Monday, April 4, 2022

WAZIRI VICKY FORD AZINDUA MPANGO WA ‘SHULE BORA’ KIBAHA

Na Mwandishi wetu, Dar

Waziri wa Uingereza anayeshughulikia masuala ya Afrika, Amerika ya Kusini na Visiwa vya Karibian Mhe. Vicky Ford amezindua mpango wa elimu unaojulikana kama ‘Shule Bora’ Kibaha mkoani Pwani.

Mhe. Ford amesema mpango wa ‘Shule Bora’ utasaidia kuboresha elimu nchini Tanzania na utawasaidia zaidi ya watoto milioni nne, ambapo nusu yao watakuwa ni watoto wa kike.

“Elimu ni kipaumbele kwa Rais Samia pamoja na Waziri wa Mkuu wa Serikali ya Uingereza……….ni lengo la Serikali ya Uingereza kuisaidia watoto zaidi ya milioni 15 hapa Tanzania kupata elimu, lakini tumeanza na hawa wachache lakini pia tumezingatia usawa wa kijinsia ambapo nusu ya sehemu ya msaada huu utamnufaisha mtoto wa kike,” amesema Mhe. Ford.

Nae Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amesema kuwa msaada wa pound milioni 180 zilizotolewa na Serikali ya Uingereza utasaidi sana kuboresha sekta ya elimu nchini kupitia mpango wa elimu wa 'Shule Bora'.

Prof. Mkenda amesema pamoja na mambo mengine, kuwa msaada wa Serikali ya Uingereza kupitia mpango huu wa elimu utasaidia sana kuboresha mazingira ya elimu nchini ikiwa ni pamoja nan miundombinu ya shule, vitabu na sheria pamoja na mitaala inayotumika kufundishia.

“………….‘Shule Bora’ itaiwezesha Serikali yetu kufanya mapitio ya Sera ya elimu ya 1978, kuboresha Sheria ya Elimu, kuboresha mitaala ya elimu, kuangalia idadi ya walimu pamoja na wakufunzi na wahadhiri,” amesema Prof. Mkenda

Kwa upande wake, Naibu Waziri Ofisi ya Rais – Tamisemi, Mhe. David Silinde amemhakikishia Waziri Ford kuwa fedha zote za mpango wa elimu wa ‘Shule Bora’ zitatumika kama ilivyokusudiwa ili kuwawezesha watoto wa kitanzania kunufaika na elimu.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda akimkaribisha Waziri wa Uingereza anayeshughulikia masuala ya Afrika, Amerika ya Kusini na Visiwa vya Karibian Mhe. Vicky Ford katika viwanja vya shule ya msingi Mkoani ambapo mpango wa elimu wa 'Shule Bora' umezinduliwa 

Waziri wa Uingereza anayeshughulikia masuala ya Afrika, Amerika ya Kusini na Visiwa vya Karibian Mhe. Vicky Ford akiangalia baadhi ya vitu vilivyotengenezwa na watoto wa Shule ya Msingi Mkoani kabla ya uzinduzi wa mopango wa elimu wa 'Shule Bora'

Waziri wa Uingereza anayeshughulikia masuala ya Afrika, Amerika ya Kusini na Visiwa vya Karibian Mhe. Vicky Ford akiangalia baadhi ya vitu vilivyotengenezwa na watoto wa Shule ya Msingi Mkoani kabla ya uzinduzi wa mpango wa elimu wa 'Shule Bora'


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda na Waziri wa Uingereza anayeshughulikia masuala ya Afrika, Amerika ya Kusini na Visiwa vya Karibian Mhe. Vicky Ford wakizindua mpango wa elimu wa 'Shule Bora' 


Waziri wa Uingereza anayeshughulikia masuala ya Afrika, Amerika ya Kusini na Visiwa vya Karibian Mhe. Vicky Ford akiongea na wageni (hawapo pichani) baada ya uzinduzi wa mpango wa 'Shule Bora'





No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.