudi akiwa na Mhe. Balozi Shingiro wakivuka mpaka kuelekea Burundi kwa ajili ya kujionea eneo ambalo limetengwa na Serikali ya Burundi kwa ajili ya ujenzi wa OSBP

Mhe. Prof. Kabudi akiwa na Mhe. Balozi Shingiro wakiangalia jiwe ambalo ni mpaka kati ya Tanzania na Burundi

Hotuba

Picha ya pamoja ya viongozi wakionesha upande wa Tanzania

Picha ya viongozi wakiwa mpakani

Picha ya pamoja