Thursday, October 15, 2015

Flyover ya TAZARA kuanza kujengwa mwezi ujao

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Mhandisi Patrick Mfugale (kulia) na Meneja Mkuu wa Kampuni ya SUMITOMO MITSUI, Bw. Ichiro Aok kutoka Japan wakiweka saini Mkataba wa kuanza ujenzi wa barabara ya juu (flyover) katika eneo la TAZARA. 

SUMITOMO MITSUI ni kampuni iliyoshinda zabuni ya kujenga barabra hiyo, ambao ujenzi wake unatarajiwa kuanza mwezi Novemba 2015 na kukamilika katika kipindi cha miaka mitatu. 

Wengine katika picha waliosimama watatu kutoka  kulia ni  Waziri wa Ujenzi na Mgombea wa nafasi ya Rais kupitia CCM, Dkt. John Pombe Magufuli, kushoto kwake ni Balozi wa Japan nchini Tanzania, Mhe. Masaharu Yoshida na Mwakilishi Mkazi wa JICA nchini Tanzania.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Mhandisi Patrick Mfugale (kulia) na Meneja Mkuu wa Kampuni ya SUMITOMO MITSUI, Bw. Ichiro Aok kutoka Japan wakibadilishana mikataba baada ya kuweka saini.
Waziri wa Ujenzi na Mgombea wa nafasi ya Rais kupitia CCM, Dkt. John Pombe Magufuli akiongea kabla ya uwekaji saini kukamilika. Dkt. Magufuli alieleza kuwa barabara hiyo itakapokamilika itakuwa ni ya kwanza ya aina yake katika nchi za Afrika Mashariki.
Mshauri mwelekezi wa kampuni hiyo Bw. Keigo Konno akionyesha jinsi mradi huo utakavyokuwa huku Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikianowa Kimataifa, Balozi Mbelwa Kairuki akifuatilia 
Sampuli ya barabra ya juu ya TAZARA itakavyokuwa baada ya ujenzi kukamilika.
Barabara ya juu
Waziri wa Ujenzi na Mgombea wa nafasi ya Rais kupitia CCM, Dkt. John Pombe Magufuli (kulia) akiteta jambo na Balozi wa Japan hapa nchini.
======================
PICHA NA: REUBEN MCHOME.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.