Thursday, October 22, 2015

Waziri Membe aagana na watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula akifungua hafla ya kumuaga Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe iliyoandaliwa na watumishi wa Wizara hiyo na kufanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere
Baadhi ya watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa waliohudhuria hafla hiyo
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Hassan Simba Yahya akitoa muhtsari wa shughuli chache ambazo Waziri Membe alizisimamia kwa umahiri mkubwa katika kipindi chake cha miaka 9 ya Uwazi wa Mambo ya Nje. Waliokaa ni Mhe. Membe na Balozi Mulamula ambao wanasikiliza kwa maikini shughuli zilizotekelezwa na Mhe. Waziri Membe.

Waheshimiwa Mabalozi wanaowakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali, Wakuu wa Idara/Vitengo na watumishi wakisikiliza kwa makini shughuli ambazo Mhe. Waziri Membe amezisimamia ipasavyo ikiwemo suala la maslahi ya watumishi.

Sehemu nyingine ya Waheshimiwa Mabalozi wanaowakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali, Wakuu wa Idara/Vitengo na watumishi wakisikiliza kwa makini shughuli ambazo Mhe. Waziri Membe amezisimamia ipasavyo ikiwemo suala la maslahi ya watumishi

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Mindi Kasiga akitangaza Tuzo na Zawadi mbalimbali ambazo zitatolewa kwa ajili ya Mhe. Waziri na Naibu Waziri na Wenza wao.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (kushoto) akisoma maneno yaliyoandikwa katika Tuzo ya Uongozi iliyotolewa na Wizara ya Mambo ya Nje na kukabidhiwa na Katibu Mkuu, Balozi Liberata Mulamula 

Waziri Membe akifurahia zawadi iliyotolewa na Wizara ya Mambo ya Nje.

Waziri Membe akipokea zawadi kwa niaba ya Mama Membe ambaye hakuweza kufika katika hafla hiyo. Bi. Amisa Mwakawago, Mkurugenzi Msaidizi katika Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu alikabidhi zawadi hiyo kwa niaba ya Wizara.

Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa, Mhe. Begum Karim Taj naye akikabidhi zawadi kwa Mhe. Waziri kwa niaba ya Waheshimiwa Mabalozi wa Tanzania

Naibu Katibu Mkuu, Balozi Hassan Simba Yahya akipokea zawadi kwa niaba ya Naibu Waziri, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim ambaye hakuweza kuhudhuria hafla hiyo kutokana na majukumu ya kitaifa.

Balozi Mulamula na Mama Mwakawago wakionesha zawadi ya Mama Mahadhi Juma Maalim.
Waheshimiwa Mabalozi wanaowakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali, Wakuu wa Idara/Vitengo na watumishi wakishuhudia zoezi la utoaji wa zawadi.

Waziri Membe akiongea na watumishi wa Wizara wakati wa hafla hiyo.
Mkuu wa Itifaki, Balozi Juma Maharage akitoa neno la shukrani katika hafla hiyo

Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy naye akiongea machache katika hafla hiyo

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati, Bw. Elibariki Maleko akionekana mtu mwenye furaha katika hafla hiyo, baada ya kutangazwa kuwa ameteuliwa kuwa Naibu Balozi wa Tanzania nchini Uganda. Wengine waliotangazwa kuwa Naibu Mabalozi ni Bi. Rosemary Jairo, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora ambaye anakuwa Naibu Balozi nchini Afrika Kusini na Bw. Andy Mwandembwa, Mkurugenzi Msaidizi katika Idara ya Itifaki ambaye anakuwa Naibu Balozi nchini Sweden.

Wakati wa maakuli. Mhe. Waziri akiwa ameshikilia sahani ya chakula na anyemfuatia ni Katibu Mkuu anayeonekana akichota chakula

Naibu Katibu Mkuu naye anajichotea chakula

Waheshimiwa Mabalozi nao wanajichotea chakula

Mhe. Waziri, Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu wakiwa katika picha ya pamoja na Waheshimiwa Mabalozi na Wakuu wa Idara/Vitengo

Mhe. Waziri, Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu wakiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Idara/Vitengo.

Mhe. Waziri, Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu wakiwa katika picha ya pamoja na Wasaidizi wa Waziri na Naibu Waziri.
Mhe. Waziri, Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu wakiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu.
Mhe. Waziri, Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu wakiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali.
Mhe. Waziri, Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu wakiwa katika picha ya pamoja na Waheshimiwa Mabalozi Wanawake.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.