Friday, October 30, 2015

APOKEA UONGOZI WA KILIMANJARO FC UBALOZINI NA KUKUBALI KUWA MLEZI WA TIMU HIYO

Mhe. Balozi Dora Msechu ameupokea Ubalozini  Ujumbe wa timu maarufu  ya soka ya watanzania waishio Sweden,  Kilimanjaro FC, ambao walikuja kumkabidhi Mhe. Balozi makombe waliyoshinda kwenye mashindano mbalimbali hapa Sweden. Mhe. Balozi Dora Msechu ameipongeza na kuishukuru Kilimanjaro FC kwa kuiwakilisha vyema nchi yetu kwenue fani ya michezo hapa Sweden na kuwahamasisha waongezee bidii zaidi na wasibweteke na mafanikio wanayoyapata.

Aidha, Mhe. Balozi Dora Msechu amekubali ombi la Kilimanjaro FC la kuwa Mlezi wa timu hiyo na kuahidi ushirikiano wake pale itakapowezekana.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.