Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia, Mhe. Innocent Shiyo akiwasilisha mada kuhusu fursa za biashara na uwekezaji katika kanda ya Afrika katika mkutano wa mabalozi unaoendelea Zanzibar |
Mkutano wa mabalozi ukiendelea Zanzibar |
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Rajab akitoa tathmini ya mkutano wa mabalozi unaoendelea Zanzibar |
Sehemu ya mabalozi wakifuatilia kikao |
Mabalozi wanaoziwakilisha nchi za Palestina, Indonesia na Vietnam hapa nchini wamefanya ziara katika Hospitali ya CCBRT na kujionea utoaji wa huduma za afya na kazi mbalimbali zinazofanywa na Hospitali hiyo pamoja na kuangalia maeneo ya ushirikiano.
Ziara ya mabalozi hao imefanyika leo Jijini Dar es Salaam ambapo mabalozi waliofanya ziara katika hospitaali hiyo ni Balozi wa Palestina nchini, Mhe. Hamdi Mansour AbuAli, Balozi wa Indonesia nchini, Mhe. Triyogo Jatmiko na Balozi wa Vietnam nchini, Mhe. Nguyen Nam Tien.
Akiongea wakati wa ziara hiyo, Afisa Mtendaji Mkuu wa CCBT, Bi. Brenda Msangi amesema kuwa ziara ya mabalozi hao imelenga kujifunza na kujionea shughuli mbalimbali zinazotolewa na hospitali hiyo na kwamba CCBRT inaamini kuwa baada ya ziara hiyo mabalozi watapata fursa ya kujionea maeneo ya ushirikiano baina ya nchi zao hospitali hiyo.
“Tunategemea baada ya ziara hii mabalozi wataona maeneo ya ushirikiano, sisi kama CCBRT tuna maeneo matatu ambayo tunapenda kushirikiana nao, eneo la kwanza ni utoaji wa huduma, vifaa na vifaa tiba, na mwisho ni kuwajengea uwezo wataalamu wetu. Maeneo yote haya ni muhimu hasa ukizingatia CCBRT inatoa huduma bobezi na za kibingwa,” amesema Bi. Msangi
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati, katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Hemed Mgaza amesema kuwa mabalozi wamefanya ziara katika hospitali hiyo kwa lengo la kujionea utoaji wa huduma mbalimbali zinazotolewa na CCBRT na kupata fursa kuona maeneo ya ushirikiano baina ya nchi zao na CCBRT.
“Katika ziara ya mabalozi hapa CCBRT, mabalozi wameonesha kuridhishwa na shughuli zinazofanywa na hospitali hii, na baada ya ziara hii watawasiliana na nchi zao na kuona maeneo ya ushirikiano katika kuboresha zaidi sekta ya afya,” amesema Balozi Mgaza.
Naye Balozi wa Palestina nchini, Mhe. Hamdi Mansour AbuAli amesema ameridhishwa na huduma zinazotolewa na CCBRT katika kuboresha afya za watanzania nchini na kuahidi kuwasiliana na serikali ya Palestina kuona ni jinsi gani serikali yake inaweza kushirikiana na hospitali hiyo katika kuboresha sekta ya afya nchini Tanzania.
“Nimekuwa nikipita maeneo haya mara kwa mara lakini sikujua kuwa huduma nzuri zinatolewa hapa CCBRT, nawapongeza kwa jitihada hizi za kuuelimisha umma kuhusu magonjwa mbalimbali na njia za kuyakabili. Naahidi baada ya ziara hii nitawasiliana na Serikali yangu na kuona ni maeneo gani tunaweza kushirikiana katika kuboresha sekta ya afya,” amesema Balozi AbuAli
Kadhalika, Balozi wa Indonesia nchini, Mhe. Triyogo Jatmiko amesema kazi inayofanywa na hospitali ya CCBRT katika kuwahudumia watanzania hususan akina mama wenye changamoto ya fistula na watu wenye ulemavu wa viungo ni kazi kubwa na inayoigusa jamii.
“Jitihada zinazofanywa na serikali ya Tanzania katika kuboresha vituo vya afya ni nzuri……nimeguswa na jinsi hospitali hii inavyowahudumia wananchi, baada ya ziara hii tutakaa na kuangalia maeneo ya ushirikiano,” amesema Balozi Jatmiko.
Ziara hiyo iliratibiwa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki iliongozwa na Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati, Balozi Hemed Mgaza pamoja na Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Balozi Ceaser Waitara.
Mabalozi wakiwa katika kituo cha mabinti cha CCBRT wakati walipofanya zaira hospitalini hapo |
Mabalozi wakiwajulia hali akina mama wanaokabiliwa na changamoto ya Fistula katika hospitali ya CCBRT |
Balozi wa Palestina nchini, Mhe. Hamdi Mansour AbuAli akionesha mabalozi wenzake kitu wakati wa ziara ya mabalozi hao katika hospitali ya CCBRT |
Mabalozi wakiwa katika picha ya pamoja na Afisa Mtendaji Mkuu wa CCBRT Bi. Brenda Msangi pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Hospitali hiyo |
Semina ya namna bora ya uzalishaji wa vifaranga vya matango bahari na ukulima bora wa zao la mwani uliofanyika katika Hoteli ya Verde mjini Zanzibar |
Picha ya pamoja |
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imeahidi kuendelea kushirikiana na vyuo vikuu nchini ili kupanua wigo wa kutoa elimu kwa wanafunzi kuhusu fursa mbalimbali zinazotolewa na wahisani yakiwemo mashirika ya Kikanda, Kimataifa na nchi marafiki.
Ahadi hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga alipokutana na Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe. Henry James na baadhi ya Viongozi wa Serikali za wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) na Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) jana katika Ofisi za Mkuu wa Wilaya ya Ubungo.
“Fursa za Masomo Nje ya Nchi na ajira zimekuwa zikitangazwa na kuratibiwa na Wizara ya Mambo ya Nje kwa kushirikiana na wadau wengine ili kuendelea kupanua wigo wa kutoa elimu kwa wanafunzi kuhusu fursa mbalimbali zinazotolewa na Wizara Kikanda na Kimataifa.,” Alisema Balozi Mindi
Naye Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Bw. Kheri James amepongeza jitihada zinazotekelezwa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki katika kuhakikisha watanzania wanapata fursa mbalimbali za masomo na kazi Nje ya nchi kwani jambo hilo ni la kizalendo.
“Wizara ina fursa ya ziada ya kuviunganisha vyuo vikuu nchini na Vyuo Vikuu Nje ya nchi kwa ufadhili wa masomo, mahusiano kati ya vyuo vya Tanzania na vya Nje na kubadilishana wanafunzi katika taaluma mbalimbali ili kuwajengea uwezo na ufanisi katika masomo,”Alisema Bw. James.
Kikao hicho kimehudhuriwa na Rais wa Serikali ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Bw. Spencer Minja na Rais wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji Bw. Mark Makaranga ambapo pamoja na mambo mengine wanafunzi hao wameipongeza na kuiomba Wizara kuandaa Kongamano la wanafunzi wa Elimu ya Juu kuhusu Mtangamano wa Jumuiya ya Kikanda na Kimataifa.
Halmashauri ya Wilaya ya Ubungo ina vyuo vitano ambavyo ni, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Shule Kuu ya Sheria, Chuo cha Maji na Chuo cha Mtakatifu Joseph.
Rais wa Serikali ya wanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji Bw. Mark Makaranga akieleza jambo wakati wa kikao |
Kikao kikiendelea |
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akifungua Mkutano wa Tano wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Malawi uliofanyika jijini Dar es Salaam |
Waziri wa Sheria wa nchini Malawi Mhe. Titus Mvalo akihutubia wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Tano wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Malawi uliofanyika jijini Dar es Salaam |
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro na Waziri wa Sheria wa nchini Malawi Mhe. Titus Mvalo wakibadilishana nyaraka kwenye Mkutano wa Tano wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Malawi uliofanyika jijini Dar es Salaam |
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro na Waziri wa Sheria wa nchini Malawi Mhe. Titus Mvalo wakisaini Hati za Makubaliano kwenye Mkutano wa Tano wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Malawi uliofanyika jijini Dar es Salaam |
Mkurugenzi wa Idara ya Afrika Katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Naimi Azizi akitoa neno la ukaribisho wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Tano wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Malawi uliofanyika jijini Dar es Salaam |
Balozi wa Tanzania nchini Malawi Mhe. Humphrey Polepole akifuatilia Mkutano wa Tano wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Malawi uliokuwa ukiendelea |
Sehemu ya Maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia Mkutano wa Tano wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Malawi uliokuwa ukiendelea jijini Dar es Salaam |
Picha ya pamoja |
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara Bw. Ally S. Gugu na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati Bw. Kheri Abdul Mahimbali wakibadilishana mawazo wakati wa Mkutano wa Tano wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Malawi uliokuwa ukiendelea jijini Dar es Salaam |
Mkutano wa Tano wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Malawi ukiendelea |
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax amewasisitiza Diaspora wote Duniani kutumia huduma za kifedha kupitia kwa watoa huduma waliosajiliwa ili kuendelea kuchangia uchumi wa Tanzania.
Dkt. Tax ametoa wito huo jijini Dar es Salaam aliposhiriki uzinduzi wa huduma ya kutuma na kupokea fedha kwa baadhi ya nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) iliyoanzishwa na Kampuni ya Simu za Mkononi ya Vodacom kupitia huduma ya kutuma fedha ya M-Pesa.
Amesema, upo umuhimu mkubwa kwa Diaspora kutumia huduma za kifedha zilizosajiliwa ili kuhakikisha usalama wa fedha zao na kuweka kumbukumbu sawa. Amesema kwa mujubu wa Takwimu kutoka Benki Kuu ya Tanzania Diaspora walichangia uchumi wa Taifa kwa kiasi cha Dola za Kimarekani milioni 30 mwaka 2019 na mwaka 2021 Diaspora walichangia uchumi wa Taifa kwa Dola za Kimarekani milioni 569 sawa na kuchangia asilimia 0.8 ya pato la Taifa.
Mhe. Dkt. Tax ameipongeza Kampuni ya Vodacom kwa kuwekeza katika ubunifu na kuboresha huduma zao wakati wote ili kuendana na mahitaji ya wananchi kulingana na mabadiliko ya Teknolojia.
Amesema anaipongeza Kampuni hiyo kwa kuwa mstari wa mbele katika kuiunganisha Afrika kupitia huduma zao ambapo kwa sasa wamepanua wigo kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na kuongeza ukanda wa nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) jambo ambalo litawawezesha Diaspora kwenye maeneo hayo kutuma na kupokea fedha pasipo kikwazo chochote.
“Sekta ya fedha ni sekta muhimu katika nchi yoyote, Serikali inaona jambo hili ni kubwa kwa sababu ya umuhimu wa sekta ya fedha lakini kwa kutambua kwa sasa dunia ipo katika uchumi wa kidigitali. Uchumi wa kidigitali unafanya kazi kidigitali hivyo nawasihi Diaspora kutumia huduma hii ili kuweza kuchangia maendeleo ya taifa kwa kuwa benki na taasisi nyingine zinazotoa huduma za kifedha zimerahisisha biashara na uwekezaji na shughuli za kiuchumi kwa ujumla,” alisema Dkt. Tax.
Kadhalika Mhe. Dkt. Tax ameipongeza Benki Kuu ya Tanzania kwa kutoa miongozo mbalimbali inayowawezesha watoa huduma za fedha nchini kuandaa huduma zenye manufaa kwa wanannchi na kuahidi Serikali kuendelea kushirikiana na Sekta Binafsi ili kutimiza lengo la kuwainua wananchi kiuchumi kupitia huduma mbalimbali.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Vodacom M-pesa, Bw. Epimack Mbeteni amesema kuzinduliwa kwa huduma ya M-Pesa katika ukanda wa SADC kumetoa fursa ya kuongeza wigo wa kutuma na kupokea pesa katika nchi nyingi zaidi barani Afrika hususan nchi za SADC.
“Wateja wetu wanaweza kupokea na kutuma fedha katika ukanda wa Sadc, sasa tumeiunganisha Afrika na M-Pesa, jambo hili litachangia ukuaji wa uchumi wa taifa letu,” amesema Bw. Mbeteni
Bw. Mbeteni ameongeza kuwa uzinduzi wa huduma hiyo utarahisisha ufanyaji wa biashara na huduma nyingine za kijamii. Uzinduzi wa huduma hiyo uliongozwa na kauli mbiu ya “Dunia Kijiji, Afrika ni M-Pesa”. Katika uzinduzi huo, Dkt. Tax aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Mhe. Godwin Gondwe.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akiwasilisha hotuba ya ufunguzi aliposhiriki uzinduzi wa huduma ya kutuma na kupokea fedha kwa baadhi ya nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) iliyoanzishwa na Kampuni ya Simu za Mkononi ya Vodacom kupitia huduma ya kutuma fedha ya M-Pesa
Mkurugenzi wa Vodacom M-pesa, Bw. Epimack Mbeteni akiongea na washiriki wakati wa uzinduzi wa huduma ya kutuma na kupokea fedha kwa baadhi ya nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) |
Washiriki wakifuatilia mkutano wa uzinduzi wa wa huduma ya kutuma na kupokea fedha kwa baadhi ya nchi za SADC |
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akizungumza na waandishi wa habari kuhusu huduma ya kutuma na kupokea fedha kwa baadhi ya nchi za SADC |
Washiriki wakifuatilia mkutano wa uzinduzi wa wa huduma ya kutuma na kupokea fedha kwa baadhi ya nchi za SADC |
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax katika picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Mhe. Godwin Gondwe na wafanyakazi wa Kampuni ya simu ya Vodacom |
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine akitoa hotuba ya ufunguzi wa Mkutano wa Tano (5) wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Malawi katika ngazi ya Maafisa Waandamizi unaofayika jijini Dar es Salaam.
|
Sehemu ya ujumbe wa Malawi wakifuatilia Mkutano wa Tano (5) wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Malawi katika ngazi ya Maafisa Waandamizi uliokuwa ukiendelea jijini Dar es Salaam. |
Mkurugenzi wa Idara ya Afrika na Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Malawi Bw. William Kantayeni akichangia jambo kwenye Mkutano wa Tano (5) wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Malawi uliokuwa ukiendelea jijini Dar es Salaam. |
Balozi wa Tanzania nchini Malawi Mhe. Balozi Humphrey Polepole akifuatilia mkutano wa Tano (5) wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Malawi katika ngazi ya Maafisa Waandamizi uliokuwa ukiendelea jijini Dar es Salaam. |
Meza kuu wakifuatilia Mkutano wa Tano (5) wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Malawi katika ngazi ya Maafisa Waandamizi uliokuwa ukiendelea katika ukumbi wa Mikutano wa Kamataifa wa Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam |