Friday, July 26, 2024

BALOZI KOMBO NA MANAIBU WAKE WAPOKELEWA KATIKA OFİSİ NDOGO ZA WIZARA DSM

 


 

 





















 

 

 

 

 

 



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo amewasili na kupokelewa katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam akitokea Ikulu ya Dar es Salaam baada ya kuapishwa kuwa Waziri na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Katika mpokezi hayo, Mhe. Balozi Kombo aliiambatana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Cosato Chumi na Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Mhe. Dennis Lazaro Londo na kulakiwa kwa bashasha na viongozi na Watumishi wa Wizara waliokusanyika katika Ofisi ndogo, Dar Es Salaam.


Mhe. Balozi Kombo pamoja na Naibu Mawaziri, Mhe. Londo na Mhe. Chumi waliteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kushika nyadhifa hizo katika mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri yaliyofanyika Julai 21, 2024

 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.