Tuesday, April 26, 2022

JAMHURI YA KOREA YAAHIDI KUENDELEA KUSAIDIA MIRADI YA MAENDELEO NCHINI


Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Korea Mhe. Chung Eui-yong ameelezea kuwa Serikali ya nchi hiyo itaendelea kushirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kutekeleza miradi mbalimbali ya kimaendeleo ikiwemo ujenzi wa barabara na reli, usafiri wa majini, kuendeleza kilimo, uchumi wa buluu, uvuvi katika bahari kuu na teknolojia ya habari na mwasiliano.

Waziri Chung ameeleza haya alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Masahriki Mhe. Balozi Liberata Mulamula ambaye yupo ziarani nchini Korea. 

Vilevile, Waziri Mulamula na Mwenyeji wake Mhe.Chung Eui-yong katika mazungumzo yao wamejadili kuhusu kuendelea kudumisha uhusiano mzuri wa kidiplomasia uliopo baina ya mataifa hayo rafiki. Vilevile wamekubaliana kuendelea kuibua maeneo mapya ya ushirikiano wa kiuchumi na kijamii kwa manufaa ya pande zote mbili. 

Waziri Mulamula akiwa nchini humo anatarijia atashiriki sherehe za maadhimisho ya miaka 30 ya uhusiano wa Kidiplomasia kati ya Tanzania na Jamhuri ya Korea yatakayofanyika jijini Seoul tarehe 29 Aprili 2022. Tanzania na Korea zilianzisha uhusiano wa Kidiplomasia Aprili 29,1992. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.Balozi Liberata na Rais wa Shirika la Maendeleo la Korea (KOICA) Dkt. Sohn Hyuk-Sang wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watendaji wa Shirika hilo (kulia) na ujumbe wa Tanzania (kushoto)
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.Balozi Liberata akiwa katika mazungumzo na Rais wa Shirika la Maendeleo la Korea (KOICA) Dkt. Sohn Hyuk-Sang (wakwanza kulia) yaliyofanyika jijini Seoul, Korea.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata akimkabithi picha ya wanyama wa mbugani (yakuchorwa) Katibu Mkuu Mstaafu wa Umoja wa Mataifa Mhe. Ban Ki-moon wakiwa katika mazungumzo alipomtembelea ofisini kwake jijini Seoul, Korea.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Korea Mhe. Chung Eui-yong akimsikiliza Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula walipokutana kwa mazungumzo jijini Seoul, Korea.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata na Katibu Mkuu Mstaafu wa Umoja wa Mataifa Mhe. Ban Ki-moon wakiwa katika mazungumzo alipomtembelea ofisini kwake jijini Seoul, Korea.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula na Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Korea Mhe. Chung Eui-yong wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika jijini Seoul, Korea
Balozi wa Tanzania nchini Korea Mhe.Togolani Mavula akifuatilia mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea
Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Caesar Waitara akifuatilia mazungumzo yaliyokuwa yakiendelea
Mazungumzo yakiendelea
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akiwa katika mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Korea Mhe. Chung Eui-yong alipomtembelea ofisini kwake jijini Seoul, Korea. 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.