Wednesday, April 27, 2022

WIZARA YA MAMBO YA NJE YAJIPANGA KUWAJENGEA UWEZO WATUMISHI WAKE

Na Waandishi wetu, Dodoma

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imejipanga kuwajengea uwezo wa kazi watumishi wake ili kuwawezesha kutekeleza kwa vitendo Diplomasia ya Uchumi.


Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Balozi Joseph Sokoine wakati akifungua Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo uliofanyika leo Jijini Dodoma


“Tumekuwa na kikao cha Baraza la Wafanyakazi kama ilivyo kwa mujibu wa Sheria, kikao kilijadili pamoja na mambo mengine, bajeti ya Wizara kwa mwaka mpya wa fedha 2022/2023, kuboresha utendaji kazi wa Wizara pamoja na maslahi ya watumishi.


“Katika masuala tuliyojadili leo katika kuboresja maslahi ya wafanyakazi ni pamoja na eneo la mafunzo ili kuendelea kuwajengeauwezo watumishi wetu wa kutekeleza majukumu yao ikiwa ni pamoja na utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi kwa vitendo,” amesema Balozi Sokoine  


Kwa upande wake Katibu wa TUGHE ngazi ya Taifa, Bw. Amani Msuya ameupongeza uongozi wa Wizara kwa kuyapa kipaumbele maslahi ya watumishi na kuwataka Watumishi kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa bidii na maarifa yote kwa maslahi mapana ya Taifa.


Naye Mwenyekiti wa TUGHE wa tawi la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Pilly Sukwa amesema kuwa kikao cha baraza kimejadili masuala ya Bajeti pamoja umuhimu wa kuboresha zaidi maslahi ya watumishi wa Wizara ili kuwaongezea morali ya kazi wakati wa utekelezaji wa majukumu yao kwa tija na ufanisi zaidi.


“Katika eneo langu mimi kama mwenyekiti wa TUGHE hapa Wizarani ni kuhakikisha kuwa maslahi ya watumishi ikiwemo mishahara na maslahi mengine yamezingatiwa. Ninaishukuru Wizara mambo yote haya yamezingatiwa wakati wa mkutano huu wa Baraza,” amesema Bi. Sukwa.


Baraza la Wafanyakazi wa Wizara limefanyika kwa lengo kupokea na kujadili Taarifa ya Utekelezaji wa Bajeti ya Wizara kwa Mwaka 2021/2022 na Makadirio ya Makisio ya Bajeti kwa Mwaka 2022/2023.


Kikao hicho pia kimehudhuriwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Mohammed Rajab na Wakuu wa Idara na Vitengo wa Wizara hiyo.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara, Balozi Joseph Sokoine akizungumza wakati wa kufungua Mkutano wa Baraza hilo uliofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa St. Gasper jijini Dodoma tarehe 27 Aprili 2022. Pamoja na mambo mengine Mkutano huo ulipokea na kujadili Taarifa ya Utekelezaji wa Bajeti ya Mwaka 2021/2022 na Makadirio ya Makisio ya Bajeti ya Mwaka 2022/2023.
Balozi Sokoine (katikati) akifungua mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Kushoto kwa Balozi Sokoine ni  Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Mohammed Rajab akifuatiwa na Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,  Bw. Alex Mfungo. Wa kwanza kushoto ni Mwenyekiti wa TUGHE Tawi la Wizara, Bi. Pilly Sukwa akifuatiwa na Katibu wa TUGHE, Bw. Hassan Mnondwa.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Mohammed Rajab naye akizungumza wakati wa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara.
Sehemu ya Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakishiriki mkutano huo. Kutoka kulia ni Bw. Japhary Kachenje, Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Wizara, Balozi Caroline Chipeta, Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma za Sheria cha Wizara, Bw. Swalehe Chondoma, Mhasibu Mkuu wa Wizara na Balozi Agnes Kayola, Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda.
Mwenyekiti wa TUGHE Tawi la  Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Pilly Sukwa akizungumza wakati wa Mkutano huo wa Baraza la Wafanyakazi
Katibu wa TUGHE ngazi ya Taifa, Bw. Amani Msuya naye akichangia jambo wakati wa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Sokoine (katikati walioketi) akiwa katika picha  na Ssehemu ya Wajumbe wa Baraza hilo
Picha ya pamoja  
Picha ya pamoja
Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Justine Kisoka akiwasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa Bajeti ya Wizara ya Mwaka 2021/2022 na Makadirio ya Makisio ya Bajeti ya Mwaka 2022/2023 kwa wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi
Mjumbe wa Baraza ambaye pia ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Diplomasia ya Uchumi, Bw. Magabilo Murobi akichangia jambo wakati wa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi
Mjumbe wa Baraza la Wafanyakazi, Bw. Abel Maganya naye akichangia hoja wakati wa mkutano wa Baraza la Wafanyakazi.

 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.