Wednesday, March 10, 2021

MAKATIBU WAKUU SADC WAENDELEA NA KIKAO

 Na Mwandishi wetu,

Makatibu Wakuu wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) wameendelea na kikao chao kwa siku ya pili ikiwa ni maandalizi ya mkutano wa baraza la mawaziri wa SADC unaotarajiwa kufanyika tarehe 12 – 13 Machi, 2021 kwa njia ya mtandao jijini Dar es Salaam.  

Ujumbe wa Tanzania katika kikao hicho unaongozwa na Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge pamoja na Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Amina Shaban.   

Mkutano wa Baraza la Mawaziri ujumbe wa Tanzania utaongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Africa Masahariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) ataongoza ujumbe wa Tanzania.

Mwenyekiti wa Sasa katika Jumuiya ya SADC ni msumbiji na ndiye atakayeongoza majadiliano ya Mkutano huu.

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge akiwasilisha mada katika kikao cha Makatibu Wakuu wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kinachoendelea jijini Dar es Salaam kwa njia ya mtandao. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Amina Shaban. Kikao hicho ni maandalizi ya Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC utakafanyika tarehe 12 - 13, Machi 2021 kwa njia ya mtandao jijini Dar es Salaam. 


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge akiwasilisha mada katika kikao cha Makatibu Wakuu wa SADC kinachoendelea jijini Dar es Salaam kwa njia ya mtandao. Kikao hicho ni maandalizi ya Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC utakafanyika tarehe 12, Machi kwa njia ya mtandao jijini Dar es Salaam. 


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge, akiongoza ujumbe wa Tanzania katika kikao cha makatibu wakuu wa SADC, kushoto ni Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Amina Shaban pamoja na Kaimu Mkurugenzi, Idara ya Ushirikiano wa Kikanda, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Agnes Kayola


Washiriki wa kikao cha makatibu wakuu wakifuatilia kikao kinachoendelea kwa njia ya mtandao jijini Dar es Salaam


Washiriki wa kikao cha makatibu wakuu wakifuatilia kikao kinachoendelea kwa njia ya mtandao jijini Dar es Salaam


Kikao kikiendelea  



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.