Thursday, May 5, 2022

BALOZI MBAROUK AMPOKEA KATIBU MKUU JUMUIYA YA MADOLA ZANZIBAR

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk amempokea Katibu Mkuu Jumuiya ya Madola Mhe. Patricia Scotland alipowasili Zanzibar katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume.

Mhe. Scotland yupo nchini kwa ziara maalumu ya kukutana na kumfahamisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan maudhui ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Madola unaotarajiwa kufanyika nchini Rwanda mwezi Juni 2022.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akimpokea Katibu Mkuu Jumuiya ya Madola Mhe. Patricia Scotland alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume, Zanzibar  

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akimkaribisha Katibu Mkuu Jumuiya ya Madola Mhe. Patricia Scotland alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume, Zanzibar  

Katibu Mkuu Jumuiya ya Madola Mhe. Patricia Scotland akizungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume, Zanzibar 

Mazungumzo baina ya Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk na Katibu Mkuu Jumuiya ya Madola Mhe. Patricia Scotland yakiendelea katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume, Zanzibar 





No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.