Thursday, May 5, 2022

WAZIRI MULAMULA APOKEA NAKALA ZA HATI YA UTAMBULISHO YA BALOZI WA MTEULE WA ETHIOPIA NCHINI

 

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula akipokea Nakala ya Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Ethiopia nchini Mhe. Sibru Mamo Kedida alipofika katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam  kujitambulisha baada ya kuwasili nchini  

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula akionesha Nakala ya Hati za Utambulisho alizopokea kutoka kwa Balozi Mteule wa Ethiopia nchini Mhe. Sibru Mamo Kedida alipofika katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam  kujitambulisha baada ya kuwasili  nchini

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula akiangalia Nakala ya Hati za Utambulisho alizopokea kutoka kwa Balozi Mteule wa Ethiopia nchini Mhe. Sibru Mamo Kedida alipofika katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam  kujitambulisha baada ya kuwasili nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Balozi Mteule wa Ethiopia nchini Mhe. Sibru Mamo Kedida alipofika katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam  kujitambulisha baada ya kuwasili nchini

Balozi Mteule wa Ethiopia nchini Mhe. Sibru Mamo Kedida akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula alipofika katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam  kujitambulisha baada ya kuwasili nchini

Mazungumzo yakiendelea

Mazungumzo yakiendelea

Maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiongozwa na Mkuu wa Itifaki nchini Balozi Yusuph Mndolwa (wa kwanza kushoto) ulioambatana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula  hayupo pichani ukifuatilia mazungumzo kati wa Balozi Mulamula na Balozi Mteule wa Ethiopia nchini alipofika katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam kuwasilisha nakala ya Hati za Utambulisho

Balozi Mteule wa Ethiopia nchini Mhe. Sibru Mamo Kedida akimkabidhi zawadi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula alipofika katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam kukabidhi nkala ya Hti za Utambulisho baada ya kuwasili nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (wa pili kulia) akiwa na Balozi Mteule wa Ethiopia nchini Mhe. Sibru Mamo Kedida (wa pili kushoto) katika picha ya pamoja baada ya kukabidhi Nakala ya Hati za Utambulisho alipofika katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam  kujitambulisha baada ya kuwasili nchini. wa kwanza kulia ni Mkuu wa Itifaki nchini Balozi Yusuph Mndolwa na wa kwanza kushoto ni ofisa Ubalozi wa Ethiopiaa nchini Bw. Mulato.




Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (Mb) amepokea nakala ya Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Ethiopia nchini Mhe. Shibru Mamo Kedida leo katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.

Baada ya kupokea nakala ya hati hizo viongozi hao walipata fursa ya kuzungumza ambapo Balozi Mulamula alimhakikishia Balozi Mteule ushirikiano wa hali ya juu kumuwezesha Balozi huyo kutekeleza majukumu yake ya kibalozi hapa nchini na kuhakikisha uhusiano kati ya Tanzania na Ethiopia unaendelea kuimarika.

‘‘Unaona timu yangu niliyoambatana nayo hapa, nichukue nafasi hii kukuhakikishia kuwa Wizara itakupa ushirikiano wote utakaouhitaji katika kutekeleza majukumu yako, saa 24 milango yetu iko wazi, tunataka uhusiano kati ya nchi zetu uzidi kuimarika,’’ alisema Balozi Mulamula.

Balozi Mulamula amesema Tanzania imefarijika kupata balozi mpya baada ya Balozi wa awali kumaliza muda wake wa uwakilishi, na kuongeza kuwa kitendo hicho ni ishara ya uhusiano mzuri na urafiki uliopo baina ya Tanzania na Ethiopia.

Naye Balozi Mteule wa Ethiopia Mhe. Sibru Mamo Kedida amemshukuru Waziri Mulamula  kwa jinsi alivyompokea na kuelezea uhusiano kati ya Tanzania na Ethiopia ulivo mzuri na kuahidi kuwa atahakikisha uhusiano huo unazidi kukua na kuimarika.

“Ethiopia na Tanzania zimekuwa katika uhusiano mzuri sana  kidiplomasia, nchi zzetu zimekuwa na lengo moja, nitahakikisha uhusiano kati ya nchi hizi unaimarika na hata kufikia nchi hizi Tanzania na Ethiopia zinashirikiana kufanya biashara na uwekezaji kwa maslahi ya pande mbili,” amesema Mhe. Balozi Kedida

 

 

BALOZI MBAROUK AMPOKEA KATIBU MKUU JUMUIYA YA MADOLA ZANZIBAR

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk amempokea Katibu Mkuu Jumuiya ya Madola Mhe. Patricia Scotland alipowasili Zanzibar katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume.

Mhe. Scotland yupo nchini kwa ziara maalumu ya kukutana na kumfahamisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan maudhui ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Madola unaotarajiwa kufanyika nchini Rwanda mwezi Juni 2022.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akimpokea Katibu Mkuu Jumuiya ya Madola Mhe. Patricia Scotland alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume, Zanzibar  

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akimkaribisha Katibu Mkuu Jumuiya ya Madola Mhe. Patricia Scotland alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume, Zanzibar  

Katibu Mkuu Jumuiya ya Madola Mhe. Patricia Scotland akizungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume, Zanzibar 

Mazungumzo baina ya Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk na Katibu Mkuu Jumuiya ya Madola Mhe. Patricia Scotland yakiendelea katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume, Zanzibar 





Wednesday, May 4, 2022

SHEHENA YA KWANZA YA PARACHICHI KUTOKA TANZANIA YAWASILI NCHINI INDIA

Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Anisa Mbega leo tarehe 04 Mei 2022 amepokea kwa mara ya kwanza shehena ya matunda aina ya Parachichi kutoka Tanzania ikiwa ni mwendelezo wa juhudi za Ubalozi huo za kutafuta masoko ya bidhaa za mazao ya mbogamboga na matunda nchini India.

 

Akizungumza na Naibu Mwenyekiti wa Bandari ya Jawalarlal Nehru ya mjini Mumbai, Bw. Unmesh Sharad Wagh mara baada ya kupokea shehena hiyo, Balozi Mbega ameishukuru Serikali ya India kwa kuendelea kushirikiana na Tanzania kwenye sekta mbalimbali ikiwemo Kilimo na kwa pamoja na Bw. Wagh walikubaliana kushirikiana katika sekta ya uchukuzi hususan katika kubadilishana ujuzi kwenye masuala ya Bandari.

 

Katika maelezo yake Balozi Mbega amesema kuwa, wafanyabiashara wa India wamehamasika kutokana na juhudi za uhamasishaji zinazofanywa nchini humo na Ubalozi kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa hapa nchini na sasa wapo tayari kuanza kuingiza matunda aina ya Nanasi na Embe kutoka Tanzania.

 

“Huu ni mwendelezo wa juhudi za Ubalozi kwa kushirikiana na Serikali na TAHA wa kuendelea kutafuta masoko ya bidhaa za mazao ya mbogamboga na matunda nchini India. Wafanyabiashara wa India wamehamasika na sasa wanakamilisha taratibu za kuanza kuingiza nanasi na embe za Tanzania nchini India, amesema Balozi Mbega.  

 

Pia, Balozi Mbega amekishukuru Chama cha Wakulima wa Mbogamboga na Matunda Tanzania (TAHA) kwa ushirikiano wao uliofanikisha shehena hiyo ya Parachihci kuwasili India salama.

 

Shehena hiyo ya kwanza ya parachichi  imewasili nchini India kupitia Bandari yaJawalar Nehru ya mjini Mumbai kwa ushirikiano kati ya Kampuni ya IG Fruits ya India na Kampuni ya Avoafrica ya Makambako mkoani Iringa.

Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Anisa Mbega (kushoto mwenye miwani myeusi) akikata utepe wakati wa mapokezi rasmi ya Kontena lenye matunda aina ya Parachcihi kutoka Tanzania lililowasili nchini humo tarehe 04 Mei 2022 kupitia Bandari ya Jawalar Nehru ya mjini Mumbai. Kontena hilo la Parachichi limewasili nchini humo kwa ushirikiano kati ya Kampuni ya IG Fruits ya India na Kampuni ya Avoafri ya Makambako mkoani Iringa. 

Balozi Anisa (Katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa bandari ya Mumbai baada ya kupokea na kufungua Kontena lenye Parachichi kutoka Tanzania
Picha ya pamoja
Balozi Anisa akiwa kwenye mazungumzo na Naibu Mwenyekiti wa Bandari ya Jawaharlal Nehru ya Mumbai, Bw. Unmesh Sharad Wagh baada ya kupokea matunda hayo ya parachichi  kutoka Tanzania. Katika mazungumzao yao walikubaliana kushirikiana katika kubadilishana ujuzi kati ya Tanzania na India kwenye masuala ya Bandari 

 

Monday, May 2, 2022

WAZIRI MULAMULA AFANYA MAZUNGUMZO NA NAIBU WA USALAMA WA TAIFA WA INDIA


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula amefanya mazungumzo na Naibu Mshauri wa Usalama wa Taifa wa India Mhe. Vikram Misri jijini Dar es Salaam. 


Mazungumzo yao yalijikita kujalidi masuala mbalimbali kuhusu ulinzi na usalama katika ngazi ya Kitaifa, Kanda na Kimataifa kama vile changamato za wahamiaji haramu, ushafirishaji haramu wa binadamu, ugaidi na uharamia. 

Waziri Mulamula amemweleza Mhe. Misri kuwa hali ya usalama ndani ya nchi na kwenye mipaka ya nchi yetu ni salama na tumekuwa tukiendelea kushirikiana vizuri na nchi jirani zinazotuzunguka na Jumuiya za kikanda katika kutatua changamoto mbalimbali kama vile usafirishaji haramu wa binadamu, uharamia na masuala ya ugaidi. 

Naibu Mshauri wa Usalama wa Taifa wa India Mheshimiwa Balozi Vikram kwa upande wake ameeleza kuridhishwa kwake na namna Serikali ya Tanzania inavyoshiriki kutatua na kukabiliana na changamoto za ulinzi na usalama katika ngazi ya Taifa, Kikanda na Kimataifa. Vilevile aliongeza kusema kuwa Serikali ya India itaendelea kushirikiana na Tanzania katika eneo la ulinzi na usalama.

Naibu Mshauri wa Usalama wa Taifa wa India H.E Amb. Vikram Misri yupo nchini kwa ziara ya kikazi ambapo anatarajia kuonana na viongozi mbalimbali wa Serikali.
Mazungumzo yakiendelea
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiwa katika mazungumzo na Naibu Mshauri wa Usalama wa Taifa wa India Mhe. Vikram Misri yaliyofanyika jijini Dar es Salaam. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula Naibu Mshauri wa Usalama wa Taifa wa India Mhe. Vikram Misri wakiwa katika picha ya pamoja na ujumbe kutoka India na Watendaji wa Wizara
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula na Naibu Mshauri wa Usalama wa Taifa wa India Mhe. Vikram Misri wakisalimiana walikutana kwa mazungumzo jijini Dar es Salaam

Sunday, May 1, 2022

WAFANYAKAZI WA WIZARA YA MAMBO YA NJE WALIVYOSHIRIKI MEI MOSI JIJINI DODOMA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) yaliyofanyika kitaifa kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma tarehe 01 Mei 2022

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi zawadi ya Shilingi milioni tatu, Bi. Pamela Yegela, Msaidizi wa Mtendaji Mkuu ambaye ni Mfanyakazi Hodari wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa mwaka 2022

Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiingia kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma kwa furaha wakati wa maadhimisho ya kitaifa ya Siku ya Wafanyakazi Duniani.
Sehemu ya Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwa kwenye maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani
Sehemu nyingine ya Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani
Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwenye maadhimisho ya Mei Mosi jijiji Dodoma

Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwa na nyuso za furaha kuadhimisha siku ya Wafanyakazi Duniani 
Sehemu nyingine ya Wafanayakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani
Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani
Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa maadhimisho ya Mei Mosi yaliyofanyika kitaifa jijini Dodoma

 
x

Thursday, April 28, 2022

MAMLAKA YA MJI WA BUSAN KUSAIDIA KUENDELEZA UCHUMI WA BLUU NCHINI

Mamlaka ya mji wa Busan imeonesha utayari wa kuisadia Tanzania katika kuendeleza uchumi wa buluu na uvuvi.

Haya yamejili wakati wa mazumgumzo yaliyofanyika baina ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula na Mstahiki Meya Mhe. Park Heong Joon alipomtembelea ofisini kwake katika Mji wa Busan, Jamhuri ya Korea. 

Katika mazungumzo hayo Mhe. Park ameeleza kuwa mamlaka ya Mji wake imekuwa ikifuatilia kwa ukaribu juhudi zinazofanywa na Serikali ya Tanzania katika kuendeleza uchumi wa buluu na uvuvi na hivyo wameona ni wakati muafaka kwao wa kushirikiana na kuisaidia Serikali katika kuendeleza sekta hiyo. Mhe. Park aliainisha baadhi ya maeneo ambayo wanakusudia kusaidia ili kuiinua sekta hiyo ikiwemo kutoa nafasi za mafunzo kwa vitendo kwa wadau na wataalam wa sekta ya uchumi wa buluu na vifaa vya kisasa vya uvuvi. 

“Kwa muda mrefu tumekuwa tukifuatilia na kuvutiwa na jitihada zinazofanywa na Serikali ya Tanzania katika kuendeleza sekta ya uchumi wa bluu na uvuvi, tupotayari kutoa mchango wetu katika kuendeleza sekta hii muhimu kwa maendeleo ya wananchi na Serikali ya Tanzania” alisema Mstahiki Meya Mheshimiwa Park.

Kwa upande wake Waziri Mulamula alieleza kuwa Serikali ya Tanzania inatambua mafanikio makubwa ambayo Mamlaka ya mji wa Busan imeyapata kutokana na jitihada zao za kuendeleza sekta ya uchumi wa bluu, hivyo imekuwa ni nafasi hadhimu kwa Tanzania kupata fursa ya kushirikiana na kusaidiwa na mamlaka ya mji huo katika kundeleza uchumi wa buluu na uvuvi. 

“Kwa miaka 30 sasa tumeendelea kufurahia na kunufaika na matunda ya uhusiano mzuri wa kidiplomasia, leo hii ninayofuraha kubwa kuona uhusiano huu unafungua mlango mwingine mpya wa ushirikiano ambao utaleta manufaa makuwa kwa wananchi na Serikali yetu, nafurahi zaidi kuona hili linafanyika baina yetu na mamlaka ya Mji wa Busia ambao umepiga hatua kubwa katika sekta hii, kitu ambacho kinanipa matumaini kuwa tukitumia vyema uzoefu na maarifa tutakayopata kutoka kwenu tutapiga hatua kubwa ya maendeleo ndani ya muda mfupi” alieleza Balozi Mulamula. 

Sambamba na hayo Mstahiki Meya alieleza nia yake kushirikiana na Tanzania katika maeneo mengine mbalimbali ya kiuchumi na kijamii. Miongoni mwa vitu alivyovitaja katika maeneo hayo ni pamoja na kununua zao la kahawa ya Tanzania, kuanzisha ushirikiano na urafiki na mji mojawapo wa Tanzania, kuhimiza makampuni na wafanyabiashara wa Mji wake kuwekeza Tanzania na ushirikiano katika Utamaduni na Sanaa. 

Wakati huohuo, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula amekutana na kufanya mazungumzo na wafanyabiashara wa mji wa Busan, Korea. 

Mazungumzo hayo yamefanyika sambamba na kongamano la biashara lililoandaliwa na Ubalozi wa Tanzania kwa kushirikiana na mamlaka ya Mji huo. Kongamano hilo lililenga kutangaza fursa mbalimbali za uwekezaji na vivutio vya utalii vilivyopo nchini kwa wafanyabiasha hao.

Akizungumza na wafanyabiashara hao Waziri Mulamula amewashawishi kuja nchini kuwekeza kwenye fursa zinazotokana na uchumi wa buluu, ambapo amewaeleza kuwa Tanzania ni sehemu salama kwa uwekezaji wao, vilevile, utashi na utayari wa kisiasa katika masuala ya uwekezaji kwa sasa umekuwa wa hali ya juu kuliko wakati mwingine wowote. Aliongeza kusema Serikali imefanya maboresho muhimu ya sera, sheria na kanuni za uwekezaji. 

“Tanzania tupo tayari na tunashauku kubwa ya kufanyakazi na sekta binafsi ya Busan katika kuendeleza sekta yetu ya uchumi wa buluu ambayo bado ipo chini kimaendeleo” Waziri Mulamula. 

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wafanyabiashara hao wameonesha kuvutiwa na fursa walizoelezwa kupatikana katika sekta ya uchumi wa buluu na wameeleza nia na utayari wao wa kuwekeza katika sekta hiyo hapa nchini.

Katika tukio jingine Waziri Mulamula amekutana na kufanyamazungumzo na Mwenyekiti na Rais wa Eximbank ya Korea Bw. Moon Kyu, Bang katika Makao Makuu ya Benki hiyo jijini Seoul, Korea.  

Waziri Mulamula yupo nchini Korea kwa ziara ya siku tano (5) kufuatia mwaliko wa Waziri wa Mambo ya Nje wanchi hiyo Mhe. Chung Eui-yong. Vilevile Waziri Mulamula atashiriki hafla ya maadhimisho ya miaka 30 ya uhusiano wa Kidiplomasia kati ya Tanzania na Jamhuri ya Korea itayofanyika jijini Seoul tarehe 29 Aprili 2022. Tanzania na Korea zilianzisha uhusiano wa Kidiplomasia Aprili 29,1992.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akipokelewa na mwenyeji wake Mstahiki Meya wa Mji wa Busan Mhe. Park Heong Joon alipowasili ofisini kwake. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akiwa katika mazunguzo na Mstahiki Meya wa Mji wa Busan, Korea Mhe. Park Heong Joon alipomtembelea ofisini kwake.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula na Mstahiki Meya wa Mji wa Busan, Korea Mhe. Park Heong Joon wakifurahia jambo walipokutana kwa mazungumzo 
Mazungumzo yakiendelea
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula na Mstahiki Meya wa Mji wa Busan, Korea Mhe. Park Heong Joon wakiwa katika picha ya pamoja na watendaji wa Serikali ya Tanzania na Mji wa Busan.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.Balozi Liberata Mulamula akiwa katika mazungumzo na Rais wa Eximbank ya Korea Bw. Moon Kyu, Bang (wakwanza kulia) alipotembelea Makao Makuu ya Benki hiyo jijini Seoul. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.Balozi Liberata Mulamula na Rais wa Eximbank ya Korea Bw. Moon Kyu, Bang (wapili kushoto) wakiwa katika picha. Wengine ni Balozi wa Tanzania nchini Korea Mhe. Togolani Mavula (wapili kulia) Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia Balozi Caesar Waitara na baadhi ya watendaji wa benki hiyo. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.Balozi Liberata akimkabithi picha ya wanyama wa mbugani (yakuchorwa) Mstahiki Meya wa Mji wa Busan, Korea Mhe. Park Heong Joon

Wednesday, April 27, 2022

WIZARA YA MAMBO YA NJE YAJIPANGA KUWAJENGEA UWEZO WATUMISHI WAKE

Na Waandishi wetu, Dodoma

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imejipanga kuwajengea uwezo wa kazi watumishi wake ili kuwawezesha kutekeleza kwa vitendo Diplomasia ya Uchumi.


Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Balozi Joseph Sokoine wakati akifungua Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo uliofanyika leo Jijini Dodoma


“Tumekuwa na kikao cha Baraza la Wafanyakazi kama ilivyo kwa mujibu wa Sheria, kikao kilijadili pamoja na mambo mengine, bajeti ya Wizara kwa mwaka mpya wa fedha 2022/2023, kuboresha utendaji kazi wa Wizara pamoja na maslahi ya watumishi.


“Katika masuala tuliyojadili leo katika kuboresja maslahi ya wafanyakazi ni pamoja na eneo la mafunzo ili kuendelea kuwajengeauwezo watumishi wetu wa kutekeleza majukumu yao ikiwa ni pamoja na utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi kwa vitendo,” amesema Balozi Sokoine  


Kwa upande wake Katibu wa TUGHE ngazi ya Taifa, Bw. Amani Msuya ameupongeza uongozi wa Wizara kwa kuyapa kipaumbele maslahi ya watumishi na kuwataka Watumishi kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa bidii na maarifa yote kwa maslahi mapana ya Taifa.


Naye Mwenyekiti wa TUGHE wa tawi la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Pilly Sukwa amesema kuwa kikao cha baraza kimejadili masuala ya Bajeti pamoja umuhimu wa kuboresha zaidi maslahi ya watumishi wa Wizara ili kuwaongezea morali ya kazi wakati wa utekelezaji wa majukumu yao kwa tija na ufanisi zaidi.


“Katika eneo langu mimi kama mwenyekiti wa TUGHE hapa Wizarani ni kuhakikisha kuwa maslahi ya watumishi ikiwemo mishahara na maslahi mengine yamezingatiwa. Ninaishukuru Wizara mambo yote haya yamezingatiwa wakati wa mkutano huu wa Baraza,” amesema Bi. Sukwa.


Baraza la Wafanyakazi wa Wizara limefanyika kwa lengo kupokea na kujadili Taarifa ya Utekelezaji wa Bajeti ya Wizara kwa Mwaka 2021/2022 na Makadirio ya Makisio ya Bajeti kwa Mwaka 2022/2023.


Kikao hicho pia kimehudhuriwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Mohammed Rajab na Wakuu wa Idara na Vitengo wa Wizara hiyo.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara, Balozi Joseph Sokoine akizungumza wakati wa kufungua Mkutano wa Baraza hilo uliofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa St. Gasper jijini Dodoma tarehe 27 Aprili 2022. Pamoja na mambo mengine Mkutano huo ulipokea na kujadili Taarifa ya Utekelezaji wa Bajeti ya Mwaka 2021/2022 na Makadirio ya Makisio ya Bajeti ya Mwaka 2022/2023.
Balozi Sokoine (katikati) akifungua mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Kushoto kwa Balozi Sokoine ni  Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Mohammed Rajab akifuatiwa na Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,  Bw. Alex Mfungo. Wa kwanza kushoto ni Mwenyekiti wa TUGHE Tawi la Wizara, Bi. Pilly Sukwa akifuatiwa na Katibu wa TUGHE, Bw. Hassan Mnondwa.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Mohammed Rajab naye akizungumza wakati wa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara.
Sehemu ya Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakishiriki mkutano huo. Kutoka kulia ni Bw. Japhary Kachenje, Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Wizara, Balozi Caroline Chipeta, Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma za Sheria cha Wizara, Bw. Swalehe Chondoma, Mhasibu Mkuu wa Wizara na Balozi Agnes Kayola, Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda.
Mwenyekiti wa TUGHE Tawi la  Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Pilly Sukwa akizungumza wakati wa Mkutano huo wa Baraza la Wafanyakazi
Katibu wa TUGHE ngazi ya Taifa, Bw. Amani Msuya naye akichangia jambo wakati wa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Sokoine (katikati walioketi) akiwa katika picha  na Ssehemu ya Wajumbe wa Baraza hilo
Picha ya pamoja  
Picha ya pamoja
Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Justine Kisoka akiwasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa Bajeti ya Wizara ya Mwaka 2021/2022 na Makadirio ya Makisio ya Bajeti ya Mwaka 2022/2023 kwa wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi
Mjumbe wa Baraza ambaye pia ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Diplomasia ya Uchumi, Bw. Magabilo Murobi akichangia jambo wakati wa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi
Mjumbe wa Baraza la Wafanyakazi, Bw. Abel Maganya naye akichangia hoja wakati wa mkutano wa Baraza la Wafanyakazi.