Saturday, July 27, 2024

WAZIRI KOMBO AANZA KAZI RASMI












Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.) ameanza kazi rasmi katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.

Mhe. Kombo ameanza majukumu hayo muda mfupi baada ya makabidhiano ya ofisi na aliyekuwa Waziri Mhe. January Makamba (Mb).

Makabidhiano hayo yalihudhuriwa pia na Naibu Mawaziri ambao waliteuliwa pamoja, Mhe. Cosato Chumi na Mhe. Dennis Londo

Mhe. Waziri katika siku yake ya kwanza amekutana na kufanya mazungumzo na Mgombea wa nafasi ya Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Kanda ya Afrika, Mhe. Dkt. Faustine Ndungulile.

Aidha, Mhe. Waziri amekutana na baadhi ya Wakurugenzi waliopo jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kutekeleza majukumu

mbalimbali ambapo amepoeka taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya Wizara.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.