Monday, April 4, 2022

WAZIRI MULAMULA AFANYA MAZUNGUMZO NA WABUNGE WA EALA


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula na Naibu Waziri Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk leo tarehe 4 Aprili 2022 wamekutana na kufanya mazungumzo na Wabuge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA) wa Tanzania yaliyofanyika katika Makao Makuu ya Wizara jijini Dodoma.

Akizungumza na Wabunge hao Waziri Mulamula amewapongeza kwa kazi nzuri wanayoendelea kuifanya kupitia chombo hicho muhimu katika Jumuiya, ya kuhakikisha Jumuiya inaendelea kustawi zaidi. Vilevile, Waziri Mulamula ametoa wito kwa wabunge hao kuendele kuwa wamoja katika kutetea, kufuatilia na kulinda maslahi ya Taifa na Jumuiya kwa ujumla. 

Wabunge hao ambao walifanya ziara ya kikazi Wizarani wameeleza kuridhishwa na ushirikiano wanaoupata kutoka kwa Viongozi na Watendaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki katika utekelezaji wa majukumu yao. Aidha,kupitia Wizara wameipongeza Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuwasilisha kwa wakati ada ya unachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. 

Ziara hiyo ililenga kubadilishana mawazo na uzoefu baina yao na Viongozi wa Wizara sambamba na kutoa mrejesho wa maendeleo ya masuala mbalimbali muhimu yanayoendelea katika Jumuiya.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akielezea jambo wakati wa mazungumzo na Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA) wa Tanzania yaliyofanyika katika Makao Makuu ya Wizara jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akifuatilia mazungumzo na Wabuge wa Bunge la Afrika Mashariki wa Tanzania yaliyofanyika katika Makao Makuu ya Wizara jijini Dodoma.
Mazungumzo yakiendelea
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (wannne kushoto) Naibu Waziri Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (watatu kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na Wabuge wa Bunge la Afrika Mashariki
Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki Mhe. Dr. Abdullah Hasnuu Makame akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo kati ya Wabunge wa EALA, Waziri Mhe. Mulamula na Naibu Waziri Mhe. Mbarouk yaliyofanyika katika Makao Makuu ya Wizara jijini Dodoma.
 Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki Mhe. Adam Kimbisa akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo kati ya Wabunge wa EALA, Waziri Mhe. Mulamula na Naibu Waziri Mhe. Mbarouk yaliyofanyika katika Makao Makuu ya Wizara jijini Dodoma.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.