Tuesday, May 8, 2012

Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (MB), atafanya mazungumzo na waandishi wa habari kwenye Ukumbi wa Mikutano Wizarani tarehe 09 Mei, 2012 kuanzia saa tano asubuhi.

Masuala atakayozungumzia ni pamoja na kampeni za mgombea wa nafasi ya Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AU), Bi. Nkosazana Dlamini-Zuma, anayeungwa mkono na Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC).

Imetolewa na,

KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI,
WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA,
DAR ES SALAAM.

08 MEI, 2012

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.