Thursday, October 22, 2015
Waziri Membe aagana na watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje
Baadhi ya watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa waliohudhuria hafla hiyo |
Waziri Membe akifurahia zawadi iliyotolewa na Wizara ya Mambo ya Nje. |
Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa, Mhe. Begum Karim Taj naye akikabidhi zawadi kwa Mhe. Waziri kwa niaba ya Waheshimiwa Mabalozi wa Tanzania |
Naibu Katibu Mkuu, Balozi Hassan Simba Yahya akipokea zawadi kwa niaba ya Naibu Waziri, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim ambaye hakuweza kuhudhuria hafla hiyo kutokana na majukumu ya kitaifa. |
Balozi Mulamula na Mama Mwakawago wakionesha zawadi ya Mama Mahadhi Juma Maalim. |
Waheshimiwa Mabalozi wanaowakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali, Wakuu wa Idara/Vitengo na watumishi wakishuhudia zoezi la utoaji wa zawadi. |
Waziri Membe akiongea na watumishi wa Wizara wakati wa hafla hiyo. |
Mkuu wa Itifaki, Balozi Juma Maharage akitoa neno la shukrani katika hafla hiyo |
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy naye akiongea machache katika hafla hiyo |
Wakati wa maakuli. Mhe. Waziri akiwa ameshikilia sahani ya chakula na anyemfuatia ni Katibu Mkuu anayeonekana akichota chakula |
Naibu Katibu Mkuu naye anajichotea chakula |
Waheshimiwa Mabalozi nao wanajichotea chakula |
Mhe. Waziri, Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu wakiwa katika picha ya pamoja na Waheshimiwa Mabalozi na Wakuu wa Idara/Vitengo |
Mhe. Waziri, Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu wakiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Idara/Vitengo. |
Mhe. Waziri, Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu wakiwa katika picha ya pamoja na Wasaidizi wa Waziri na Naibu Waziri. |
Mhe. Waziri, Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu wakiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu. |
Mhe. Waziri, Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu wakiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali. |
Mhe. Waziri, Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu wakiwa katika picha ya pamoja na Waheshimiwa Mabalozi Wanawake. |
Balozi Mpya wa Misri awasilisha Nakala za Hati za Utambulisho
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mpya wa Misri, Mhe. Yasser Ahmed Al Eldin Elshawaf |
Waziri Membe akishikana mkono na Balozi mpya wa Misri mara baada ya kupokea Nakala za Hati za Utambulisho. |
Waziri Membe akiangalia na kufurahia zawadi aliyokabidhiwa na Balozi mpya wa Misri |
Waziri Membe akiagana na Balozi mpya wa Misri nara baada ya zoezi la kuwasilisha Nakala za Hati za Utambulisho kukamilika |
Wednesday, October 21, 2015
Waziri Membe akutana na Kiongozi wa Timu ya Waangalizi wa Uchaguzi Mkuu kutoka Umoja wa Afrika.
Kiongozi wa timu ya waangalizi wa Uchaguzi Mkuu kutoka Umoja wa Afrika (AU), ambaye pia ni Rais Mstaafu wa Msumbiji Mhe. Armando Emilio Guebuza akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe ambapo Waziri Membe alimueleza kiongozi huyo hali ya utulivu na amani inavyoendelea katika kipindi chote tangu kuanza kwa kampeni kuelekea siku ya uchaguzi mkuu hapo tarehe 25-10-2015.
Mkurugenzi wa Idara ya Afrika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Samwel William Shelukindo(kushoto) pamoja na baadhi ya wajumbe wa timu hiyo ya waangalizi wa Umoja wa Afrika wakifuatilia mazungumzo hayo.
Kiongozi wa timu ya waangalizi wa Uchaguzi Mkuu kutoka Umoja wa Afrika ambaye pia ni Rais Mstaafu wa Msumbiji Mhe. Armando Emilio Guebuza akisisitiza jambo katika mazungumzo hayo.
Msaidizi wa Waziri Bw. Thobias Makoba (katikati) pamoja na Ofisa wa Wizara ya Nje anayeshughulikia masuala ya Afrika Bi. Zuleha Tambwe wakifuatilia mazungumzo hayo.
Mhe. Membe akifurahia jambo na Mhe. Guebuza mara baada ya kumaliza Mazungumzo yao.
Rais Mstaafu wa Msumbiji na Kiongozi wa timu ya waangalizi wa Uchaguzi Mkuu kutoka Umoja wa Afrika Mhe. Armando Emilio Guebuza, akiagana na Mheshimiwa Membe mara baada ya Mazungumzo hayo.
=================
PICHA NA: REUBEN MCHOME.
Monday, October 19, 2015
Waziri Membe awausia Mabalozi wa Tanzania
Mhe. Membe anaonekana akifurahia zawadi ya ramani inayoonesha mandhari mbalimbali za nchi ya Japan. Zawadi hiyo alikabidhiwa na Balozi wa Tanzania nchini Japan, Mhe. Batilda S. Burian |
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Taarifa zaidi kuhusu Mahujaji kutoka Tanzania waliofariki na kujeruhiwa huko Saudi Arabia
Mahujaji wengine watatu kutoka Tanzania ambao walikuwa hawaonekani tokea ajali ya kukanyagana kwa mahujaji ilipotokea Makkah nchini Saudi Arabia tarehe 24 Septemba 2015 wametambuliwa kuwa, ni miongoni mwa mahujaji waliofariki dunia. Kutambuliwa kwa mahujaji hao kunafanya idadi ya mahujaji wa Tanzania waliopoteza maisha katika ajali hiyo kufikia ishirini na tano (25). Majina kamili ya mahujaji hao ni Bi. Faiza Ahmed Omar na Bi. Rehema Ausi Rubaga kutoka kikundi cha Khidmati Islamiya pamoja na Bw. Masoud Juma Khamis kutoka Kikundi cha Ahlu Dawaa.
Hadi sasa mahujaji kumi na tano (15) kutoka Tanzania bado hawajulikani walipo na jitihada za kuwatafuta bado zinaendelea. Aidha, miili ya mahujaji kumi na tisa (19) kutoka Tanzania tayari imeshazikwa nchini Saudi Arabia.
Serikali ya Saudi Arabia inaendelea kutoa taarifa zaidi za kuwatambua mahujaji waliofariki dunia au kujeruhiwa katika ajali hiyo na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa itaendelea kutoa taarifa kwa umma kuhusu wahanga wa ajali hiyo kadri itakapokuwa inazipokea.
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,
Dar es Salaam
19 Oktoba, 2015
Sunday, October 18, 2015
Balozi Kasyanju awasilisha Hati za Utambulisho kwa Mtukufu Alexandre
![]() |
Mheshimiwa Balozi Irene F. M. Kasyanju akiwasilisha Hati za Utambulisho kwa Mtukufu Willem-Alexander Claus George Ferdinand, Mfalme wa Uholanzi. |
![]() |
Mheshimimwa Balozi Irene F. M. Mkwawa Kasyanju akiwasili kwenye Kasri la Mfalme wa Uholanzi |
![]() |
Balozi Irene F.M. Kasyanju akiwa katika picha ya pamoja na Mtukufu Willem-Alexander Claus George Ferdinand, Mfalme wa Uholanzi. |
Subscribe to:
Posts (Atom)