Thursday, July 4, 2024

RAIS NYUSI AKUTANA NA DKT. MWINYI ZANZİBAR

Rais wa Jamhuri ya Msumbiji Mheshimiwa Filipe Nyusi amekutana na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi Ikulu Zanzibar

Akizungumza na Dkt. Mwinyi Mheshimiwa Nyusi alitumia nafasi hiyo kumuaga kwa kuwa amemaliza kipindi chake cha uongozi nchini Msumbiji na kumshukuru kwa Ushirikiano aliompatia alipokuwa Waziri wa Ulinzi wa Tanzania.

Amemuahidi kuwa Msumbiji itaendelea kudumisha uhusiano na ushirikiano wake na Tanzania haşa ikizingatiwa historia ya uhusiano uliopo kati ya Tanzania na Msumbiji

Naye Mhe. Dkt. Mwinyi amemshukuru Mhe. Nyusi kwa kumtembelea Zanzibar na kumkaribisha kutembelea Zanzibar wakati mwingine.

Mheshimiwa Nyusi alikuwa nchini kwa ziara ya kitaifa kuanzia tarehe Mosi Julai 2024

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi akimpokea Rais wa Jamhuri ya Msumbiji Mheshimiwa Filipe Nyusi alipowasili Ikulu Zanzibar

 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Rais wa Jamhuri ya Msumbiji Mheshimiwa Filipe Nyusi alipowasili Ikulu Zanzibar

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi akiwa na Rais wa Jamhuri ya Msumbiji Mheshimiwa Filipe Nyusi alipowasili Ikulu Zanzibar

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi akiwa na Rais wa Jamhuri ya Msumbiji Mheshimiwa Filipe Nyusi alipomtembelea Ikulu Zanzibar

 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi na ujumbe wake akizungumza na Rais wa Jamhuri ya Msumbiji Mheshimiwa Filipe Nyusi alipomtembelea  Ikulu Zanzibar
Rais wa Jamhuri ya Msumbiji Mheshimiwa Filipe Nyusi akizungumza alipomtembelea Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani)  Ikulu Zanzibar

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi akimkabidhi zawadi ya Picha   Rais wa Jamhuri ya Msumbiji Mheshimiwa Filipe Nyusi   alipomtembelea  Ikulu Zanzibar
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi akiwa na Rais wa Jamhuri ya Msumbiji Mheshimiwa Filipe Nyusi katika picha ya pamoja  alipomtembelea  Ikulu Zanzibar

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.