Wednesday, July 10, 2024

WAZIRI BYABATO AIPONGEZA BURUNDI KWA KUDUMISHA AMANI NA USALAMA

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayesimamia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato na Balozi wa Burundi nchini Tanzania Mhe. Leontine Nzeyimana katika picha ya pamoja alipowasili kwenye hafla ya maadhimisho ya miaka 62 ya Uhuru wa Jamhuri ya Burundi iliyofanyika jijini Dar es Salaam

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayesimamia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato amepoingeza Jamhuri ya Burundi kwa kuendelea kulinda na kudumisha amani na usalama nchini humo.

Naibu Waziri Byabato amasema hayo alipokuwa akihutubia Jumuiya ya Wadiplomasia na wageni wengine waalikwa kwenye hafla ya maadhimisho ya miaka 62 ya Uhuru wa Jamhuri ya Burundi iliyofanyika jijini Dar es Salaam. Vilevile alibainisha kuwa katika kipindi hicho cha miaka 62 dunia imeshuhudi Taifa hilo likipiga hatua muhimu ya maendeleo katika nyanja mbalimbali ikiwemo siasa na uchumi. 

“Hakika mtakubaliana nami kuwa katika kipindi cha miaka 62, Burundi imefanikiwa kwa kiasi kikubwa katika nyanja za kisiasa na kiuchumi. Mathalani, kisiasa tangu kusainiwa kwa Mkataba wa Amani hapa jijini Dar es Salaam mwaka 2006, Burundi imeweza kudumisha amani na usalama nchini kote pamoja na kukuza demokrasia na utawala bora” Alieleza Naibu Waziri Byabato

Mbali na hayo Waziri Byabato aliongeza kuwa Tanzania na Burundi zimeendelea kuwa na ushirikiano wa karibu wakati wote, ukichagizwa na mkaba uliosaniwa mwaka 1975 wa uanzishaji wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ambao ulifungua ushirikiano katika sekta mbalimbali za kimkakati ikiwemo elimu, afya, kilimo, biashara na uwekezaji, utalii,nishati, usafirishaji, ulinzi na usalama na masuala ya uhamiaji. 

Kwa upande wake Balozi wa Burundi nchini Tanzania Mhe. Leontine Nzeyimana alieleza kuwa katika kipindi cha miaka 62 ya uhuru, Taifa hilo linajivunia kuendelea kudumisha uhusiano mzuri wa kidiplomasia na Mataifa mbalimbali duniani na nchi jirani katika Kanda ya Afrika Mashariki.

Balozi Nzeyimana aliendelea kubainisha kuwa katika nyanja ya uchumi Burundi inaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo ikiwemo Tanzania, ambapo mradi wa SGR unatarajiwa kuliunganisha Taifa hilo na Bandari ya Dar es Salaam hivyo kutoa mchango mkubwa katika kurahishisha na kuongeza biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na Burundi. 

Takwimu zinaonyesha kuwa biashara kati ya Tanzania na Burundi inaendelea kukua ambapo ilifikia dola milioni 212.8 mwaka 2022/2023 kutoka dola 61.3 milioni mwaka 2017/2018. Huku takriban asilimia 95 ya mizigo ya Burundi ikipitia Bandari ya Dar es Salaam. 

Tanzania na Burundi zinashirikiana kwa karibu katika ngazi za kikanda na kimataifa ikiwemo EAC, ICGRL, AU, UN, Jumuiya ya Nchi zisizofungamana na Siasa za Upande wowote (NAM). 

Aidha Naibu Waziri Byabato alisisitiza dhamira ya Serikali ya Tanzania ya kuendelea kufanya kazi kwa karibu na Serikali ya Burundi ili kuimarisha zaidi uhusiano kwa manufaa ya pande zote mbili na watu wake. Vile vile, kuendelea kuwa mshirika wa wakati wote na wa kuaminika wa Burundi kwenye masuala ya kikanda na kimataifa.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayesimamia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato akihutubia wageni waalikwa kwenye hafla ya maadhimisho ya miaka 62 ya Uhuru wa Jamhuri ya Burundi iliyofanyika jijini Dar es Salaam
Picha ya pamoja
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayesimamia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato akifurahia jambo na baadhi ya wageni waalikwa kwenye hafla ya maadhimisho ya miaka 62 ya Uhuru wa Jamhuri ya Burundi iliyofanyika jijini Dar es Salaam
Balozi wa Burundi nchini Tanzania Mhe. Leontine Nzeyimana akihutubia kwenye hafla ya maadhimisho ya miaka 62 ya Uhuru wa Jamhuri ya Burundi iliyofanyika jijini Dar es Salaam
Sehemu ya wageni waalikwa wakifuatilia matukio kwenye hafla ya maadhimisho ya miaka 62 ya Uhuru wa Jamhuri ya Burundi iliyofanyika jijini Dar es Salaam

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.