Thursday, July 25, 2024

DKT. TULIA AMUAPISHA BALOZI MAHMOUD THABIT KOMBO KUWA MBUNGE

 




 







 

 

 

 




Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Akson amemuapisha Balozi Dkt. Mahmoud Thabit Kombo kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika hafla ndogo iliyofanyika Ofisi Ndogo za Bunge jijini Dar es Salaam tarehe 25 Julai,2024.

Hafla hiyo ya uapisho imehudhuriwa na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Stergomena Tax, Naibu Waziri Mteule wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Dennis Lazaro Londo, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Samwel Shelukindo, Naibu Katibu Mkuu Balozi Said Shaib Mussa na watendaji wengine wa Ofisi ya Bunge.

Tarehe 21 Julai, 2024 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan alimteua Balozi Dkt. Mahmoud Thabit Kombo kuwa Mbunge na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. 

Mhe. Rais pia aliwateua Mhe. Dennis Lazaro Londo (Mb) kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki na Mhe. Cosato David Chumi (Mb) kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje. Waziri.

 Mhe. Balozi Kombo na Manaibu Waziri wateule wataapishwa tarehe 26 Julai, 2024 Ikulu jijini Dar es salaam.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.