Saturday, October 17, 2015

Rais Kikwete Azindua na kuweka jiwe la msingi ujenzi wa Bandari kubwa ya Bagamoyo.

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete wa tatu waliosimama kutoka kushoto, Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Pinda, na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete, Wengine kutoka kwa Rais Kikwete ni Balozi wa China nchini Tanzania, Mhe. Lu Youqing, Mtendaji Mkuu wa Mfuko Mkuu wa Akiba wa Oman, Mhe. Abdulsalam Murshidi, Mawaziri na viongozi mbalimbali wote kwa pamoja wakiwashuhudia Wawakilishi wa nchi za Tanzania,Oman na China wakiweka saini Makubaliano ya kujenga Bandari kubwa na ya kisasa ya Bagamoyo.
Wawakilishi hao wakionyesha nyaraka za mmakubaliano walizosaini na kubadilishana kama ishara ya wazi ya kuanza kwa ujenzi wa Bandari hiyo.
Mhe. Rais Kikwete akiweka rasmi jiwe la msingi la Bandari hiyo huku Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Pinda pamoja na viongozi wengine wa Oman, Tanzania na China  wakishuhudia.
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (katikati), Makamu wa Rais wa kampuni ya China Merchants Group, Dkt. Hu Jianhua (kushoto) na Mtendaji Mkuu wa Mfuko Mkuu wa Akiba wa Oman Mhe. Abdulsalam Murshidi,  (kulia) wakichanganya udongo,kama ishara ya kukubaliana kuanza rasmi ujenzi wa mradi huo wa Bandari.
Mhe. Rais akiwa katika picha ya pamoja mara tu baada ya kuweka jiwe la msingi na kuchanganya udongo.
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza muda mfupi kabla ya kutiliana saini na kuweka jiwe la msingi ili kubariki ujenzi wa Bandari ya kisasa ya Bagamoyo.

Katika uzinduzi huo Mhe. Rais amesisitiza serikali ihakikishe wananchi wote waliopisha eneo lao ili kujengwa kwa bandari hiyo wanalipwa fidia stahiki ikiwa ni pamoja na kujengewa nyumba nzuri za kisasa.
Waziri Mkuu wa Tanzania, Mhe. Mizengo Peter Pinda akizungumza katika mkutano huo.
Balozi wa China hapa nchini,Mhe. Lu Youqing akitoa hotuba fupi katika mkutano huo wa uzinduzi na uwekaji jiwe la msingi ili kujenga Bandari kubwa na ya kisasa ya Bagamoyo.
Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Samwel John Sitta akitoa hotuba yake kuhusu mambo ya uchukuzi,kabla ya kuzinduliwa kwa ujenzi wa Bandari hiyo.
Makamu wa Rais Mtendaji wa kampuni inayojenga mradi huo wa Bandari ya Bagamoyo ya China Merchants Group, Dkt. Hu Jianhua, akizungumza katika mkutano huo.
Mtendaji Mkuu wa Mfuko Mkuu wa Akiba wa Oman, Mhe. Abdulsalam Murshidi akizungumza na kutoa shukrani za kipekee kwa Rais Kikwete kwa kukubali kuzindua na kuweka jiwe la msingi la mradi huo.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Ukanda Maalum wa Uwekezaji (EPZA), Kanali Mstaafu Joseph Simbakalia akizungumza machache kuhusu mambo ya uwekezaji hapa nchini.
Mkuu wa Mkoa wa Pwani Eng. Evarist Ndikilo akitoa hotuba fupi wakati wa uzinduzi huo wa Bandari ya Bagamoyo.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Simba Yahya (kulia) akizungumza na  Mkuu wa Itifaki, Balozi Juma Mohammed Maharage wakati wa uzinduzi huo.
Mabalozi mbali mbali wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini, Wakurugenzi na Maofisa wa Wizara ya Mambo ya  Nje pamoja na Wananchi waliohudhuria kushuhudia uzinduzi wa ujenzi wa Bandari hiyo ya Bagamoyo.

Moja ya picha inayoonyesha ramani ya Bandari hiyo itakavyokua.

Mkutano huo ukiendelea.
 Mabalozi mbalimbali wakisikiliza kwa makini hotuba ya Mheshimiwa Rais.
Mabalozi mbalimbali wakisikiliza kwa makini hotuba ya Mheshimiwa Rais. 
 Mabalozi mbalimbali wakisikiliza kwa makini hotuba ya Mheshimiwa Rais.
 Kikundi cha ngoma cha kabila la Wakwere, kikitumbuiza katika uzinduzi huo.
==========================
PICHA NA: REUBEN MCHOME.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.